SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Jun 4, 2015

NOOIJ ABEBA 23 TAIFA STARS SAFARI YA ADDIS KUFUATA DAWA YA 'KUNYONGA' MAFARAO

Na Baraka Kizuguto, DAR ES SALAAM
KOCHA Mkuu wa timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) Mart Nooij ametangaza kikosi cha wachezaji 23 watakaoondoka leo jioni kuelekea Addis Ababa nchini Ethiopia kuweka kambi ya wiki moja kujiandaa na mchezo dhidi ya Misri
Akizungumza na Waandishi wa Habari, Mholanzi huyo amesema watatumia kambi ya Ethiopia kujiandaa na mchezo wa Misri, vijana wapo katika hali nzuri na wameahidi kupambana kuhakikisha wanafanya vizuri katika mchezo huo.
Mchezo kati ya Misri na Tanzania unatarajiwa kuchezwa Juni 14, katika uwanja wa Borg El Arab jijini Alexandria, ikiwa ni mchezo wa kuwania kufuzu kwa fainali za Mataifa Afrika (AFCON) mwaka  2017.
Kocha Mart Nooij amechukua wachezaj 23 wa kuivaa Misri

Kikosi cha Stars kinaondoka saa 11 jioni kwa Shirika la ndege la Ethiopia ambapo inatarajiwa kuwasili jiji la Addis Ababa majira ya saa 1 jioni kwa saa za Afrika Mashariki.
Wachezaji wanaosafiri kuelekea nchini Ethiopia ni Deogratias Munish, Aishi Manula, Mwadini Ali, walinzi Shomari Kapombe, Oscar Joshua, Erasto Nyoni, Nadir Haroub, Aggrey Morris, Mwinyi Haji, Salum Mbonde na Juma Abdul.
Wengine ni Mwinyi Kazimoto, Abdi Banda, Salum Telela, Frank Domayo, Jonas Mkude, Said Ndemla, washambuliaji Saimon Msuva, John Bocco, Thomas Ulimwengu, Mbwana Samatta, Mrisho Ngassa na Juma Liuzio.
Msafara wa Taifa Stars utaongozwa na Wajumbe wa Kamati ya Utendaji, Vedastus Lufano na Geofrey Irick Nyange “Kaburu”.
Naye mjumbe wa kamati ya Utendaji  ya TFF Vedastus Lufano amesema timu inakwenda kuweka kambi Ethiopia kwa ajili ya kupambana katika mchezo dhidi ya Misri.
Kikosi kingine cha timu ya Taifa kitaondoka nchini siku ya jumamosi kuelekea nchini Rwanda kucheza mchezo wa kirafiki na timu ya taifa ya Rwanda katika kumbukumbu ya mauaji ya Kimbali.
Kocha Salum Mayanga ataondoka na kikosi cha wachezaji 18 kuelekea nchini Rwanda kwa ajili ya mchezo huo wa kirafiki, akisaidiwa na kocha Bakari Shime.
Wachezaji watakaondoka kwenda Rwanda ni Peter Manyika, Said Mohamed, Emmanuel Semwanda, Joram Mgeveke, Hassan Isihaka, Gadiel Michael, Hassan Dilunga, Rashid Mandawa, Atupele Green, Kelvin Friday, Hassan Kessy, Ibrahim Hajibu, Malimi Busungu, Mudathir Yahya, Deus Kaseke, Andre Vicent, Amri Kiemba na Mohamed Hussein.

MANCHESTER UNITED IMEWAPIKU BARCELONA NA BAYERN KUMNASA MCHEZAJI HUYU

11a
Usajili ndio mpango mzima hivi sasa huko Ulaya. Manchester united imewashinda Bayern Munich na Barcelona kwenye vita ya kupaya saini ya mchezaji wa Borussia Dortmund.
Mchezaji huyo ambae anacheza sehemu ya midfield amesakubaliana mambo ya msingi na Manchester united. Gundogan anatarajiwa   kutangazwa na Manchester united kuwa mchezaji mpya wa club hiyo.
11

MAKOMBE 24 KABLA YA KUONDOKA, JE BABU XAVI ANAWEZA KUONGEZA MOJA JUMAMOSI?


Wakati Xavi Harnandez ,35, anajiandaa na kustaafu rasmi baada ya kuitumikia Barcelona kwa miaka 17 ya maisha yake, swali je, atafanikiwa kuongeza kombe jingine hapo keshokutwa.

