SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

May 25, 2015

HUU NDIO UAMUZI WA MAN U KWA FALCAO

 
Frank Lampard, Didier Drogba, Steven Gerrard na Brad Fiedal leo watacheza mechi zao za mwisho katika ligi kuu ya England baada ya miaka zaidi ya 10 kwa kila mmoja wao.
Hata hivyo macho na masikio ya wapenzi wengi wa soka yapo katika kuangalia hatma ya mshambuliaji wa kicolombia Radamek Falcao ndani ya klabu ya Manchester United.

Falcao ambaye alijiunga na United kwa mkopo wa mwaka mmoja akitokea Monaco, ameambiwa rasmi na United kwamba klabu hiyo haitoweza kumuongezea muda ndani ya klabu hiyo, hii ni kwa mujibu wa mhariri mkuu wa Dailymail – Ian Ladyman.
Falcao ambaye ameshindwa kung’ara na Man United na hivyo kutumia muda mwingi benchi, ameifungia timu hiyo magoli 4 na kutoa pasi za magoli 4.

Kwa mujibu Ladyman, Falcao alikuwa na mazungumzo na kocha Louis Van Gaal kuhusu hatma yake na hata alikubali kupunguza matakwa ya mshahara ili aendelee kubaki Old Trafford lakini haikuwezekana.

Mchezaji huyo anategemewa kucheza mechi yake ya mwisho leo dhidi ya Hull City katika siku ya mwisho ya Barclays Premier League na baada ya hapo atasafiri kwenda kwao kujiunga na Colombia kwa ajili ya michuano ya Copa America.

TFF YATOA MAAMUZI JUU YA MART NOOIJ


KOCHA-TAIFASTARS
Kamati ya utendaji ya TFF imesikitishwa na mwenendo mbovu wa Taifa Stars Rais wa TFF, Jamal Malinzi kwa niaba ya kamati ya utendaji amewaomba radhi wapenzi wa mpira kwa matokeo mabaya ya Taifa Stars kwenye michuano ya  Cosafa.
Kikao cha kamati ya utendaji kilipokea taarifa juu ya mwenendo wa timu ya Taifa.
Baada ya majadiliano ya kina, ilikubaliwa kuwa kocha mkuu wa timu ya Taifa, Mart Nooij apewe changamoto maalumu ya kufuzu kwa fainali za Afrika kwa wachezaji wa ndani CHAN na asipofanikisha jambo hilo mkataba wake utasitishwa mara moja.
Maamuzi haya yamezingatia hali halisi ya timu ya Taifa ambayo inakabiliwa na michuano mbalimbali ya kimataifa ndani ya kipindi kifupi.
Aidha katika kuliimarisha benchi la ufundi la timu ya Taifa, Leopald Tasso Mkebezi ameteuliwa kuwa meneja mpya wa timu ya Taifa.
Mkebezi amewahi kuwa meneja wa timu ya Taifa katika kipindi cha mwaka 2006 – 2012.

KUHUSU CHANONGO KUMALIZANA NA YANGA MENEJA WAKE ANEA

943612_heroa
STORI ya winga Haruna Chanongo kusajiliwa na Yanga imegonga vichwa vya habari nchini, lakini taarifa mpya kutoka kwa Meneja wake, Jamal Kasongo ni kwamba bado nyota huyo hajamwaga wino Jangwani.
Msimu uliopita wa ligi kuu soka Tanzania bara uliomalizika mei 9 mwaka huu, Chonongo alikuwa anaichezea Stand United ya Shinyanga.
“Ni vyombo vya habari, hatujakaa na viongozi wa Yanga zaidi ya kunipigia simu tu!. Amefananua Kasongo na kuongeza: “Tumezungumza na kufika mahala ambapo tumewaacha wajifikirie (Yanga) na sisi tufikirie, lakini bado hajasaini”.
“Sijakaa mezani kuzungumza nao, nilipigiwa simu tu na kiongozi mmoja wa Yanga na muda si mrefu nimewaambia kwamba tunapaswa kukaa mezani”.
Kwanini Kasongo ambaye pia ni wakala wa Mbwana Samatta wa TP Mazembe, anaweka ngumu kumruhusu Chanongo kusaini Yanga?

“Kubwa zaidi kwangu ni mkataba, kuna vipengele ambavyo nataka lazima viwepo, unajua  tunachotazama ni hatima ya mtoto (Chanongo) kwenda mbele zaidi, nadhani kama Chanongo atakaa zaidi ya mwaka mmoja Yanga atakuwa wa hapa hapa, nina ofa nyingi za nje, kwahiyo nataka kujua kama Chanongo atasaini Yanga hatima yake itakuwaje?’ Amesema Kasongo.

