SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Sep 1, 2016

KIUNGO MTANZANIA APATA TIMU AFRIKA KUSINI

Na Haji balou
KIUNGO wa zamani wa
Simba SC na Azam FC,
Abdulhalim Humud ‘Gaucho’
amejiunga na klabu ya Real
Kings FC ya Ligi Daraja la
Kwanza Afrika Kusini.

Humud ambaye msimu
uliopita alichezea Coastal
Union ya Tanga iliyoshuka
daraja kutoka Ligi Kuu ya
Vodacom Tanzania Bara,
amesaini mkataba wa
mwaka mmoja kujiunga na
timu ya Durban, Kwazulu-
Natal.

Real Kings walipanda Ligi
Daraja la Kwanza mwaka
huu na wakafanikiwa kufika
fainali ya ligi ya ABC
Motsepe League.

Wakala aliyefanikisha
Humud kusaini Real Kings,
amesema leo kwa simu
kutoka Durban kwamba ana
matumaini mchezaji huyo
atafanya vizuri Afrika
Kusini.

Jul 15, 2016

JORDAN IBE AIHAMA LIVERPOOL

Na Haji balou
Timu ya Bournemouth imekamilisha usajili wa winga wa Liverpool Jordan Ibe kwa Ada ya Euro million 15.

Ibe amesaini mkataba wa miaka minne ya kuitumikia Timu hiyo inayotumia uwanja wa Vitality.

LUIS NANI ASAINI TIMU HII HAPA LA LIGA

Na Haji balou
Mchezaji wa zamani wa Manchester United ya Uingereza Luis Nani amesaini mkataba mkataba wa miaka mitatu ya kuitumikia Valencià ya Hispània.

Nani amesajiliwa kwa Euro million 8.5 akitokea katika klabu ya Fenerbahce ya uturuki ambayo aliisaidia kushika nafasi ya pili nyuma ya mabingwa Besiktas.

Jul 14, 2016

MHISPANIA WA AZAM FC ATAJA TOFAUTI YA MAKIPA WA HISPANIA NA TANZANIA

Na Haji Balou
KOCHA Mkuu wa makipa wa Klabu
Bingwa ya Afrika Mashariki na Kati Azam
FC, Jose Garcia, amesema kuwa makipa
aliowakuta ndani ya timu hiyo wapo
vizuri.

Kocha huyo hakusita kuelezea utofauti
wa makipa kutoka Tanzania na Hispania
mara baada ya kuwaona wa Azam FC,
ambapo alisema magolikipa wa hapa
wana nguvu sana lakini wanakosa mbinu.

“Watanzania wana nguvu sana, ila
wanakosa mbinu, lakini kwa upande wa
kule Hispania wako vizuri zaidi na
wanazo mbinu, na hicho ambacho
nimeongea na wenzangu ili tuweze
kukifanyia kazi,” alimalizia kocha huyo
mwenye umbile kubwa na mrefu
atayesaidiana majukumu hayo na Idd
Abubakar.

Ukiondoa makipa wa Azam FC, Aishi
Manula, Mwadini Ally na Metacha Mnata
aliyepandishwa kutoka timu ya vijana na
Kauju Agustino wa Azam B wanaendelea
kufanya maandalizi ya msimu mpya, kuna
makipa wengine wawili wa kigeni
wanawania nafasi moja ya kusajiliwa,
Daniel Yeboah (Ivory Coast) na Juan
Jesus Gonzalez (Hispania).

CHANZO WWW.AZAMFC.COM

WACHEZAJI KUMI WALIO KAMILISHA USAJILI LIGI KUU BARA

Na Haji Balou
AKlabu za Ligi Kuu Bara kwa ajili ya msimu
mpya ligi kuu bara 2016/2017, kwa kuboresha
baadhi ya maeneo yenye mapungufu na
kuyaongezea nguvu.

Atupele Green (ametoka Ndanda kwenda
JKT Ruvu)
Mfungaji bora wa kombe la shirikisho FA na
klabu ya Ndanda kwa msimu uliomalizika
amemwaga wino kuitumikia JKT Ruvu kwa
msimu mpya, kwa uwezo wake mkubwa wa
kufumania nyavu atakua msaada mkubwa
kwa JKT Ruvu.

Mohamed Mkopi (ametoka Prisons kwenda
Mbeya City)
Moja ya matatatizo msimu uliomalizika
Mbeya city ni ubutu wa safu ya ushambuliji,
Mkopi ni mzuri kwenye kufunga na
kutengeneza nafasi za kufunga kwa wenzake,
kwa usajili huu Mbeya City watafaidika nao.

Hassan Kessy (ametoka Simba kwenda
Yanga)
Amesaini kuitumikia Yanga kwa miaka miwili,
usajili huu ni bora kwa Yanga sababu upande
wa beki ya kulia Yanga imekua aina mpinzani
kwa muda mrefu Juma Abduli amekuwa
akitawala, ujio wa Kessy Yanga utaleta
upinzani sahihi kwenye nafasi hiyo.

Shiza Kichuya (ametoka Mtibwa kwenda
Simba)
Mmoja wa viungo bora msimu uliomalizika
akiwa Mtibwa, amejiunga na Simba kwa ajili
ya msimu mpya, uwezo wake mkubwa
uwanjani utakuwa faida kwa Simba hapa ni
kama Simba imepiga bao kwa usajili wa
Kichuya.

Muzamili Yassin (ametoka Mtibwa kwenda
Simba)
Hakuna shaka na uwezo wa Muzamili ni
mmoja wa viungo bora chipukizi kwa msimu
uliomalizika, huu ni moja ya usajili bora
kwenda Simba kutokana na uwezo mkubwa
wa Muzamili kutengeneza nafasi za kufunga
kwa wenzake na ndicho kitu Simba walikuwa
wamekosa kwa kipindi kirefu tangu kuondoka
kwa Boban.