Barcelona inashuka dimbani mjini Berlin, Ujerumani kucheza fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Juventus ya Italia.
Utaona katika picha hiyo hapo juu, Xavi akiwa amezungukwa na makongwe 24 aliyowahi kubeba akiwa na Barcelona kwa miaka 17.
Hapo kuna makombe manane ya La Liga, matatu ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, mawili ya UEFA Super Cups, matatu ya Copa del Reys, sita ya Spanish Supercups na mawili ya Kombe la Dunia kwa klabu.


Swali ni kwamba ataweza kubeba kombe lake la 25 kabla ya kuondoka Barcelona?

MWADUI YA JULIO YAIBOMOA TENA MBEYA CITY, YAMTWAA STRAIKA PAUL NONGA

Kama ulidhani Mwadui Football club wanafanya utani, basi ujue unajidanganya maana sasa wamemsajili straika tegemeo wa Mbeya City, Paul Nonga.

Nonga amemsajili Nonga ambaye aliwahi kuichezea ikiwa daraja la tatu klabla ya kuondoka na kujiunga na JKT Oljoro ya Arusha.
Nonga amejiunga leo na Mwadui FC ingawa haijaelezwa mkataba huo utakuwa ni wa muda gani kama ni mwaka mmoja au miwili.
Saa chache zilizopita, Mwadui FC inayofundishwa na Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ imemsajili beki wa Mbeya City, Anthony Matogolo.
 
Benchi la ufundi la matajiri hao wa Mwadui kutoka mkoani Shinyanga linaonyesha limepania kujiimarisha mara tu baada ya kupanda Ligi Kuu Bara.
Mwadui FC ni kati ya timu zilizokuwa katika daraja hilo katika miaka ya 1980. Sasa imerudi tena na inaonekana imepania kuleta ushindani hasa.

Jun 2, 2015

AZAM FC YAWARUHUSU SIMBA KUMCHUKUA BEKI HUYU

Na Prince Akbar, DAR ES SALAAM
AZAM FC imewataka Simba SC kuwasilisha maombi ya kumchukua beki David Mwantika (pichani kushoto) kama kweli kweli wanamuhitaji.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Saad Kawemba ameiambia BIN ZUBEIRY jana kwamba, Mwantika ana Mkataba na klabu hiyo hadi mwishoni mwa mwaka.
“Tunasikia sikia tu kwenye vyombo vya Habari kwamba Simba wanamtaka Mwantika, sisi hatuna tatizo, Simba SC wao waje tuzungumze,” amesema.
Mwantika alisajiliwa na Azam FC miaka miwili iliyopita kutoka Prisons ya Mbeya kwa Mkataba wa kudumu- kwamba atakapoacha mpira, atahamia kufanya kazi kwenye kampuni ya Bakhresa Group Limited, wamiliki wa klabu hiyo.
Maana yake- Simba SC nao kama wanataka kumchukua beki huyo mwenye miraba minne, wawe tayari kumhakikishia ajira nyingine baada ya soka.
Mwantika mwenyewe alipoulizwa kuhusu hilo alisema; “Ni kweli mimi ni mchezaji halali wa Azam, kama Simba wananitaka kweli, wakazungumze na Azam FC, sioni tatizo,”amesema.

BERBATOV 'AFUNGASHIWA VIFURUSHI' VYAKE AS MONACO

MSHAMBULIAJI wa zamani wa kimataifa wa Bulgaria, Dimitar Berbatov anatafuta timu ya tatu ya kujiunga nayo England, baada ya kutemwa na AS Monaco ya Ufaransa.
Berbatov alijiunga na vigogo hao wa Ligue 1 Januari mwaka 2014 kutoka Fulham ya England na atakumbukwa kwa kufunga bao la pili katika ushindi wa 3-1 kwenye dhidi ya Arsenal kwenye Ligi ya Mabingwa msimu huu.
Pamoja na hayo, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 34 sasa yuko huru baada ya kuachwa na Monaco, iliyomaliza katkka nafasi ya tatu kwenye Ligue 1 msimu huu.
Ligue 1 giants AS Monaco have confirmed they have released Bulgarian striker Dimitar Berbatov
Vigogo wa Ligue 1, AS Monaco wamethibitisha kumtema Dimitar Berbatov

Katika taarifa kwenye tovuti ya klabu hiyo, Makamu wa Rais wa Monaco, Vadim Vasilyev, amesema; "Dimitar Berbatov ameonyesha kipaji chake chote na soka babu kubwa. Dhahiri ni miongoni mwa washambuliaji wakubwa waliojiunga na AS Monaco. Tunajivunia alicholeta katika klabu na tunamtakia kila la heri aendako,".'
Berbatov alikuwa na wakati mzuri akichezea klabu ya Tottenham Hotspur kabla ya kujiunga na Manchester United  iliyomsaini kwa dau la Pauni Milioni 30.75 mwaka 2008.
Amefunga mabao 48 katika Ligi Kuu ya England katika misimu minne chini ya kocha Sir Alex Ferguson, kabla ya kuhamia Fulham, ambako alicheza kwa msimu mmoja na nusu.
He scored 48 Premier League goals in four seasons for Manchester United after arriving in 2008
Before his move to the Red Devils, he enjoyed a successful spell with Tottenham
Mkongwe wa umri wa miaka 34 aling'ara Ligi Kuu England kabla ya kuhamia Ufaransa ambako nako ameacha kumbukumbu nzuri