HUYU NDIYE ATAKAE ZIBA PEGO LA NGASSA YANGA



Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
YANGA SC imewapiga bao wapinzani, Simba SC na Azam FC katika vita ya kuwania saini ya kiungo hodari wa pembeni, Deus Kaseke.
Kaseke amesaini Mkataba wa miaka miwili na Yanga SC asubuhi ya leo, makao makuu ya klabu, Jangwani, Dar es Salaam mbele ya Katibu Mkuu, Dk Jonas Tiboroha na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji, Isaac Chanji.
Kaseke anatua Yanga SC kama mchezaji huru baada ya kumaliza Mkataba wake Mbeya City, aliyoichezea kwa miaka mine iliyopita.
Akizungumza na BIN ZUBEIRY baada ya kusaini Mkataba huo, Kaseke amesema; “Nimefurahi kutua Yanga SC, ni timu ambayo kwa kweli nilikuwa nina ndoto za kuichezea kwa muda mrefu,”. 
Deus Kaseke katikati akisaini Yanga SC leo, kulia ni mjomba wake, Bahati Kaseke na kushoto Katibu wa Yanga SC, Dk Jonas Tiboroha
Kaseke amesema anafahamu changamoto inayomkabili baada ya kusaini Yanga SC, ushindani wa nafasi dhidi ya wachezaji wengine bora waliopo kwa mabingwa hao wa Tanzania.
“Yanga SC ni timu kubwa, ina wachezaji bora na ndiyo maana ni mabingwa. Baada ya kusajili, sasa natakiwa kufanya mazoezi kwa bidii ili niwe katika kiwango bora zaidi na kuwashawishi makocha wanipe nafasi,”amesema.
Kaseke amesema lengo lake ni kufika mbali zaidi kisoka na anataka aitumie Yanga SC kama ngazi ya kupanda kwenda nje kucheza soka ya kulipwa.
Yanga SC wanamsajili Kaseke baada ya kumpoteza kiungo wake bora wa pembeni, aliyekuwa anaweza kucheza pia kama kiungo wa kati na mshambuliaji, Mrisho Ngassa aliyesaini Free State Stars ya Afrika Kusini.
Kaseke pia ana sifa kama Ngassa, mbali na kuteleza pembeni kwa kasi, pia anaweza kucheza kama kiungo wa kati na mshambuliaji.
Ilikuwa vita usiku wa kuamkia leo, viongozi wa Simba na Yanga wakifukuzana kumsaka Kaseke hadi hatimaye wana Jangwani kufanikiwa kumnasa na wamemalizana naye. 
Azam wenyewe walikuwa wanamfuatilia kimya kimya mchezaji huyo- na hawakuwa na spidi ambayo walikuwa nayo Simba SC- maana yake hili ni pigo zaidi kwa wana Msimbazi.  
Deus Kaseke sasa anapatikana Jangwani, Dar es Salaam

PETER MWALYANZI ASAINI SIMBA MIAKA MIWILI



Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES ALAAM
WAKATI Yanga SC wakisherehekea saini ya winga Deus Kaseke, Simba SC nao wamefanya yao mchana huu.
Kiungo hodari mchezeshaji Peter Mwalyanzi kutoka timu ile ile, Mbeya City aliyotokea Kaseke amesaini Mkataba wa miaka miwili kujiunga na Wekundu wa Msimbazi.
Mwalyanzi moja ya viungo waliong’ara katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Barav msimu huu ambaye alikuwa anamchezesha vizuri Kaseke, amesaini ofisini kwa Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya klabu hiyo, Zacharia Hans Poppe, Mbezi, Dar es Salaam.
Na Poppe aliyekuwa na Mjumbe wa Kamati ya Uteneaji, Collins Frisch akasema; “Sisi tunajua wachezaji bora na Simba SC ndiyo nyumbani kwa wachezaji bora,”.
Mjumbe wa Kamati ya Utendaji, Collins Frisch akimshuhudia Peter Mwalyanzi wakati anasaini ofisini kwa Hans Poppe leo

Poppe amesema kwamba Mwalyanzi ni pendekezo la kocha Mserbia, Goran Kopunovic lakini hata washauri wengine wa masuala ya kitaalamu wameridhishwa na uwezo wa mchezaji huyo.
Kwa upande wake, Mwalyanzi ameiambia BIN ZUBEIRY kwamba anajisikia furaha kusaini timu hiyo kubwa, kwani ni hatua moja kubwa mbele katika maisha yake ya soka.
“Mchezaji yeyote anapokuwa anaibuka katika nchi hii, ndoto zake ni siku moja kucheza timu kubwa kama hizi, na mimi nimefurahi sana kujiunga na Simba SC,”amesema.
Mwalyanzi ameongeza kwamba baada ya kusaini, anaomba ushirikiano kutoka kwa wachezaji wenzake, viongozi na mashabiki ili aweze kufanya vizuri.  
Zacharia Hans Poppe akimshuhudia Peter Mwalyanzi wakati anasaini leo Mbezi

Mapema leo, Yanga SC imemsainisha Mkataba wa miaka miwili kiungo mshambuliaji, Deus Kaseke makao makuu ya klabu, Jangwani, Dar es Salaam mbele ya Katibu Mkuu, Dk Jonas Tiboroha na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji, Isaac Chanji.
Kaseke anatua Yanga SC kama mchezaji huru baada ya kumaliza Mkataba wake Mbeya City, aliyoichezea kwa miaka mine iliyopita.
Akizungumza na BIN ZUBEIRY baada ya kusaini Mkataba huo, Kaseke amesema; “Nimefurahi kutua Yanga SC, ni timu ambayo kwa kweli nilikuwa nina ndoto za kuichezea kwa muda mrefu,”.
Kaseke amesema anafahamu changamoto inayomkabili baada ya kusaini Yanga SC, ushindani wa nafasi dhidi ya wachezaji wengine bora waliopo kwa mabingwa hao wa Tanzania.
“Yanga SC ni timu kubwa, ina wachezaji bora na ndiyo maana ni mabingwa. Baada ya kusajili, sasa natakiwa kufanya mazoezi kwa bidii ili niwe katika kiwango bora zaidi na kuwashawishi makocha wanipe nafasi,”amesema.