SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Mar 21, 2015

MICHAEL CARRICK ASAINI MKATABA MPYA MAN UNITED

KIUNGO Michael Carrick amepata bonge la furaha Manchester United kuelekea mechi na mahasimu wao wakubwa, Liverpool baada ya kusaini Mkataba mpya mwaka mmoja Old Trafford.
Taarifa ya Manchester United iliyotumwa BIN ZUBEIRY imesema kwamba kiungo huyo anabaki kuwa mchezaji muhimu katika kikosi cha Louis van Gaal licha ya kukosa miezi miwili na nusu ya kwanza ya msimu kwa sababu ya kuwa maumivu ya kifundo cha mguu, alichoumia katika mazoezi ya kwanza ya Mholanzi huyo Agosti mwaka jana.
Van Gaal amempa Unahodha Msaidizi Carrick, baada ya kiungo huyo kuonyesha mchezo mzuri na kutengeneza bao la kwanza lililofungwa na Marouane Fellaini mwishoni mwa wiki katika ushindi wa 3-0 nyumbani dhidi ya Tottenham kabla ya yeye mwenyewe kufunga.
Carrick has made 17 appearances for Manchester United this season 
Michael Carrick ameichezea United mechi 17 msimu huu baada ya kuwa nje mwanzoni mwa msimu kwa sababu ya maumivu ya enka

Mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 33, aliyejiunga na United kutoka Spurs kwa ada ya uhamisho ya Pauni Milioni 18.6 mwaka 2006, alitarajiwa kumaliza Mkataba wake mwishoni mwa msimu.

NGASSA APATA ‘GONJWA LA AJABU’ YANGA SC NA LEO HAWEZI KUCHEZA DHIDI YA MGAMBO

Na Mahmoud Zubeiry, TANGA
KIUNGO mshambuliaji wa Yanga SC, Mrisho Khalfan Ngassa amepata ugonjwa ambao yeye mwenyewe hauelewi na leo anaweza kukosa mechi dhidi ya Mgambo Shooting.
Yanga SC wanacheza na JKT Mgambo leo Uwanja wa Mkwakwani, Tanga katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, lakini Ngassa ambaye ni tegemeo kweli la timu hiyo hali yake tete.
Ngassa amesema kwamba alimaliza vizuri mechi dhidi ya Kagera Sugar Jumatano, Yanga SC ikishinda 2-1, lakini Alhamisi mambo yakageuka.
Mrisho Ngassa ameumia 'kiajabu ajabu' na leo hatacheza dhidi ya Mgambo Shooting Uwanja wa Mkwakwani, Tanga

“Nilikuwa napanda basi jana kwa safari ya kuja Tanga, mguu ukaanza kuuma. Maumivu yakazidi nikiwa kwenye basi. Tulipofika nikamuambia dokta. Ameanza kuhangaika nao tangu hapo, lakini wapi, hali bado tete,”alisema Ngassa jana usiku.
“Nimejaribu kuweka barafu kupoza maumivu, lakini hali bado si nzuri na sijui tatizo ni nini,”amesema Ngassa.
Wazi Yanga SC kumkosa Ngassa leo dhidi ya Mgambo ni pigo kubwa, kwa sababu mchezaji huyo amekuwa chachu ya ushindi katika klabu hiyo.
Wakati Yanga SC itaingia kwenye mchezo wa leo na kumbukumbu ya ushindi wa 2-1 dhidi ya Kagera, Mgambo nao katika mchezo uliopita waliifunga 2-0 mjini hapa.


KURASA ZA MWANZO NA ZA MWISHO ZA MAGAZETI YA MICHEZO LEO IJUMAA

.
.
.
.
.
.
.
.