SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Jan 20, 2016

SAMATTA ARUDI MAZEMBE KUMALIZIA MKATABA, KATUMBI HOI

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa
Tanzania, Mbwana Ally Samatta
anaondoka asubuhi ya leo kwenda
Lubumbashi, Jamhuri ya Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Kongo (DRC),
kujiunga na klabu yake, TP Mazembe
wakati sakata la uhamisho wake
likiendelea.

Samatta anaondoka na Maofisa wa
Wizara ya Michezo walioteuliwa
kwenda kuzungumza na Rais wa TP
Mazembe, Moise Katumbi
kumshawishi amruhusu mchezaji huyo

kujiunga na KRC Genk ya Ubelgiji.
Lakini iwapo Katumbi ataendelea
kusistiza msimamo wake wa kutaka
Samatta aende Nantes ya Ufaransa,
basi mchezaji huyo ataamua kubaki
Mazembe amalizie miezi yake mitatu
ya Mkataba wake ili aondoke kama
mchezaji huru Aprili.