Edo Christopher (ametoka Toto kwenda
Kagera)
Kagera wanazidi kujiimarisha kwa ajili ya
msimu mpya baada ya kuponea kushuka
daraja msimu uliomalizika, ujio wa Edo
kwenye eneo la ushambuliaji utaongeza
chachu kutokana na uwezo wake wa kufunga
na uzoefu kwenye ligi kuu bara.
Juma Mahadhi (ametoka Coastal kwenda
Yanga)
Ni usajili bora kufanywa na Yanga kwa msimu
ujao, uwezo wake mkubwa kwenye mechi
dhidi ya Mazembe kwenye kombe la
shirikisho umeleta faraja kubwa kwa wapenzi
wa Yanga pamoja na wanachama.

Aziz Gilla (ametoka Mgambo JKT kwenda
JKT Ruvu)
JKT Ruvu wanajiimarisha kwenye maeneo
mbali mbali kwa ajili ya msimu mpya, ujio wa
winga mpya Aziz Gilla utakuwa msaada
kwenye timu yao hasa nidhamu yake na
uhamasishaji wa wenzake.

Vicent Andrew (ametoka Mtibwa kwenda
Yanga)
Amesaini Yanga kwa mkataba wa miaka
miwili licha ya ugumu wa namba kwenye
eneo analo cheza kwa sababu imejaza watu
wenye uzoefu lakini ni moja ya usajili bora
sababu ana uwezo wa kucheza namba zaidi
ya tatu uwanjani.

Dany Mrwanda (ametoka Majimaji kwenda
Kagera)
Kikubwa ni uzoefu wake kwenye ligi utakuwa
msaada mkubwa kwa Kagera timu ambayo
inajiimarisha kwa msimu mpya.

Jul 7, 2016

VALDEZ ASAINI TIMU HII HAPA ENGLAND

Na Haji balou
Kipa wa zamani wa Fc barcelona Na Manchester united Victor Valdez amesaini mkataba wa miaka miwili Na klabu ya Middlesbrough ya nchini England.

Valdez mwenye umri wa miaka 34 amekuwa Na wakati mgumu tangu atue Manchester united akitokea  Barcelona baada ya kukosa nafasi ya kucheza katika klabu hiyo.

Kupitia account yake ya Twitter Valdez aliandika hivi  “Very Proud to be part of Middlesbrough.

“A new challenge for me from today!”.

MANYIKA JR AZUNGUMZIA SKENDO YA MAPENZI INAYOMKABILI

Na Haji balou
Mchezaji wa timu ya Simba Peter manyika Jr amesema yeye ni mmoja kati ya wachezaji wenye nidhamu isipokuwa mashabiki wengi wanamsema kutokana Na jinsi wanavyo mwona.

Manyika alisema hayo alipokuwa akihojiwa Na Sauda mwilima kupitia kipindi cha Mcheza kwao kinachorushwa na channeli ya Star Tv.

Pia alipoulizwa kuhusu skendo za mapenzi zinazo mkabili Manyika alisema kuwa "Siku zote ukiwa maarufu watu watazungumzia sana mahusiano yako kutokana Na aina ya mpenzi ambaye unatoka nae".

"Kiukweli Mimi nipo Na mpenzi wangu huyu huyu ambae ninae kwa miaka miwili sasa Ila kwakuwa watu wanaongea waache waongee" alisema Manyika Jr.

Mashabiki walianza kumtuhumu Manyika Jr anashuka kiwango baada ya kugundua anatoka kimapenzi na binti wa kiarabu ambaye anamfanya Manyika kushindwa kufanya mazoezi Mara kwa Mara.

Jul 6, 2016

KIUNGO WA SEVILLA ASAINI MILAN

Na Haji balou
Timu ya Inter Milan imekalilisha usajili wa kiungo wa Sevila Na timu ya taifa ya Argentina Ever banega kwa mkataba wa miaka mitatu.

Banega aliisaidia Sevilla kuchukua mataji mawili mfululizo ya kombe la Europe league Na sasa ameamua kwenda Italy kwa uhamisho huru ili kitafuta changamoto mpya.

SIMBA YAMWEKA NJIA PANDA ISIHAKA

NA Haji Balou
Beki wa kati wa timu ya simba Hassan Isihaka amesema bado hajajua mustakabali wake Na timu yake ya simba katika msimu ujao.

“Wao bado hawajanifuata na mimi niko
njia panda kwani sifahamu lolote juu ya
maisha yangu ya Simba kama nitakuwepo
kwenye timu katika msimu ujao ama la,
lakini ni bora waniambie mapema nijue
nachukua maamuzi gani.

“Nasikia tu tetesi kuwa wanataka
kunipelekea Mbao FC ya Mwanza, lakini
kwangu sidhani kama nitaenda huko kwa
sababu mchezaji ndiye anayechagua wapi
aende sasa kama wao wamepanga
kunipeleka huko wataenda kucheza
wenyewe,” alisema Isihaka.

SOURCE: CHAMPIONI

Jul 5, 2016

20% AKUBALI YAISHE ASAINI MIAKA MITANO KWA MAN WATER

Na Haji balou
Msanii mkongwe wa muziki, Abbas Hamisi
Kinzasa ‘20%’ amerudi katika label yake ya
zamani ‘Combination Sound’ inayosimamiwa na
mtayarishaji mkongwe wa muziki nchini Man
Water.

Muimbaji huyo ambaye mwaka 2011 alitwaa
tuzo saba za Kilimanjaro Music Award (KTMA)
kwa mara moja, huku producer wake Man Water
akichukua tuzo mara mbili mfululizo za producer
bora (mwaka 2013 na 2014), tayari
amesharekodi ngoma kadhaa chini ya producer
huyo.

Kupitia instagram, Man Water ameandika:
Twenty Percent is back 2016, kaa mkao wa kula
ngoma zenye jumbe nzito na za kusisimua, kila
kitu kiko sawa sasa, new page.
20% kwa sasa anajipanga kuachia wimbo wake
mpya utaotoka Julai 18 mwaka huu huku
akijapanga kuandaa albamu yake iitwayo ‘Sauti
ya Gharama’.

