SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Mar 3, 2016

BAADA YA ISIHAKA KUFUNGIWA SIMBA HAYA NDIO ALIYOSEMA HAMISI KIIZA

Na Haji balou


Mshambuliaji wa Simba, Hamisi Kiiza naye yuko katika wakati mgumu baada ya kuandika mambo mtandaoni akionyesha kuupinga uongozi wa Simnba kumsimamisha nahodha wake, Hassan Isihaka.

Simba ilitangaza kumfungia Isihaka kwa muda usiojulikana kutokana na kitendo chake cha kumtolea mwalimu wake, Jackson Mayanja maneno yasiyo ya kiungwana.


Taarifa kutoka ndani ya Simba zimeeleza, Kiiza ameanza kujitetea akitupia lawama magazeti. Kwamba yaliandika na kumchafua Isihaka.

Lakini hali halisi inaonyesha haikuwa hivyo kwani yeye alianza kutupia mtandaoni hata kabla ya magazeti kuandika.

Presha imekuwa kubwa kwa Kiiza baada ya uongozi kumtaka aombe radhi. 

Lakini presha ikawa kubwa zaidi baada ya mhusika mwenyewe, Isihaka kuona amefanya kosa na kuamua kumuomba radhi kocha wake na uongozi.


Kiiza alitupia maneno kwenye mtandao wa Instagram akidai Isihaka anachafuliwa. Jambo lililoonyesha wazi alikuwa akiupinga uongozi. Lakini hakueleza kama alikuwa akiunga mkono nahodha huyo kinda amjibu kocha wake hovyohovyo.

ALICHOSEMA MANEGER WA HASSAN KESSY KUHUSU MKATABA MPYA SIMBA

Na Haji balou
Meneja wa Hassan Kessy amesema bado anahitaji mchezaji huyo aendelee kuitumikia Simba.
Athuman Tippo amesema Kessy hadi sasa ni mchezaji wa Simba ingawa mkataba wake unaendea ukingoni.

Lakini wanatoa nafasi kubwa kwa Simba kuingia naye tena mkataba kama wanamhitaji. “Ni suala la kukubaliana. Kama Simba watakuwa tayari, mimi naona ni vizuri  Kessy abaki Simba.

Hata hivyo itategemea tutafikiaje makubaliano,” alisema Tippo
mchezaji wa zamani wa Coastal Union na Milambo ya Tabora.
Kauli hiyo ya Tippo maarufu kama Zizzou Fashion inakuja siku moja baada ya Kocha Mkuu wa Simba, Jackson Mayanja kusema Kessy kama ataendelea kusumbua kuhusiana na suala la kusaini,
basi anaweza akaenda zake.

MATOKEO YA MECHI ZA JANA LIGI KUU ENGLAND

TIMU ya Liverpool imeichapa mabao
3-0 Manchester City katika mchezo
wa Ligi Kuu ya England usiku huu
Uwanja wa Anfiled.

Ushindi huo ni sawa na kisasi cha
kufungwa kwa penalti 3-1 katika
fainali ya Kombe la Ligi, maarufu
kama Capital One Cup Februari 28,
Uwanja wa Wembley baada ya sare
ya 1-1.

Katika mchezo wa leo, mabao ya
Liverpool yamefungwa na Adam
Lallana dakika ya 34, James Milner
dakika ya 41 na Roberto Firmino
dakika ya 57.

Nyota wa Manchester United, Juan
Mata akidjangilia baada ya kuifungi
timu yake pekee katika ushindi wa 1-0 victory over Watford
Mchezo mwingine wa Ligi Kuu ya
England usiku huu, Manchester United imeendeleza wimbi la ushindi baada ya kuifunga 1-0 Watford, bao pekee la Juan Mata dakika ya 83 Uwanja wa Old Trafford.

Arsenal imefungwa 2-1 nyumbani na
Swansea City Uwanja wa Emirates
katika mchezo mwigine wa ligi hiyo.
Mabao ya Swansea yamefungwa
na Wayne Routledge dakika ya 32
na Ashley Williams dakika ya 74,
wakati la Gunners limefungwa na Joel Campbell dakika ya 15.
Nahodha wa Swansea City
akimtungua kipa wa Arsenal, Petr
Cech katika mchezo wa Ligi ya
England baada ya krosi ya Gylfi
Sigurdsson Uwanja wa
Emirates.

Stoke City imeilaza 1-0 Newcastle
United, bao pekee la Xherdan Shaqiri
dakika y 80 Uwanja wa Britannia.

West Ham United imeilaza 1-0 Tottenham Hotspur, bao pekee la Michail Antonio dakika ya saba.