SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Mar 19, 2015

MAN CITY KUMUUZA YAYA TOURE

YayaToure_1509466a

Mabingwa wa ligi ya Uingereza Manchester City watamuuza Yaya Toure msimu huu katika mpango unaolenga kuwauza wachezaji wengine wa kilabu hiyo kwa lengo la kununua wachezaji chipukizi watakaoongozwa na mchezaji Kevin De Bruyn wa Wolfsburg.
Kushindwa kwa kilabu hiyo na Barcelona katika mechi ya kufuzu kwa robo fainali ya kombe la vilabu bingwa Ulaya kumethibitisha kwamba mabadiliko makubwa yanahitajika katika kilabu hiyo.
Katika wachezaji kumi na moja walioanzishwa katika mechi dhidi ya Barcelona ni Sergio Aguerro mwenye umri wa maka 26 aliye chini ya umri wa miaka 27.
Huku Aguerro,Joe Hart,Vincet Kompany,Fernandinho na David Silva wakiwa na maisha marefu katika kilabu hiyo ,waliosalia huenda wakauzwa.
Hii inamaanisha kwamba Yaya Toure,Bacary Sagna,Martin Demichelis,Alkesandar Kolarov ,Samir Nasri na James Milner ambaye kandarasi yake inaisha hatma yao haijulikani.
Kati ya wachezaji ambao hawakuanzishwa katika uwanja wa Nou Camp siku ya jumatano usiku,Gale Clichy,Pablo Zabaleta,Jesus Navas,Fernandinho,Steven Jovetic na Edin Dzeko huenda pia wakauzwa.
Frank lampard amesema kuwa anaondoka ili kujiunga na kilabu ya New York City nchini Marekani.

KIBIBI KIZEE CHA TURIN CHAFANYA BALAA ULAYA, HUYO TEVEZ MOTO WAKE USIKIE HIVYO HIVYO!

‘KIBIBI KIZEE’ cha Turin kimeinuka tena. Habari ndiyo hiyo. Juventus ya Italia imefuzu Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, kufuatia ushindi wa mabao 3-2 ugenini dhidi ya Borussia Dormund usiku huu Uwanja wa Westfalenstadion, Dortmund, Ujerumani.
Juve sasa inakwenda Robo Fainali kwa ushindi wa jumla wa mabao 5-1, baada ya awali kupata ushindi mwembamba nyumbani wa 2-1. 
Mshambuliaji wa zamani wa Manchester United, Carlos Tevez aliifungia Juve bao la kwanza dakika ya tatu, kabla ya Alvaro Morata kufunga la pili dakika ya 70 kwa pasi ya Muargentina huyo. 
Tevez aliyewahi pia kuchezea Manchester City, aliifungia Juve bao la tatu zikiwa zimesalia dakika 10 na hicho kinakuwa kipigo cha nne kwa 
Dortmund katika mechi nne walizokutana na Juventus kwenye michuano ya Ulaya.
Timu nyingine zilizotinga Robo Fainali ni PSG, Monaco zote za Ufaransa, Atletico Madrid, Real Madrid, Barcelona, FC Porto na Bayern Munich.
Droo ya Robo Fainali itapangwa Ijumaa Saa 7:00 mchana kwa saa za Afrika Mashariki.
The Argentine striker is mobbed by his Juventus team-mates after his early strike gave the Serie A giants a 3-1 aggregate lead 
Carlos Tevez akipongezwa na wenzake baada ya kufunga mabao mawili katika ushindi wa 3-0 dhidi ya Borussia Dortmund usiku huu 

BARCA YAISINDIKIZA NA 1-0 MAN CITY EUROPA LEAGUE

BAO pekee la Ivan Rakitic limeipa Barcelona ushindi wa 1-0 dhidi ya Manchester City katika mchezo wa marudiano hatua ya 16 Bora Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Rakitic alifunga bao hilo dakika ya 31, akimalizia krosi ya Lionel Messi na sasa Barca inafuzu Robo Fainali kwa ushindi wa jumla wa mabao 3-1, baada ya awali kushinda 2-1 England.
Katika mchezo huo, mshambuliaji wa Manchester City, Sergio Aguero alikosa penalti dakika ya 78 ambayo iliokolewa na kipa Marc-Andre ter Stegen. Penalti hiyo ilitolewa baada ya yeye mwenyewe kuangushwa na Gerard Pique.
Man City imeungana na timu nyingine mbili za England, Chelsea na Arsenal kuaga katika 16 Bora ya Ligi ya Mabingwa na sasa zote zitahamia kwenye Europa League.
Kikosi cha Barcelona kilikuwa; Ter Stegen, Alves/Adriano dk90, Pique, Mathieu, Alba, Rakitic/Rafinha dk84, Mascherano, Iniesta, Messi, Suarez na Neymar.
Man City: Hart, Sagna, Kompany, Demichelis, Kolarov, Nasri/Navas dk46, Toure/Bony dk72, Fernandinho, Milner/Lampard dk87, Silva na Aguero.
Barcelona completed their two-legged victory over Manchester City to book a place in the quarter-finals of the Champions League
Wachezaji wa Barcelona wakimpongeza Ivan Rakitic baada ya kufunga bao pekee dhidi ya Manchester City usiku huu

KURASA ZA MWANZO NA ZA MWISHO ZA MAGAZETI YA MICHEZO ZIPO HAPA

.
.
.
.
.
.
.
.
.