Jul 4, 2016

SUAREZ MWINGINE ASAINI BARCELONA

Na Haji balou
FC BARCELONA imesibitisha kumsajili kiungo wa timu ya Villarreal Denis Suarez Na kesho anatarajiwa kupimwa afya.

Suarez mwenye umri wa miaka 22 alicheza Barcelona B kabla ya kuondoka kuamia Sevilla Na baadae kujiunga Na Villarreal ambayo aliisaidia mpaka kufika hatua ya nusu fainali Na  sasa amerudi tena  Barcelona.

Denis Suarez hana udugu wowote Na staa wa timu hiyo Luis Suarez ambaye alijiunga Barcelona misimu miwili iliyo pita.

STAA MWINGINE TOTENHAM KUJIUNGA REAL MADRID

Na Haji balou
Klabu ya Real madrid  tayari Kutoa euro million 35 ili kumnasa kipa namba moja wa Totenham Na Timu ya taifa ya Ufaransa  Hugo Lloris.

Kama Hugo Lloris  atajiunga Na Real Madrid atakuwa mchezaji watatu kujiunga Na Real Madrid akitokea Totenham kwa kipindi cha hivi karibuni  wachezaji wengine ni Gareth Bale, Luka Modric Na Emmanuel aliye enda kwa mkopo.

Jul 3, 2016

MAN UNITED KUVUNJA REKODI USAJILI WA POGBA

Na Haji Balou
Timu ya Manchester United imeiambia Timu ya Juventus kuwa wapo tayari kutoa Euro million 100 kwa ajilii ya kiungo Paul Pogba.

Manchester United wapo tayari kumlipa uero 250,000 kwa wiki kwa staa huyo wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 23.

MJUE STAA ANAYELIPWA MSHAHARA MKUBWA ZAIDI YA MESSI NA RONALDO

Na Haji balou
Neymar wa Barcelona ndiye anachukua
mshahara mkubwa zaidi kwa mwaka
mmoja anafuatiwa na Messi na hivyo
kuifanya Barcelona kuwa inalipa mshahara
mkubwa zaidi ikifuatiwa na Madrid.

10 BORA HII HAPA:

1.Neymar: euro milioni 56

2..Messi: euro milioni 50

3.Cristiano: euro milion 47.5

4..Ibrahimovic: euro milioni 26.7

5.Bale: euro milioni 21.4

6.Rooney: euro milioni 16.9

7.Luis Suarez: euro milioni 16

8.Iniesta: euro milioni 16

9.Hazard: euro milioni 16

10.Aguero: euro milioni 15.1

NDUGU WA KIPRE KUSAJILI SIMBA

Na Haji balou
SIMBA SC imemaua –
baada ya kuingia Mkataba
na kocha Mcameroon
Joseph Marius Omog sasa
imehamia kwenye kusajili
wachezaji bora wa kigeni.
Wakati tayari ikiwa imefikia
makubaliano na
mshambuliaji wa kimataifa
wa Burundi, Laudit Mavugo
aje kusiani Mkataba wa
miaka miwili, Simba SC
inaleta mshambuliaji hatari
kutoka Ivory Coast.

Huyo ni Goue Frederic Noel
Blagnon aliyezaliwa
Desemba 26, mwaka 1985
ambaye anatokea klabu ya
African Sports ya kwao,
Ivory Coast.

Jul 2, 2016

LIVERPOOL YAONGEZA KIFAA KIPYA KUIMARISHA ULINZI

Na Haji balou
TIMU ya Liverpool imekamilisha uhamisho wa staa wa Schalke 04 Na Timu ya taifa ya Cameroon Joel Matip.

Matip ambaye anacheza nafasi ya beki wa kati amejiunga Na Liverpool kwa uhamisho huru baada ya kumaliza mkataba Na Timu yake ya Schalke 04 ya Ujerumani.

.

Jul 1, 2016

PEP GUARDIOLA AMEMSAJILI STAA HUYU HAPA KUTOKA SPAIN

Na Haji balou
TIMU ya Manchester city imekamilisha uhamisho wa Staa wa kimataifa wa Hispania Na Klabu ya Celta Vigo Manuel Agudo Durán "Nolito" Kwa Ada ya Euro million 13.8.

Nolito mwenye umri wa miaka 29 amesaini mkataba wa miaka minne ya kuitumikia Manchester City awali  alikuwa anatakiwa Na Klabu ya Fc Barcelona.

HAYA NDIO MAAMUZI YA BARCELONA KUHUSU NEYMAR

Na Haji balou
Klabu ya Fc Barcelona wamekubali yaishe Na wameamua kukaa pamoja Na mchezaji wao Neymar ili kumbakiza katika kikosini  katika msimu ujao.

Staa huyo wa Brazil alikuwa tayari kuihama klabu hiyo ya katalunya Kama watashindwa kuongeza mshahara wake katika msimu ujao.

Neymar mwenye umri wa miaka 24 anataka kulipwa Euro million 16.5 ili abaki lakini Barcelona hawakuwa tayari kumlipa kiasi hicho cha pesa hata hivyo Manchester United walikuwa tayari kumlipa Neymar kiasi hicho cha pesa Na wakaanza kumfukuzia Staa huyo.

Jun 30, 2016

GUARDIOLA ANAMTAKA STAA HUYU WA BARCELONA

Na Haji balou
Kocha mpya wa Manchester City Pep Guardiola anampango wa kumsajili kipa namba moja wa Timu ya Taifa ya Chile Na Klabu ya Fc Barcelona ya nchini Hispania Claudio Bravo.

Guardiola anataka kumsajili Bravo ambaye ameisaidia Timu yake ya  Taifa kushinda kombe la Copa America lakini pia kumpa changamota kipa namba moja wa Timu hiyo Joe Hart ambaye hajafanya vizuri katika michuano ya Euro inayoendelea nchini Ufaransa.

