Feb 20, 2015
BALOTELLI AING’ARISHA LIVERPOOL DAKIKA ZA MWISHO
7:31 AM
BAO pekee la mshambuliaji wa kimataifa wa Italia,
Mario
Balotelli limeipa Liverpool ushindi wa 1-0 dhidi ya Besiktas katika
mchezo wa kwanza hatua ya 32 Bora Europa League Uwanja wa Anfield usiku wa jana.
Mshambuliaji huyo wa
zamani wa Manchester City, Inter Milan na AC Milan, alifunga bao hilo
kwa penalti dakika ya 85, kufuatia winga Jordon Ibe kuchezewa faulo
kwenye eneo la hatari.
Mtaliano huyo alimpokonya mpira Nahodha Jordan Henderson na ‘akazinguana’ na Daniel Sturridge kabla ya kwenda kupiga.
Mapema,
Demba Ba na Adam Lallana walipoteza nafasi nzuri za kufunga kwa kila
timu na baada ya ushindi huo mwembamba Anfield, Liverpool inajiweka
katika mazingira magumu kuelekea mchezo wa marudiano nchini Uturuki
Alhamisi ijayo.
Kikosi cha
Liverpool kilikuwa; Mignolet, Can, Skrtel, Sakho, Ibe, Henderson,
Allen/Lovren dk63, Moreno, Lallana/Sterling dk77, Sturridge na
Coutinho/Balotelli dk63.
Besiktas: Gonen, Kurtulus, Franco, Gulum, Ramon, Hutchinson, Kavlak, Tore, Sosa/Ozyakup dk60, Sahan/Frei dk72 na Ba.
Balotelli akishangilia 'kigumu' mbele ya mashabiki wa Liverpool baada ya kufunga
ALICHOSEMA MSUVA BAADA KUIFUNGA PRISONS
7:23 AM
MSHAMBULIAJI wa Mabingwa wa
zamani wa ligi kuu ya Tanzania bara, Dar es salaam Young Africans, Simon
Msuvu baada ya kufanikiwa kuipandisha timu yake katika kilele cha ligi
hiyo kwa kuifungia mabao mawili kati ya matatu katika mchezo dhidi ya
Tanzania Prisons, mshambuliaji huyo amefunguka na kudai kuwa anajisikia
vizuri anapopangwa kucheza na Ngassa au Sherman.
Akizungumza na Shaffihdauda.com
baada ya mchezo huo, Alipoulizw nani kati ya nyota hao wawili
anawakubali akicheza nao, Msuva amesema kuwa yeye ni mchezaji hivyo
haweze kuchagua nani wa kucheza naye lakini akipangwa na yoyote kati ya
Mrisho Ngassa na Khap Sherman lazima atekeleze majukumu yake kama
mchezaji.
“ Ah hiyo ni kazi ya mwalimu,
yeye ndio anajua amuanzishe nani asimuanzishe nani, hayo ni majukumu
yake, Mimi mtu yoyote nitakayepewa nicheze naye nacheza naye” Amesema
Simon Msuva amabye ameibuku shujaa kwa kifumania nyavu mara mbili
akiiteketeza Prisons katika uwanja wao wa Nyumbani Sokoine, Jijini
Mbeya.
Akizungumzia mchezo huo kwa
ujumla Msva amewasifia Prisons kwa kusema kuwa ni timu nzuri lakini
baadhi ya makosa madogo madogo ndio yaliyowagharimu hadi wao kuibuka na
pointi tatu na mabao matatu.
“Prisons ni timu nzuri sio kwamba
ni timu mbovu, sema makosa ambayo wao wliyateda sisi ndio tuliyatumia
na ndio maana tumeweza kutoka na ushindi” Amemalizia Msuva.
Katika mchezo huo Yanga ilipata
bao la kwanza katika dakika ya 3 kupitia kwa Simon Msuva ambaye
aliunganisha kona safi kutoka kwa Mbrazil Andrey Coutinho, Dakika nane
baadaye Beki wa Prisons Lugano Mwagama, akaiandikia Yanga bao lapili
akiwa katika harakati za kuokoa shuti kali lililopigwa na Coutinho na
kumbabatiza na kuingia langoni, hadi dakia 45 za kwanza zinamalizika
Yanga walikuwa wakiongoza kwa bao 2-0.
Kipindi cha pili kilianza kwa
kasi huku Prisons wakitengeneza nafasi za mapema lakini wakashindwa
kuzitumia, Kunako dakika ya 62 kwa mara nyingine Msuva akaiandikia Yanga
bao la tatu baada ya kuunganisha kona iliyochongwa na Andrey Coutinho
na kufanya hadi dakika 90 zinakatika Yanga 3 Prisons 0.