Apr 10, 2015
ARSENAL WATUA ARGENTINA KUKAMILISHA USAJILI WA 'MESSI'
7:59 AM
KIONGOZI wa Arsenal, Dick Law amesafiri kwenda Argentina kukamilisha usajili wa kinda Maxi Romero.
Mkuu
wa mijadala ya klabu hiyo, amepaa hadi Amerika Kusini kumalizia mpango
wa kumsajili mshambuliaji kinda wa miaka 16, ambaye tayari ameanza
kufananishwa na Lionel Messi.
The Gunners wamepiga hatua katika mazungumzo na Velez Sarsfield juu ya usajili wa Pauni Milioni 4.5 wa kinda huyo.
Arsenal ipo karibu kumsajili kinda wa miaka 16, Maxi Romero kutoka Velez Sarsfield kwa Pauni 4.5
Lakini
dili hilo limekuwa likitiwa ugumu na haki za umilikinwa Romero- hivyo
amelazimika kusafiri hadi Argentina kukamilisha mipango hiyo.
wakala wa Romero na klabu yake, Velez wote wana hisa katika kummiliki mchezaji huyo,ambayo inalketa mkanganyiko kwa Arsenal.
Ligi
Kuu ya England hairuhusu mmiliki wa tatu katika sheria za usajill na
suala hilo lazima limalizwe kama ya mchezaji kwenda kuanza kazi The
Gunners.
Romero
anatarajiwa kubaki na Velez, kwa mkopo, kwa angalau misimu miwili zaidi
kabla ya kwenda England kuanza maisha mapya Arsenal. Nyota huyo kinda hajawahi kuchezea kikosi cha wakubwa cha Velez, bali amekuwa akifanya nacho mazoezi kama mchezaji wa kikosi hicho.
ALVES AFUNGASHA, AWAAGA BARCELONA, ANAKWENDA MAN UNITED AU MAN CITY
7:55 AM
BEKI
wa pembeni, Dani Alves anatazamiwa kuondoka Barcelona mwishoni mwa
msimu baada ya mwakilishi wake kuthibitisha mlinzi huyo wa kulia wa
Kibrazil amekataa ofa ya kuongeza Mkataba.
Alves amefurahia mafanikio kwa miaka saba Barcelona, akishinda mataji manne ya Hispania na mawili ya Ligi ya Mabingwa.
Lakini mkonhwe huyo mwenye umri wa miaka 31, hajawa tayari kungeza Mkataba na klabu hiyo ya Nou Camp.
Beki wa kulia wa Brazil, Dani Alves anajiandaa kuondoka Barcelona msimu huu
Wakala
wa mchezaji huyo, Dinorah Santana, ambaye pia ni mke wa zamani wa
Alves, amesema katika Mkutano na Waandishi wa Habari jana kwamba mteja
wake amekataa ofa ya kuongeza Mkataba.
"Majadiliano yamekwisha," amesema mwanamama huyo.
"Ikiwa wamesema hii ni ofa ya mwisho, kisha (majadiliano yamekwisha).
Habari hizo zinatoa fursa kwa klabu ambazo zimekuwa zikimtaka beki huyo hodari kuanza kumfuatilia kuwania saini yake.
Beki
huyo wa zamani wa Sevilla pia ya Hispania, amekuwa akihusishwa na
mpango wa kuhamia Manchester United na Manchester City zote za England,
pamoja na Paris Saint-Germain ya Ufaransa.
Alves amekuwa na miaka saba ya mafanikio Barcelona, akishinda mataji manne ya Hispania na mawili ya Ulaya