ATLETICO MADRID KUIBOMOA LIVERPOOL KWA STAA HUYU HAPA

Na Haji balou
Gazeti moja la nchini Hispania limeripoti kuwa Timu ya Atletico Madrid imeanza mazungumzo Na klabu ya Liverpool kwa ajili ya kumchukua mshambuliaji wa Timu hiyo Christian Benteke.

Benteke raia wa Ubelgiji amekuwa Na wakati mgumu katika kikosi cha Liverpool mbele Daniel Sturridge Na Divock Origi.

Benteke ambaye alisajiliwa Na Liverpool kwa Ada ya Euro million 32 akitokea Aston Villa Na Liverpool wapo tayari kumuuza kwa Euro million 24 Mpaka 30.

Jun 27, 2016

HAYA NDIO MAAMUZI MAGUMU ALIYOYAFANYA LIONEL MESSI

Na Haji balou
MAUMIVU ya moyo
yamemshinikiza Mwanasoka
Bora wa Dunia, Lionel Messi
kustaafu kuichezea timu
yake ya taifa ya Argentina
baada ya jana kufungwa
katika fainali ya tatu
mfululizo ya Copa America
ndani ya miaka mitatu.

Messi si mgonjwa wa moyo,
bali ameumizwa n a kitendo
cha kukosa penalti ya
kwanza Argentina ikifungwa
kwa penalti 4-2 katika
fainali ya Copa America
Centenario baada ya sare
ya 0-0 ndani ya dakika 120.

Messi ambaye alimwaga
machozi na kilio baada ya
mechi hiyo alizungumza na
Televisheni ya Argentina
baada ya mechi na
kufafanua uamuzi wake. "Ni
hivyo. Mimi baso na timu ya
taifa,"alisema.

"Si kwangu. Hii ni fainali ya
nne. Uamuzi umefanyika,
nafikiri hivyo. [kushinda]
ndicho ninachoitaka zaidi.
Sikuja. nafikiri ni hivyo.
Hivyo ndivyo ninavyojisikia
kwa sasa, ninachofikiria. ni
maumivu makubwa,".

Jun 25, 2016

NYOTA WA UBELGIJI AKARIBIA KUSAINI ARSENAL

Na Haji balou
Baada ya kumkosa staa wa Leicester city Jamie vard kocha wa Arsenal Arsene Wenger ameamua kuamishia nguvu zake kwa staa wa Everton na Timu ya taifa Ubelgiji Romelu Lukaku.

Mwandishi wa habari za michezo nchini Italy ameripoti kuwa Lukaku amekubali dili la kusaini Arsenal dili hili limekuja baada ya kumkosa staa    wa England Jamie Vard.

Kwasasa Lukaku yupo nchini Ufaransa Na Timu yake ya taifa ya Ubelgiji inayoshiriki michuano ya Euro Na ameshafunga magoli mawili katika mechi tatu walizocheza.

LIVERPOOL YAKARIBIA KUMSAJILI STAA HUYU HAPA

Na Haji balou
Timu ya Liverpool ipo tayari kutoa Euro million 30 kwa Timu ya Southampton kwaajili ya kuinasa saini ya Mshambuliaji wa Timu hiyo Sadio Mane Raia wa Senegal.

Kocha wa Liverpool Juggen kloop amekuwa akimfuatilia kwa karibu Mshambuliaji huyo tangu alipo wafunga goli mbili katika mchezo wa Ligi mwishoni mwa msimu uliopita.

Jun 22, 2016

WALICHOSEMA REAL MADRID KUHUSU ALVARO MORATA

Na Haji balou
Timu ya Real Madrid imethibitisha kuwa nampango wa kumsajili Alvaro Morata kutoka Juventus msimu huu.
Morata alijiunga na Mabingwa wa Italy Juventus mwaka 2014 akitokea Real Madrid kwa mkataba wa miaka minne (4) uliogharimu Euro million 20 lakini vigogo hao wa Spain wapo tayari kutoa Euro millioni 30 ilikuinasa saini ya staa huyo.
Taarifa za kina zinasema kuwa Real Madrid imewajulisha Juventus maamuzi yao ya kumwitaji mchezaji Alvaro Morata na atajiunga katika kikosi cha kwanza cha timu hiyo inayonolewa na Zinedine Zidane.
Kwasasa Alvaro Morata yupo kwenye michuaono ya Euro inayoendelea nchini Ufaransa na amefunga magoli matatu katika mechi tatu nakuisaidia timu yake ya Hispania kuingia katika hatua ya 16 bora.


YANGA WAMEFIKIA HAPA KUHUSU HASSAN KESSY KUCHEZA MICHUANO YA CAF

Na Haji Balou
YANGA wamewaandikia
barua Simba SC kuwajulisha
kumsajili beki Hassan
Ramadhan Kessy na kuuliza
kama kuna pingamizi lolote
kutoka kwao, na wakati huo
huo nakala zimepelekwa
Shirikisho la Soka Tanzania
(TFF) na Shirikisho la Soka
Afrika (CAF).

Yanga ilishindwa kumtumia
Kessy Jumapili katika
mchezo wake wa kwanza
wa Kundi A Kombe la
Shirikisho Afrika wakifungwa
1-0 na wenyeji MO Bejaia
nchini Algeria, baada ya
CAF kuomba barua ya
kuruhusiwa kwake kuondoka
klabu yake ya zamani,
Simba SC, ambayo
hawakuwa nayo.

Na mara baada ya mchezo
huo, Yanga imewaandika
barua mahasimu wao hao
wa jadi, ikiwa
imeambatanisha Mkataba
wa Kessy na Simba ambao
unaonyesha umemalizika
Juni 15, mwaka huu na
mchezaji huyo alikuwa
sahihi kuingia Mkataba
mpya na klabu nyingine.

