SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Feb 14, 2015

TAMBWE ATUPIA ZOTE YANGA IKIICHAPA 2-0 BDF

Hisia17 (2)
YANGA SC imeanza vizuri michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika kufuatia kuichapa mabao 2-0 BDF XI ya Botswana katika mchezo wa kwanza wa raundi ya awali uliomalizika jioni hii uwanja wa Taifa, jijini Dar es salaam.
Mabingwa hao mara 24 wa Tanzania walianza mechi hiyo kwa kuonesha kandanda safi na katika dakika ya kwanza ya mchezo waliandika bao la kuongoza kupitia kwa Mrundi, Amissi Tambwe aliyefunga kwa kichwa akimalizia mpira wa kona wa winga machachari, Simon Msuva.
Tambwe aliyekuwa na umakini leo alitia kambani bao la pili dakika ya 55’ kwa njia ya kichwa akimalizia krosi ya Mrisho Khalfan Ngassa.
Katika vipindi vyote viwili, Yanga walitawala mchezo wakicheza pasi nyingi, lakini walishindwa kutengeneza nafasi nyingi za kufun
Hata hivyo Yanga waliendelea kupoteza baadhi ya nafasi walizopata na wangekuwa makini wangepata ushindi mkubwa zaidi.
Kikubwa walichofanikiwa BDF XI ni kucheza mpira wa kujilinda na kushambulia kwa kushitukiza.
Malengo yao yalikuwa kukwepa kichapo kikubwa ili wakajipange upya nyumbani na ndio utamaduni wa michuano mikubwa barani Afrika.
Kitu wanachotakiwa kujirekebisha Yanga ni kucheza mpira wa pasi wenye madhara, kwasababu wanajikuta wakigongeana pasio nyingi katika eneo lao na kushindwa kuisogeza timu na kulazimisha mashambulizi.
Mechi ya nyumbani lazima utumie mbinu nyingi kufika langoni kwa mpinzani hata kama anacheza soka la kujihami zaidi.
Yanga wanastahili pongezi kwa ushindi huo waliopata kwasababu BDF wanahitaji ushindi wa mabao 3-0 ili kuwatupa nje Yanga.
Kwa upande wa Yanga wanahitaji kufungwa bao 1-0 au sare ya 1-1 ili kusonga mbele na kwa uwezo waliokuwa nao Wanajangwani wanaweza kushinda.
Kikubwa ni kuongeza nidhamu hasa katika kutumia nafasi wanazopata na kutengeneza nafasi nyingi za magoli.
Baada ya Yanga, kesho uwanja wa Azam Complex, Mabingwa watetezi wa ligi kuu Tanzania bara, Azam fc watachuana na mabingwa wa Sudan, EL Merreick katika mechi ya raundi ya kwanza ligi ya mabingwa barani Afrika.

UNAHISI COLLABO NA DAVIDO NI SH NGAPI? HII INAMUHUSU

Davido-DiamondFans wa muziki ni mashuhuda wa Collabo kali ambazo staa wa Nigeria, DAVIDO ameshiriki na kuzifanya kuwa nyimbo kubwa Afrika na Duniani, sikuwahi kusikia juu ya kiwango cha pesa ambacho analipwa ili kufanya collabo, unaweza kuhisi anahitaji pesa kiasi gani ili afanye collabo yoyote?
Kwenye moja ya interview alizofanyiwa hivi karibuni Davido amesema anafanya muziki kwa sababu anaupenda, haitaji malipo yoyote kutoka kwa msanii ambaye anafanya naye Collabo, hakumbuki kama aliwahi kuhitaji malipo kwa ajili ya kushirikishwa kwenye ngoma yoyote.
I don’t charge for collabos, and I don’t think I have in the past. The truth is I love music and I just do it out of the love. So, I do it for free”– Davido.
Mbongo Fleva wetu DIAMOND PLATNUMZ ni mmoja ya mastaa ambao walipata nafasi kufanya collabo na DAVIDO na ikawa hit kubwa Afrika 2014.

JUAN MATA KUTIMKIA BARCELONA

25AA6F0400000578-2953414-image-m-2_1423912282584
KIUNGO wa Manchester United, Juan Mata ameingia katika rada za usajili za Barcelona kwa mwaka 2016 na tayari miamba hiyo ya Katalunya imeshaanza mipango ya usajili kwa mwaka ujao.
Kikosi cha  Luis Enrique bado kinatumikia kifungo cha kutosajili walichopewa na FIFA baada ya kuvunja sheria za uhamisho kwa wachezaji wenye umri chini ya miaka 18.
Kwa mwaka 2015 Barcelona hawatakiwi kusaini mchezaji yeyote, lakini Mata ambaye hana uhakika wa namba katika kikosi cha kwanza cha Van Gaal anahusishwa kujiunga na miamba hiyo ya Nou Camp, kwa mujibu wa gazeti la Hispania la Mundo Deportivo.

