SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Mar 15, 2016

HASSAN KESY MAMBO SAFI SIMBA SC

Uongozi wa klabu ya Simba ya Dar es Salaam umesema umefika mbali katika suala lake na beki wake, Hassan Kessy na una imani kubwa ataendelea kubaki na kuitumikia klabu hiyo msimu ujao.

Makamu Rais wa Simba, Geofrey Nyange ‘Kaburu’ amesema wameanza mazungumzo na Kessy na yako katika hatua nzuri sana.

“Tuko katika hatua nzuri sana ya mazungumzo. Tumeanza mazungumzo kipindi sasa na tuna matumaini makubwa Kessy ataendelea kubaki Simba,” alisema Kaburu katika mahojiano na SALEHJEMBE.

KESSY
“Tunaamini Kessy tunamhitaji, naye ni kijana anayeipenda Simba. Hivyo tukifikia makubaliano, tutaingia mkataba na kuwataarifu.”

Kumekuwa na taarifa huenda Kessy ana mpango wa kujiunga na Yanga hali iliyoonyesha kuwaudhi baadhi ya mashabiki wa Simba.


Hata hivyo kumekuwa na mgawanyiko kuhusiana na beki huyo wa kulia mwenye uwezo wa kupiga krosi nyingi. Wengine wakisema abaki na wengine wakikubali aende zake.

FA WAMEAMUA HIVI KUHUSU DIEGO COSTA

costa

Licha ya Barry kusema kwamba Diego Costa hakumng’ata kwenye mechi ya weekend iliypita, FA imemkuta Costa na makosa na wamempa hadi Alhamisi akatoe maelezo.
Diego Costa ameonekana aking’ata Barry kwenye mechi yao ambapo hadi alama za meno zilionekana kwenye picha video. FA imetoa statement kwamba, “Ni tabia isiyokubalika, baada kuonyeshwa kati ya pili ya njano na bado anaonyesha tabio isiyokubalika uwanjani. Hadi Alhamisi saa 12 jioni ndio muda aliopewa kutoa maeleozo”
Kwa hiyo hadi Alhamisi ambapo Costa atatoa maelezo kuhusu hili tatizo na chama cha soka cha England kitatoa hukumu yake juu ya Costa.

TFF YASOGEZA MBELE MECHI MBILI ZA YANGA NA AZAM FC

MECHI mbili za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara zinazozihusu timu za Azam na Yanga zilizopangwa kufanyika mapema wki ijayo, zimeahirishwa.
Mechi hizo ni kati ya Mtibwa Sugar na Azam FC Jumanne ya Machi 22 Uwanja wa Manungu, Turiani, Morogoro na Yanga SC dhidi ya Mwadui FC Jumatano ya Machi 23, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam mwaka huu.
Sababu za kufutwa kwa mechi hizo ni kupisha ratiba ya timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars katika mechi za kufuzu Kombe la Mataifa ya Afrika 2017.
Kiungo wa Yanga, Deus Kaseke akipasua katikati ya wachezaji wa Azam FC, Serge Wawa (kulia) na Farid Mussa (kushoto)

taifa Stars itakuwa na mchezo wa kufuzu AFCON Kundi G dhidi ya Chad mjini N’jamena Machi 25, kabla ya timu hizo kurudiana Machi 28, Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Na baada ya mechi za mwishoni mwa wiki za michuano ya klabu barani, Afrika wachezaji wa Stars wanatarajiwa kukusanywa Jumapili kabla ya safari Jumanne kuelekea Chad.
Yanga SC baada ya ushindi wa 2-1 kwenye mchezo wa kwanza wa Raundi ya Kwanza Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya APR Jumamosi mjini Kigali, watarudiana na timu hiyo ya jeshi la Rwanda Jumamosi wiki hii Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Na Azam FC baada ya kushinda 3-0 mjini Johannesburg, Afrika Kusini dhidi ya wenyeji Bidvest Wits katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Kwanza Kombe la Shirikisho Afrika, watarudiana na timu hiyo Jumapili, Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
Pamoja na hayo, Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara inatarajiwa kuendelea leo kesho na mwishoni mwa wiki.
Azam FC wataikaribisha Stand United kesho Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
Kwa Stand United ikiwa na pointi 30 baada ya kucheza mechi 22 haina nafasi ya ubingwa na wala haimo kwenye hatari ya kushuka daraja, hivyo huo ni mchezo ambao hauwatii ‘presha’ hata kidogo.
Lakini Azam FC ikiwa nafasi ya tatu kwa pointi zake 47 za mechi 20 katika mbio za ubingwa dhidi ya Yanga yenye pointi 50 za mechi 21 na Simba iliyo kileleni kwa pointi zake 54 za mechi 23 – inahitaji ushindi ili kujiimarisha.  
Simba itashuka tena dimbani Jumamosi kucheza na Coastal Union Jumamosi Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.