Na Yanga imepanga iwapo
hadi kufika Jumatano Simba
haitakuwa na majibu yoyote
ya barua hiyo – wataomba
TFF iwasaidie
kumuidhinisha beki huyo wa
kulia kuanza kazi Jangwani,
maana yake klabu yake ya
zamani haitakuwa na
pingamizi naye.

Na iwapo Simba SC
watamuwekea pingamizi
Kessy, watapaswa kuwa na
hoja za pingamizi ambalo
litasikilizwa na Kamati ya
Sheria na Hadhi za
Wachezaji ya TFF, chini ya
Mwenyekiti wake, Wakili
Richard Sinamtwa.

Na kulingana na uzito wa
suala hilo, inatarajiwa hadi
kufika Ijumaa Kessy
atakuwa amekwishapewa
baraka za kuanza kuitumikia
Yanga.

MAYANJA AREJEA DAR KUANZA MAANDALIZI YA MSIMU MPYA

Na Haji Balou
KOCHA wa Simba, Mganda
Jackson Mayanja
anatarajiwa kuwasili Juni 25
au Juni 26 na siku moja
baadaye ataanza programu
ya mazoezi ya kujiandaa na
msimu mpya.

Hayo yamesemwa na
Mwenyekiti wa Kamati ya
Usajili ya Simba, Zacharia
Hans Poppe alipozungumza
na mwandishi wetu  leo kuhusu mikakati
ya usajili na maandalizi ya
msimu mpya jana mjini Dar
es Salaam.

Kapteni huyo wa zamani wa
Jeshi la Wananchi Tanzania
(JWTZ), Popppe amesema
kwamba mara Mayanja
atakapowasili, wachezaji
wote wenye Mkataba na
Simba SC wakiwemo wapya
ambao wamesajiliwa hivi
karibuni wataanza mazoezi.

MZAMBIA WA YANGA APEWA JEZI YA COUTINHO

Na Haji balou
SIKU chache baada ya kusaini mkataba
wa miaka miwili ya kuichezea Yanga,
uongozi wa Yanga umemkabidhi jezi
namba saba mshambuliaji wake Mzambia,
Obrey Chirwa.

Chirwa alitua nchini wiki iliyopita akitokea
FC Platinum ya Zimbabwe aliyokuwa
anaichezea pamoja na mshambuliaji
tegemeo, Donald Ngoma.
Mzambia huyo, alisaini kuichezea Yanga
akichukua nafasi ya Mniger, Issoufou
Aboubacar aliyesitishiwa mkataba wake
wa kuendelea kukipiga Jangwani hivi
karibuni.

Meneja wa timu hiyo, Hafidh Saleh
alisema jezi iliyobaki ni namba saba
iliyokuwa inavaliwa na Mbrazili, Andrey
Coutinho.

Jun 20, 2016

YANGA YAANZA VIBAYA KOMBE LA SHIRIKISHO

Na Haji balou
YANGA SC imeanza vibaya mechi za
Kundi A Kombe la Shirikisho Afrika,
baada ya kufungwa bao 1-0 wenyeji
Mouloudia Olympique Bejaia Uwanja
wa Unite Maghrebine mjini Bejaia
usiku huu.

Goli pekee la MO Bejaia alikuwa ni beki
Yassine Salhi aliyefunga bao hilo
pekee dakika ya 20, akimalizia kazi
nzuri ya mshambuliaji Ismail
Belkacemi.

Matokeo hayo yanaifanya MO Bejaia
ishike nafasi ya pili katika kundi hilo,
nyuma ya TP Mazembe ambayo
iliifunga Medeama ya Ghana 3-1
katika mchezo wa kwanza mjiji
Lubumbashi Jumapili, wakati Yanga
inashika nafasi ya tatu.

Mechi zijazo za kundi hilo, Yanga
watakuwa wenyeji wa Mazembe Dar
es Salaam na Medeama
wataikaribisha Mo Bejaia.

Jun 10, 2016

DALILI MPYA YA IBRAHIMOVIC KUHAMIA MAN UTD

Na Haji balou
Staa wa zsmani wa
klabu ya Paris Saint Germain ya Ufaransa
Zlatan Ibrahimovich kuhusishwa kujiunga na
klabu ya Man United zimechukua sura mpya,
Zlatan anaripotiwa kukamilisha hatua ya nne ya
kujiunga na klabu ya Manchester United .

Dalili inayotajwa kuwa staa huyo yupo mbioni au
katika hatua za mwisho kujiunga na klabu ya
Man United zinazidi kudhihirika, baada ya
kuripotiwa tayari ametafutiwa nyumba ya kuishi
katika jiji la Manchester ambapo ndio makao
makuu au mji inapotoka klabu ya Man United.

Kwa mujibu wa nyaraka iliyopostiwa katika
websites ya Proto Group Ltd ambao ni mawakala
wa nyumba inaashiria kuwa mipango ya Zlatan
kutangazwa kujiunga na Man United ipo tayari
kutokana na mji alipotafutiwa nyumba ya kuishi,
kwani kabla ya hapo alikuwa akiishi Paris
Ufaransa .

Jun 4, 2016

IBRAHIMOVIC ATAJIUNGA NA TIMU HII ENGLAND

Na Haji balou
Sky Sport wameripoti kuwa Zlatan Ibrahimovic  atakamilisha
usajili wa kujiunga na Man United wakati
wowote kuanzia sasa ila ni kabla ya michuano
ya mataifa ya Ulaya kuanza, Sky Sport
wanaeleza kuwa kocha wa Man United Jose
Mourinho amepanga kusajili mshambuliaji
mmoja katika dirisha hili la usajili ila Zlatan
Ibrahimovic ndio chaguo lake.