HANS POPPE: SIMBA SC HATUSAJILI ‘BENDERA FUATA UPEPO’

Na Princess Asia, DAR ES SALAAM
MWENYEKITI wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe (pichani juu) amesema kwamba ‘hawasajili bendera fuata upepo’, bali wanasajili kulingana na mahitaji ya timu yao.
Akizungumza na BIN ZUBEIRY jana, Poppe amesema kwamba watu wanapenda kuona Simba SC inasajili wachezaji wanaovuma, lakini huo si mpango wa uongozi wa klabu.
“Sisi tuna kikosi kizuri ambacho kilimaliza msimu uliopita vizuri. Sasa tunachofanya ni kukiongezea nguvu kikosi kwa mujibu wa tathmini ya kitaalamu. Tunasajili mchezaji ambaye tunamuhitaji, siye anayevuma,”amesema.
Aidha, Poppe ambaye na Kapteni wa zamani wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), amesema kwamba mkakati mzima na mpango wa usajili uko vizuri.
“Kila kitu kiko vizuri, tunafanya mambo yetu kimya kimya, hatushindani na mtu kusajili, tutakuja kushindana mpira uwanjani, hao wanaosajili wanaovuma, acha waendelee, sisi tunasajili kwa mujibu wa mahitaji yetu,”amesema.
Hadi sasa, tayari Simba SC imesajili wachezaji watano wapya, ambao ni kipa Abraham Mohammed kutoka JKU ya Zanzibar, mabeki Samih Haji Nuhu kutoka Azam FC, Mohammed Fakhi kutoka JKT Ruvu na kiungo Peter Mwalyanzi kutoka Mbeya City.    
Wapinzani wao wa jadi, Yanga SC wamesajili wachezaji wanne tu ambao ni kipa Benedicto Tinocco kutoka Kagera Sugar, beki Mwinyi Hajji Mngwali kutoka KMKM na washambuliaji Malimi Busungu wa JKT Mgambo na Deus Kaseke wa Mbeya City.

MBEYA CITY YASAJILI 'STRAIKA'


Na Mwandishi Wetu, MBEYA
MSHAMBULIAJI wa kutumainiwa wa Ndanda FC ya Mtwara, Gideon Brown (pichani juu) amesaini Mkataba wa mwaka mmoja na nusu kujiunga na Mbeya City FC ya Mbeya.
Brown amechagua kujiunga na kikosi cha Juma Mwambusi katika msimu ujao huku akiweka kando ofa kadhaa, alizopata kutoka klabu mbalimbali za Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara alizopata hapo kabla.
Akizungumza mara baada ya kusaini Mkataba huo mapema jana kwenye ofisi za MCC FC zilizopo jengo la Mkapa Hall mjini Mbeya, Brown alisema kuwa limekuwa jambo zuri kwake kujiunga na timu ambayo inaweza kumpa mafanikio nje na klabu zingine zilizozoeleka.
“Watu wengi wengi wanaamini kuwa huwezi kufanikiwa bila kupita kule, binafsi nahisi ni tofauti kwa sababu kipaji kinaweza kuonekana popote,imani yangu nitafanikiwa hapa, City ni timu nzuri na ina mipango ya  ya kweli, nataka kufanya kazi kwa kiwango kikubwa na imani yangu sitawaangusha wale wote wenye mapenzi na timu hii, najaua nitakuwa chini ya mwalimu Mwambusi, huyu ni kocha ambaye siku zote nimekuwa na kiu ya kufanya nae kazi, hili limetimia sasa” alisema  mshambuliaji huyo.
Msimu uliopita Brown alikuwa moja ya wachezaji muhimu kwenye kikosi cha Ndanda Fc akicheza michezo  21 akiwa kwenye kikosi cha kwanza, na kuifungia timu hiyo ya Mtwara jumla ya mabao 5, awali mshambuliaji  huyu amewahi kukupiga kwenye timu za KMKM ya  Zanzibar na kuisaidia kutwaa taji la ligi kuu ya visiwani humo pia amecheza kwenye kikosi cha Rhino ya Tabora na Moro United.