SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Feb 20, 2016

ALICHOSEMA TAMBWE BAADA YA YANGA KUPATA USHINDI DHIDI YA SIMBA

Mshambuliaji wa Yanga, Amissi Tambwe ambaye amefunga bao la pili katika mechi ya leo ambapo Yanga imeilaza Simba kwa mabao 2-0. Beki Abdi Banda alilambwa kadi ya njano ya pili katika dakika ya 25 na kuzaa nyekundu baada ya kumwangusha Donald Ngoma.

Tambwe alifunga bao katika dakika ya 72 baada ya beki Juuko Murshid kushindwa kumdhibiti baada ya krosi safi ya Geofrey Mwashiuya.
“Tulianza vizuri, mechi ilikuwa na
ushindani mkubwa. Lakini baada ya ile kadi nyekundu, ilitusaidia sisi kuingia kwa wingi katikati na kuwabana Simba.

Mechi ilikuwa nina ushindani sana, Simba walijitahidi kucheza vizuri licha ya kuwa pungufu. Lakini sisi tulikuwa bora zaidi leo,” alisema Tambwe raia wa Burundi.
Hilo ni bao la 15 msimu huu, huku akiwa amebakiza bao moja tu kumkamata Amissi Kiiza ambaye ana mabao 16.

AZAM YAIONESHA ADABU MBEYA CITY KWAO

Mchezo kati ya Mbeya City na Azam fc umemalizika na wenyeji wamekubali kichapo cha goli 3-0 kutoka kwa Azam fc magoli ya Azam yalifungwa na Kipre Tchetche dakika 41, John Bocco dakika ya 63 na Faridi Mussa dakika ya 84.

MAPUMZIKO KATIKA UWANJA WA SOKOINE MBEYA NA HAYA NDIO MATOKEO

Dakika 45 za kipindi cha kwanza katika uwanja wa sokoine mjini Mbeya  zimemalizika na timu ya Azam inaongoza goli moja dhidi ya Mbeya city goli lililofungwa na Kipre tchetche Dakika ya 41.