Mtendaji mkuu wa Man United Ed Woodward na
wawakilishi wa Zlatan wanaripotiwa kuwa katika
mazungumzo ya mwisho ili kumsajili staa huyo
kwa mkataba wa mwaka mmoja, Zlatan kwa
sasa yupo na timu yake ya taifa ya Sweden
anajiandaa mchezo wao wa kwanza wa Euro
2016 dhidi ya Ireland utakaochezwa June 13.

Jun 3, 2016

ULIMWENGU HATARINI KUWAKOSA MISRI

Na Haji balou
MSHAMBULIAJI wa TP Mazembe ya
DRC, Thomas Emmanuel Ulimwengu
'Rambo' jana hakufanya mazoezi na
timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars
kwa sababu ya maumivu ya mguu.

Ulimwengu baada ya kuwasili na
wachezaji wenzake Uwanja wa Taifa,
alijaribu kufanya mazoezi ya awali ya
kuamsha misuli kidogo, kabla ya
kushindwa kuendelea na kutoka nje.

Madaktari wa Taifa Stars walijaribu
kuhangaika naye kumrejesha
uwanjani, lakini hakuweza kabisa
kurudi mazoezini.

Daktari Mkuu wa Taifa Stars, Gilbert
Kigadye akasema Ulimwengu aliumia
juzi Taifa Stars na jana ameshindwa
kabisa kufanya mazoezi kwa sasa wanaangalia namna ya ya punguza maumivu.

May 29, 2016

BODABODA FC YATINGA NUSU FAINAL

Na Haji balou
Leo mei 29 kulikuwa na mchezo wa robo fainali mchezo ulipigwa ktk uwanja wa Shule ya msingi  muungano kati ya timu  Likongowele fc vs Bodaboda fc.

Mpaka mchezo unamalizika
Likongowele fc o-2 Bodaboda Magoli yote ya Boda Boda fc  yalifungwa na faraja katika dk 25 na dk 80

Mecho wa jana kati Vijuso fc vs kombaini fc  utarudiwa kesho jioni ndani ya dk 7 ikitokea sare zitapigwa penaiti.

May 28, 2016

NGASSA AITAJA TIMU INAYO MWITAJI VPL

Na Haji balou
Pamoja na uongozi wa Free State Stars
ya Afrika Kusini kumzuia kiungo wake
mshambuliaji, Mrisho Ngassa kumtoa kwa
mkopo, nyota huyo amewatoa hofu
mashabiki wa Yanga na kuwaambia siku si
nyingi anarejea kwenye klabu hiyo.

Ngassa ameitoa kauli hiyo muda mfupi
baada ya kuwasili nchini kisha kutazama
mechi ya fainali ya Kombe la FA kati ya
Yanga na Azam FC kwenye Uwanja wa
Taifa, Dar ambapo Yanga ilishinda mabao
3-1.

Ngassa alijiunga na Free State inayoshiriki
Ligi Kuu Afrika Kusini, mwaka jana baada
ya mkataba wake kumalizika Yanga.
Ngassa amesema viongozi wa Yanga ndio waliowafuata Free State kwa ajili ya
kumuomba kwa mkopo ili aiongezee
nguvu timu hiyo katika hatua ya makundi
ya Kombe la Shirikisho Afrika.

NGASSA AITAJA TIMU INAYO MWITAJI VPL

Na Haji balou
Pamoja na uongozi wa Free State Stars
ya Afrika Kusini kumzuia kiungo wake
mshambuliaji, Mrisho Ngassa kumtoa kwa
mkopo, nyota huyo amewatoa hofu
mashabiki wa Yanga na kuwaambia siku si
nyingi anarejea kwenye klabu hiyo.

Ngassa ameitoa kauli hiyo muda mfupi
baada ya kuwasili nchini kisha kutazama
mechi ya fainali ya Kombe la FA kati ya
Yanga na Azam FC kwenye Uwanja wa
Taifa, Dar ambapo Yanga ilishinda mabao
3-1.

Ngassa alijiunga na Free State inayoshiriki
Ligi Kuu Afrika Kusini, mwaka jana baada
ya mkataba wake kumalizika Yanga.
Ngassa amesema viongozi wa Yanga ndio waliowafuata Free State kwa ajili ya
kumuomba kwa mkopo ili aiongezee
nguvu timu hiyo katika hatua ya makundi
ya Kombe la Shirikisho Afrika.

HABARI NJEMA KWA WAKAZI WA TANGA BAADA YA TIMU ZAO TATU KUSHUKA DARAJA

Na Haji balou
KAIMU Katibu Mkuu wa Coastal Union,
Salim Bawazir amesema timu hiyo sasa
itakuwa chini ya usimamizi wa Nassor
Binslum pamoja na uongozi wa Chama
cha Soka Mkoa wa Tanga (TRFA) kwa
ajili ya kuiwezesha kushiriki vyema Ligi
Daraja la Kwanza (FDL) ili irejee Ligi
Kuu Bara.

Akizungumza na Mwanaspoti Bawazir
alisema: “Tumepata funzo kubwa,
kugawanyika kwetu ndiko
kulikotushusha daraja, sasa hatutakubali
mambo hayo tena, tutahakikisha Coastal
inashiriki kikamilifu Ligi Daraja la
Kwanza na msimu ujao tutarejea Ligi
Kuu Bara.”

Bawaziri alisema BinSlum na TRFA
watashiriki kikamilifu katika suala zima
la usajili wa wachezaji, kocha mwenye
ujuzi na uzoefu na kuilea timu ikiwa
kwenye kanda itakayopangiwa.

“Tunatambua kwamba FDL ni ngumu
kuliko hata ligi kuu ili uweze kufuzu ni
lazima timu iwe na mikakati kabambe
na si ubabaishaji,” alisema Bawazir.

