SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

May 14, 2016

BODABODA FC YAICHAPA BLACK STARS

Image result for SPORTS
Na Haji balou
Timu ya Boda boda fc imeibuka na ushindi wa goli 3-1 dhidi ya Black stars katika mchezo wa ligi ya Mbuzi ya Vijana Cup mchezo uliopigwa katika uwanja wa shule ya  Msingi Muungano.

Magoli ya Boda boda fc yamefungwa dakika ya 27 kupitia kwa kiungo wake mshambuliaji Abuu pia goli la pili lilipatikana kupitia kwa mchezaji Kazumali katika dakika ya 40 na goli la mwisho lilifungwagwa na Mbaraka masoud katika dakika ya 85  na goli la kufutia machozi kwa upande wa Black stars lilifungwa na Ally Omari katika dakika ya 20 ya mchezo.

Ligi  hiyo itaendelea tena hapo  kesho kwa mchezo mmoja kupigwa katika uwaja wa Shule ya Msingi Muungano.