TAMBWE APELEKA FURAHA JANGWANI

Magoli mawili ya mshambuliaji Amisi Tambwe yameipa ushindi timu ya Yanga  dhidi ya PDF ya Botswana katika mchezo uliochezwa jioni hii

ALONSO ATAJA KIKOSI CHAKE BORA LIGI YA MABINGWA

AKIWA amecheza kwa zaidi ya muongo mmoja Ulaya, hapana shaka ni sahihi kusema Xabi Alonso anamjua mchezaji mzuri. 
Akiwa ameshinda taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya mara mbili, kiungo huyo wa zamani wa Liverpool ametaja kikosi cha wachezaji 11 bora wa muda wote katika zama zake wa Ligi ya Mbingwa Ulaya kwa mtazamo wake.
Kwa sasa akiwa anachezea Bayern Munich, Mspanyola huyo amemteua kipa wa timu yake, Manuel Neuer kuwa mlinda wa kikosi, ambacho ndani yake kuna washambuliaji Lionel Messi wa Barcelona na Cristiano Ronaldo wa Real Madrid.
Kikosi kamili cha Alonso ni; Manuel Neuer, Philip Lahm, Sergio Ramos, Carles Puyol, David Alaba, Zinadine Zidane, Paul Scholes, Xavi, Steven Gerrard, Cristiano Ronaldo na Lionel Messi.    
Alonso laughs with Sportsmail's Jamie Carragher earlier this season over in Germany
Alonso akifurahia na Mwandishi wa Sportsmail, Jamie Carragher mapema msimu huu Ujerumani


P
PP



 The central midfielder now plies his trade with Bundesliga champions Bayern Munich

SCHOLES ANENA

 
Aliyekuwa kiungo wa kati wa kilabu ya Manchester United Paul Scholes amesema kuwa mtindo wa timu hiyo ni m'bovu na unaenda kinyume na utamaduni wa kilabu hiyo wa kushambulia.
Mkufunzi Luois Van Gaal ameutetea mtindo huo baada ya kocha wa West Ham Sam Allardyce kuiita timu hiyo ''Long Ball United'' akiashiria mtindo wa pasi ndefu wa timu hiyo.
Scholes aliandika katika gazeti la independent nchini Uingereza :''kwa sasa ninashindwa kufurahia mechi za Man United''.
''Mara nyengine mtindo unotumiwa haufai''.
''Ukitaka kushinda wapinzani wako ni lazima ufanye mashambulizi na ili kufanikisha hilo lazima ujue kwamba pia kuna hatari yake''.
''Lakini ni wachezaji wachache katika timu hiyo ambao wako tayari kuwa jasiri."aliongezea Scholes.

PELLEGRINI: HATUMTEGEMEI YAYA

 
Mkufunzi wa Manchester United Manuel Pelegrini ana matumaini kwamba Manchester City inaweza kupambana ili kushinda taji la ligi kuu nchini Uingereza bila nyota wake Yaya Toure.
City haijashinda mechi yoyote ya ligi ya EPL tangu Toure aelekee Afrika katika michuano ya mataifa ya Afrika.
''Ni mchezaji muhimu sana na ni muhimu kwa yeye kurudi kikosini.Lakini hatutegemei mchezaji mmoja,lazima tushinde bila yeye'',.
City iko katika nafasi ya pili ikiwa nyuma ya Chelsea kwa pointi saba na hawajashinda katika mechi zote tano za ligi walizocheza,Hatahivyo Pelegrini anasema kuwa wanawaza kuhimili presha hiyo.

LEO SIKU YA WAPENDANAO DUNIANI, LAKINI UNAJUA VITU HIV


download
KIVYAKO VYAKO,,,,,
Mshambuliaji wa kimataifa wa England,,, ambaye kwa sasa anakipiga Sunderland,,, (Jamein defoe),,, ameweka rekodi ya kuzifunga timu zote za ligi kuu England,,, huku mhanga wa kipigo kikubwa wakiwa ni Man city,,, waliofungwa goli 6 ,,,
,,,,,,,,,,, JILIWAZE KIDOGO,,,,,,
Arsenal ndio timu pekee kutoka England iliyoshiriki mara nyingi zaidi ligi ya mabingwa,,, kuliko timu yoyote ile mpaka sasa,,, na pia ndio timu pekee kutoka England iliyoshiriki michuano ya ligi ya mabingwa ulaya bila kutwaa ubingwa,,, na wala hawana ndoto za kufanya hivyo siku za karibuni,,,
,,,,,,,,KIFUTA JASHO,,,,
LIVERPOOL ndio timu pekee inayoshiriki ligi kuu England kwa sasa,, ambayo haijapoteza mchezo toka mwaka huu 2015 uanze,, na ndio mana
haikushangaza mchezaji bora wa mwezi January kapewa Emre can,,, na kocha bora January Brendan Rogers,,,
,,,,,,,,HAYAKUHUSU,,,,,,,
Combination ya Radamel Falcao na Robin van Persie inachukuliwa ndio combination mbovu kuliko zote zilizowahi kutokea Man Utd,,, ukosefu wao wa magoli na kushindwa kuelewewana kiuchezaji kumepelekea captain Rooney kususa kuwapelekea mipira na kuamua kucheza kama defense midfielder ili kuwafundisha wajibu,,,
,,,,TUKUTANE TAIFA LEO