May 27, 2016

WACHEZAJI AZAM FC WAPEWA MAPUMZIKO

WACHEZAJI wa Klabu Bingwa ya Afrika
Mashariki na Kati Azam FC, wamepewa
mapumziko ya wiki tano baada ya
kumaliza mechi ya mwisho ya msimu wa
2015/16 dhidi ya Yanga kwenye mchezo
wa fainali ya Kombe la Shirikisho (Azam
Sports Federation Cup) juzi jioni.
Azam FC inayodhaminiwa na Benki ya
NMB ambayo ni benki bora kabisa
iliyosambaa kila kona nchini, ilipoteza
mchezo huo wa fainali baada ya
kufungwa mabao 3-1.

Akizungumza na mtandao rasmi wa klabu
Na mtandao huu mara baada ya
mchezo huo Ofisa Mtendaji Mkuu wa
Azam FC, Saad Kawemba, alisema kuwa
msimu ndio umeisha kwa timu hiyo na
kilichobakia ni kujipanga kwa ajili ya
kupata matokeo mazuri msimu ujao.
“Tunamshukuru Mwenyezi Mungu
tumecheza mchezo wa fainali, ingawa
matokeo yalikuwa si mazuri haikuwa
malengo yetu, tulipanga kushinda lakini
lazima tukubali ni matokeo ya mpira,”
alisema.

Kawemba alisema wachezaji watamaliza
likizo hiyo Juni 30 mwaka huu na Julai
Mosi wataanza maandalizi ya msimu
mpya.
“Kwa hiyo tutafanya nini kwa msimu ujao,
tutamuongeza nani, tutamtoa nani hayo
tutazungumza baadaye lakini sasa hivi
tunawaomba washabiki wetu wawe
watulivu na tutaendelea kujipanga,”
alisema.

HAYA NDIO MASHINDANO MAPYA YANAYO DHAMINIWA NA AZAM TV

KAMPUNI ya Azam Media Limited leo imeingia Mkataba na Shirikisho la
Mpira wa miguu Tanzania (TFF)
wenye thamani ya Sh.Bilioni 2 kurusha matangazo ya moja kwa moja ya Ligi Kuu ya Wanawake
Tanzania na Ligi Kuu ya Vijana wa
umri chini ya miaka 20.

Zoezi hilo limefanyika Ofisi za makao
Makuu ya Azam Media Ltd eneo la
TAZARA, Dar es Salaam upande wa
TFF ukiwakilishwa na Rais wake,
Jamal Malinzi na Azam Media
wakiwakilishwa na Mtendaji wake
Mkuu, Muingereza Rhys Torrington.

Akizungumza katika hafla hiyo fupi,
Torrington amesema Mkataba huo ni
wa miaka mitano na lengo laoe ni
kuendelea kusaidia kuinua michezo
Tanzania.

"Baada ya mafanikio ya awali tukiwa
na Ligi Kuu ya Wanaume na
mashindano mengine, sasa tunapiga
hatua nyingine hatika jitihada zetu
kuchangia maendeleo ya soka nchini
kwa kuingia mikataba ya ligi hizi
mbili,"amesema Torrington.

Kwa upande wake, Malinzi amesema
kwamba Ligi Kuu ya Wanawake
itaanza kwa kushirikisha klabu 10
Agosti mwaka huu na Ligi ya U20
itashirikisha klabu zote za Ligi Kuu ya Wanaume.

"Na Ligi ya U20 itachezwa sambamba na Ligi Kuu ya wanaume, kabla ya mechi za timu za wakubwa,
zitatangulia mechi za vijana. Na kila
timu itasafirisha timu yake ya vijana
kwa mechi za mikoani. Itakuwa ligi
kamili na yenye kanuni
madhubuti,"amesema Malinzi.

MUSSA MGOSI ATAJA VITU VIWILI AMBAVYO HAWEZI KUVISAHAU MSIMU HUU

Na Haji balou
Mshambuliaji mkongwe wa Simba Musa Hassan Mgosi kupitia Simba news amesema kuna vitu viwili ambavyo hatavisahau baada ya msimu huu wa VPL kumalizika huku klabu yake ikiangukia nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi.

“Kuna mambo mengi ambayo yametokea kwenye msimu wa 2015-16 lakini kwa upande
wangu, kuna vitu viwili ambavyo siwezi kuvisahau”, amesema Mgosi ambaye hakupata nafasi ya kutosha kucheza msimu huu kwenye kikosi cha Simba.

“Kitu cha kwanza ni mechi kati yetu ya nusu fainali ya FA Cup dhidi ya Coastal Union. Coastal Union haikuwa timu ya kututoa sisi
lakini kwenye mpira hakuna udogo wa ukubwa wa timu inategemea na maandalizi ya timu, iliniuma sana kutolewa na timu kama Coastal”.

“Kitu kingine kilikuwa ni kufungwa mechi zetu zote mbili na watani wetu wa jadi Yanga, katika uwepo wangu Simba muda wote, hatujawahi
kufungwa na Yanga mara mbili mfululizo kwenye msimu mmoja, niliumia sana”.

May 26, 2016

ROBO FAINAL VIJANA CUP YAANZA RASMI LEO

Na Haji balou
Hatua ya robo final ya ligi ya mbuzi vijana cup imeanza Leo kwa mchezo mmoja kupigwa  katika uwanja wa Shule ya msingi muungano.

Mchezo huo ulikuwa ni kati ya wakaanga sumu fc  dhidi ya kigamboni fc Mchezo ulio malizika kwa wakaanga sumu kuibuka Na ushindi wa goli 2-1.

May 24, 2016

LIGI YA MBUZI VIJANA CUP YAMALIZIKA HATUA YA MAKUNDI KWA SIDO FC KUIBUKA NA USHINDI

Na Haji balou
Ligi ya Mbuzi Vijana cup imeendelea tena hii Leo kwa mchezo mmoja kupigwa katika  uwanja wa shule ya msingi muungano katika kuhitimisha hatua ya makundi kati ya Sido fc dhidi ya Vijuso fc mchezo ambao umemalizika kwa Sido kuibuka Na goli 1-0.

Goli pekee la Sido fc lilifungwa Na Haikosi mpwate katika dakika ya 65 ya mchezo huo ligi hiyo itaendelea tena tarehe 26 mwezi huu kwa mechi za robo fainali.

