SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

May 28, 2016

NGASSA AITAJA TIMU INAYO MWITAJI VPL

Na Haji balou
Pamoja na uongozi wa Free State Stars
ya Afrika Kusini kumzuia kiungo wake
mshambuliaji, Mrisho Ngassa kumtoa kwa
mkopo, nyota huyo amewatoa hofu
mashabiki wa Yanga na kuwaambia siku si
nyingi anarejea kwenye klabu hiyo.

Ngassa ameitoa kauli hiyo muda mfupi
baada ya kuwasili nchini kisha kutazama
mechi ya fainali ya Kombe la FA kati ya
Yanga na Azam FC kwenye Uwanja wa
Taifa, Dar ambapo Yanga ilishinda mabao
3-1.

Ngassa alijiunga na Free State inayoshiriki
Ligi Kuu Afrika Kusini, mwaka jana baada
ya mkataba wake kumalizika Yanga.
Ngassa amesema viongozi wa Yanga ndio waliowafuata Free State kwa ajili ya
kumuomba kwa mkopo ili aiongezee
nguvu timu hiyo katika hatua ya makundi
ya Kombe la Shirikisho Afrika.

NGASSA AITAJA TIMU INAYO MWITAJI VPL

Na Haji balou
Pamoja na uongozi wa Free State Stars
ya Afrika Kusini kumzuia kiungo wake
mshambuliaji, Mrisho Ngassa kumtoa kwa
mkopo, nyota huyo amewatoa hofu
mashabiki wa Yanga na kuwaambia siku si
nyingi anarejea kwenye klabu hiyo.

Ngassa ameitoa kauli hiyo muda mfupi
baada ya kuwasili nchini kisha kutazama
mechi ya fainali ya Kombe la FA kati ya
Yanga na Azam FC kwenye Uwanja wa
Taifa, Dar ambapo Yanga ilishinda mabao
3-1.

Ngassa alijiunga na Free State inayoshiriki
Ligi Kuu Afrika Kusini, mwaka jana baada
ya mkataba wake kumalizika Yanga.
Ngassa amesema viongozi wa Yanga ndio waliowafuata Free State kwa ajili ya
kumuomba kwa mkopo ili aiongezee
nguvu timu hiyo katika hatua ya makundi
ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HABARI NJEMA KWA WAKAZI WA TANGA BAADA YA TIMU ZAO TATU KUSHUKA DARAJA

Na Haji balou
KAIMU Katibu Mkuu wa Coastal Union,
Salim Bawazir amesema timu hiyo sasa
itakuwa chini ya usimamizi wa Nassor
Binslum pamoja na uongozi wa Chama
cha Soka Mkoa wa Tanga (TRFA) kwa
ajili ya kuiwezesha kushiriki vyema Ligi
Daraja la Kwanza (FDL) ili irejee Ligi
Kuu Bara.

Akizungumza na Mwanaspoti Bawazir
alisema: “Tumepata funzo kubwa,
kugawanyika kwetu ndiko
kulikotushusha daraja, sasa hatutakubali
mambo hayo tena, tutahakikisha Coastal
inashiriki kikamilifu Ligi Daraja la
Kwanza na msimu ujao tutarejea Ligi
Kuu Bara.”

Bawaziri alisema BinSlum na TRFA
watashiriki kikamilifu katika suala zima
la usajili wa wachezaji, kocha mwenye
ujuzi na uzoefu na kuilea timu ikiwa
kwenye kanda itakayopangiwa.

“Tunatambua kwamba FDL ni ngumu
kuliko hata ligi kuu ili uweze kufuzu ni
lazima timu iwe na mikakati kabambe
na si ubabaishaji,” alisema Bawazir.