FA CUP KUENDELEA LEO

1383715-29670686-640-360
RAUNDI ya tano ya kombe la FA nchini England inaendelea leo kwa mechi nne kupigwa.
West Brom wako nyumbani kuikaribisha West Ham United, wakati Derby inachuana na Realding.
Mechi nyingine inawakutanisha Blackburn dhidi ya Stoke City.
Wekundu wa Anfield, Liverpool wanashuka dimbani ugenini kuchuana na Crystal Palace.
Michuano hiyo itaendelea kesho jumapili (Februari 15) kwa mechi tatu kupigwa.
Aston Villa wataikaribisha Leicester, Bradford watachuana na Sunderland, wakati Arsenal watakuwa nyumbani kupepetana na Middlesbrough.

OKWI NTAKOMAA NA YANGA MPAKA KIELEWEKE



Baada ya kipa Juma Kaseja kufikishwa mahakamani na Klabu ya Yanga kwa madai ya kuvunja mkataba na klabu hiyo, mshambuliaji wa Simba, Emmanuel Okwi amesisitiza kuwa atapambana mpaka mwisho na Yanga ili wamlipe haki yake anayoidai.

Okwi, kupitia Kampuni ya Agaba Muhairwe & Co Advocates ya Kampala, Uganda, alifungua kesi hivi karibuni dhidi ya Yanga akiidai klabu hiyo dola 62,000 (Sh milioni 107) kwa madai ya kukiuka mkataba aliokuwa amesaini na klabu hiyo, madai ambayo yameshafika kwenye Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).

Okwi amesema kuwa awali aliwaandikia barua Yanga kuhusu madai yake hayo ikiwa ni fedha za makubaliano ya usajili ambazo hawajammalizia, lakini uongozi huo ulikaa kimya.
Anasema baada ya hapo akaandika barua nyingine ya kuwakumbusha juu ya madai hayo yaliyotokana na hukumu ya Kamati ya Nidhamu ya TFF.
Mchezaji huyo raia wa Uganda aliongeza kuwa kutokana na hali ya kuonyesha kupuuza jambo hilo, sasa yupo kwenye hatua mpya ya kuwaandikia barua nyingine itakayokuwa na shinikizo la kulipwa mara moja, la sivyo atapeleka shitaka lake mbele zaidi.
“Nipo katika mchakato wa kuona nifanye nini na mwanasheria wangu baada ya barua za awali kutojibiwa, nimesikia kutoka kwao kuwa wamekata rufaa juu ya ile barua yangu na kutaka kunishtaki Fifa bila ya kunitaarifu kwa kunipa barua juu ya kile kinachoendelea.
“Nitatoa shinikizo la kulipwa ndani ya muda fulani. Wasipofanya hivyo nitapeleka shitaka langu ngazi za juu zaidi,” alisema Okwi.

OMOG KUWEKA REKODI LEO


Kocha Mkuu wa Azam FC, Joseph Omog, raia wa Cameroon, anatarajiwa kuweka rekodi atakapoiongoza timu yake hiyo kuvaana na mabingwa wa Sudan, El Merreikh katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi jijini Dar.


Kocha huyo ataingia kwenye vitabu vya kumbukumbu kwa kuwa kocha wa kwanza kuiongoza timu hiyo kucheza mchezo wa ligi hiyo inayosimamiwa na Shirikisho la Soka Afrika (Caf).

Msimu uliopita Azam ilishiriki Michuano ya Kombe la Shirikisho, lakini msimu huu wamepata nafasi hiyo baada ya kufanikiwa kubeba ubingwa wa Ligi Kuu Bara msimu uliopita.

Kocha huyo anaiongoza Azam kwa msimu wa pili baada ya kuanza kuinoa timu hiyo msimu uliopita akichukua nafasi ya Stewart Hall, raia wa Uingereza.


MSUVA USHINDI LAZIMA

Kiungo mwenye kazi wa Yanga, Simon Msuva, naye hakuwa nyuma kuelekea katika mchezo huo baada ya kufunguka kwa kusema kuwa wapinzani wao  BDF XI hao lazima wajipange kwa kuwa yupo fiti.

Yanga  inashuka dimbani kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kuwavaa BDF XI ya Botswana katika mechi ya kwanza ya Kombe la Shirikisho.
 
“Tumejipanga vizuri, lengo letu ni kuhakikisha tunanza kwa kasi kisha kuwamaliza mapema kwa kuwa nia yetu wote ni kusonga hatua inayofuata ya michuano hiyo,” alisema Msuva.
Yanga italazimika kushinda na ikiwezekana kwa mabao mengi zaidi ili kuhakikisha wanajiweka katika mazingira mazuri kabla ya mechi ya marudiano.