Timu zilizoingia hatua ya robo final katika kundi A  Kigamboni, Kombaini, Mnalani, na Likongowele.

Kundi B ni Sido, Bodaboda, Wakaanga sumu na Vijuso.

YANGA KUPAMBANA NA TP MAZEMBE KOMBE LA SHIRIKISHO

Na Haji balou
YANGA SC imepangwa kundi la A
katika Kombe la Shirikisho Afrika
pamoja na mabingw awa zamani
barani, TP Mazembe ya DRC, MO
Bejaia ya Algeria na Medeama ya
Ghana.

Kundi B linaundwa na timu za
Kaskazini mwa Afrika tupu ambazo ni Etoile du Sahel ya Tunisia ambao ni  mabingwa watetezi, Ahly Tripoli ya Libya, FUS Rabat na Kawkab zote za  Morocco.

Mechi za mzunguko wa kwanza
zitachezwa Juni 17, mwaka huu na
Ratiba hiyo inamaanisha Yanga
itakutana na timu ya mshambuliaji wa Tanzania, Thomas Ulimwengu wa TP Mazembe ya DRC.

May 23, 2016

KIGAMBONI FC YAENDELEA KUTOA DOZII

Na Haji balou
Mchezo wa Ligi ya Mbuzi Vijana Cup imeendelea tena hii Leo Kwa Mchezo kati ya Kigamboni fc dhidi  Mnalani Mchezo ambao umemalizika Kwa Kigamboni kuibuka Na Ushindi wa goli 2-1.

Ligi hiyo inaendelea tena hapo kesho Kwa Mchezo mmoja kupigwa kati ya
Vijuso dhidi ya Sido mchezo utakao pigwa katika uwanja wa shule ya msingi muungano.

May 22, 2016

WAKAANGA SUMU WAPEWA POINT BILA KUTOKA JASHO

NA Haji balou
Ligi ya mbuzi vijana cup imeendelea tena leo  may 22 kwa mchezo mmoja kati ya kati ya Black star dhidi ya Wakaanga Sumu
Lakini timu ya Black star haikujitokeza uwanjani na haijatoa taarifa yeyote kwa uongozi wa Ligi .

Uongozi wa ligi unalazimika kutoa pointi tatu kwa timu ya Wakaanga Sumu kupewa ushindi wa goli tatu   na point 3.

Kesho kutakuwa na mchezo kati ya Kigamboni fc Vs Mnalani fc
Mchezo wa kesho unatarajia kuwa mchezo wa mkali kwakuwa Kigamboni wanataka kuendeleza kuweka rekodi ya kutokupoteza mchezo wowote katika Ligi.

May 19, 2016

NANGANDO WAN'GAA LIGI YA MBUZI VIJANA CUP

Na Haji Balou
Ligi ya mbuzi vijana cup Leo iliendelea ktk uwanja wa shule ya msingi Muungano kati ya Likongowele fc dhidi ya Nangando fc Mpaka dakika 90 zinamalizika Nangando fc imeibuka Na ushindi wa goli 4-2.

Magoli ya Nangando yalifungwa
Dakika ya 5 na Shehani Chikanga Dakika ya 10 na Ligubi Ligubi
Dakika ya 66 na Ligubi Ligubi
Dakika ya 87 na shehani Chikanga

Magoli ya Likongowele fc dakika ya 22 na Isihaka Haji dakika ya 65 na Faraji Manyai.

Baada ya mchezo kumalizika Abilah Rashid Kocha wa Nangando fc alisema kuwa ametumia mapungufu ya wapinzani wao katika mchezo wa leo Na hiyo Ndio sababu kubwaa ya wao kuibuka Na ushindi katika mchezo wa Leo.

May 18, 2016

SIDO FC YATOKA SARE DHIDI YA WAKAANGA SUMU KUBOTA NA ZFC ZAFUNGIWA

Na Haji balou
Mchezo kati ya Sido fc dhidi ya Wakaanga sumu umemalizika katika uwanja wa shule ya msingi muungano kwa sare ya goli 2-2.

Katika kipindi cha kwanza magoli ya Sido fc walifungwa namo dakika ya 7 na 15 yote yakipachikwa na Haikosi Mpwate na goli la Wakaanga Sumu likufungwa na  Bocho Shabani dakika ya 24.

Katika kupindi cha pili Wakaanga Sumu walisawazisha goli dakika ya 70 goli lililofungwa na Stamili Abduli
Mpaka dakika 90 zinakamilika matokeo yalikuwa Wakaanga sumu 2-2 Sido fc.

Nimezungumza na kamisaa wa mashindano ya ligi Shamte Mohamedi Shamte kuzungumzia sakata la mechi mbili za juzi kati ya Kubota fc Vs Kubota fc na Jana Z fc Vs Kigamboni fc kutokumalizika uongozi uliamua haya.

Timu zote ambazo zimeanzisha fujo katika mechi ya Jana Na juzii zimefungiwa katika mashindano hayo ya Kombe la mbuzi timu hizo ni Vijuso fc Na Zfc.

ORODHA YA TOP 10 WAFUNGAJI BORA ULAYA MESSI CHALIII

Na Haji balou
Luis Suarez (29) kwa mara ya kwanza alipata tuzo hiyo mwaka 2014 baada ya kufungana magoli na
Cristiano Ronaldo wakati huo akiwa Liverpool akifunga magoli 31 na kuwa mfungaji bora pia wa EPL.

Suarez amekuwa ni mchezaji wa kwanza La Liga mbali ya Messi na Ronaldo kushinda tuzo ya ufungaji bora tangu mwaka 2009.

Ukiwa msimu wa 2015-15 ukielekea ukingoni huku ukiwa umeisha kwa baadhi ya ligi, hii ndiyo orodha ya wafungaji 10 bora wa Ulaya msimu
huu: