SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Feb 28, 2015

SAMATTA :SINA FURAHA TP MAZEMBE


samatta_cska_2
Samatta alikwenda kufanya majaribo CSK Moscow ya Urusi, lakini hakufanikiwa baada ya kupata majeruhi ya kifundo cha mguu
Na Baraka Mbolembole, Dar es Salaam,
 Mshambulizi wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Samatta ameweka wazi kuwa ataachana na mabingwa mara nne wa kihistoria wa Afrika, TP Mazembe mara baada ya kumalizika kwa mkataba wake. Akizungumza na mwandishi wa mtandao wa www.shaffihdauda.co.tz muda mfupi uliopita mshambulizi huyo wa Taifa Stars amesema kuwa hana furaha katika timu hiyo ya Congo.

 Samatta ambaye alipata nafasi ya kufanya majaribio katika klabu ya CSKA Moscow ya Urusi mwezi uliopita amepewa ofa nyingi barani ulaya na kama ataendelea kuchezea TP basi atakuwa ni mchezaji anayelipwa pesa nyingi zaidi barani Afrika. Hivi karibuni kuna vyombo vya habari ambavyo viliripoti kuwa mchezaji huyo ana furaha kuendelea kuichezea TP lakini amesema huo ni uzushi mkubwa.


 ” Sina furaha hapa ( TP Mazembe) nitaondoka wakati wa majira ya usajili katikati ya mwaka na sitaongeza mkataba” anasema Samatta. Ni wapi anakwenda, nini kinachomuondoa TP Mazembe, tafadhaLi endelea kufuatilia mtandao huu wa www.shaffihdauda.co.tz... na www.hajibalou.blogspot.com Utapata kujua wapi mchezaji huyo anakwenda. Je, tayari ameruhusiwa na Katumbi Moies mmliki wa TP?…..

WALICHO FANYIWA AZAM FC SUDAN KABLA YA MECHI YA LEO


Azam FC leo saa mbili usiku itajitupa kwenye uwanja wa AlMerrikh kukwaana na Al Merrikh SC.
Azam FC ambayo ilitua hapa Khartoum Jumanne 24/2/2015 imekuwa katika hali nzuri tangia kuwasili. Vijana wa kitanzania wanaosoma hapa Khartoum wamekuwa wenyeji wetu.
Azam FC imekodi Apartment nzima, tumekuwa tukiishi kama nyumbani, tunapika wenyewe, tuna ulinzi wa kutosha wa kambi, na walinzi wetu ambao tumesafiri nao toka Dar es Salaam wakiongozwa na afisa wa usalama wa Taifa wamekuwa wakifanya doria masaa 24.
Tulipowasili Khartoum, wapinzani wetu walijaribu kucheza mchezo mchafu wa kutuchanganya kisaikolojia kwa kuleta mabasi mawili mabovu kutupolea lakini walishangazwa kuona Azam FC ikiachana na basi lao na kupanda basi lingine zuri lililoandaliwa na viongozi wa Azam FC waliotangulia siku tatu kabla.
Jana wakati timu inaenda kufanya mazoezi uwanjani mashabiki wa Merrikh walijipanga barabarani na kurusha vumbi, makopo, mawe nk lakini polisi waliokuwa kwenye magari maalum wakisaidiwa na wanajeshi walifanikiwa kuwadhibiti.
Wenyeji wanasema mashabiki wa Merrikh ni wakorofi na wamekuwa na kawaida ya kufanya fujo kwa timu ngeni.
Benchi la ufundi la Azam FC linaloongozwa na Joseph Omog limesema hawana wasiwasi kabisa kwani wamewaandaa vijana kwa ajli ya mchezo wa leo.
CHANZO AZAM FC PAGE

DI MARIA AJUTA KUJIUNGA MAN UNITED

Mchezaji wa Manchester United Angel Di Maria
Mchezaji nyota ambaye pia ni kiungo wa kati wa Manchester United Angel Di Maria amesema kuwa alifanya makosa kujiunga na Kilabu ya Manchester United msimu uliopita.
Raia huyo wa Argentina amejaribu kuingiana na maisha ya ligi ya Uingereza na majuto yake yataongeza uvumi kwamba anapanga kuondoka katika kilabi hiyo miwshoni mwa msimu huu.
Mwandishi wa Uhispania Manolete Esteban anadai kwamba mchezaji huyo wa zamani wa kilabu ya Real Madrid ambaye amekosolewa kwa uchezaji wake amewaambia marafiki zake kwamba anajuta kuondoka katika kilabu ya Real Madrid.
Esteban aliiambia runinga ya Uhispania katika kipindi cha La Goleada kwamba Di maria alikiri kwa rafikiye katika kilabu ya Real Madrid kuwa anajuta kujiunga na Manchester United.

SIMBA YATAKATA TAIFA AJIBU APIGA HAT-TRICK


simba ushindiNa Richard Bakana, Dar es salaam
Klabu ya Simba ya Jijini Dar es salaam leo imefanikiwa kutoa dozi ya msimu kwa maafande wa Tanzania Prisons, baada ya kuwafunga mabao 5-0 katika mchezo wa ligi kuu ya Tanzania bara uliopigwa katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.
 Katika mchezo huo mshambuliaji wa Simba Ibrahim Ajib ndio aliibuka kinara wa kufumania nyavu baada ya kutupia kambani bao 3 (Hat trick) ambapo katika kipindi cha pili alipumzishwa baada ya kupewaa kadi njano.
Simba walijipatia ushindi huo kupitia kwa Ibrahim Ajib dakika ya 15, dakika 21 na dakika ya 42 kwa mkwaju wa penati, na kufanya muamuzi wa mchezo huo Odongo ampatie mpira wake kwa kazi nzuri aliyoifanya.
Baada ya kutengeneza nafasi nyingi za mabao Okwi naye akaiandikia Simba bao la nne katika dakika ya 74 kabla ya Ramadhan Singano kumaliza kazi kwa kufunga bao la tano katika dakika ya 82 kufatia kazi nzuri ya Emanuel Okwi.
Kwa ushindi huo Simba inakuwa imeweka rekodi nzuri ya kufunga mabao mengi katika mchezo huku ikiwa ni salamu kuelekea mchezo na Yanga wiki kesho Machi 8.

VAN GAAL ATAJA TATIZO LA MAN UNITED


Kilabu ya Manchester United haiwezi kushinda taji la ligi kwa kuwa haina mshambuliaji mwenye uwezo wa kufunga mabao 20 kwa msimu.
Meneja Luois Van Gaal amesema kuwa mshambuliaji mwenye mabao mengi katika klabu hiyo ni Van Persie mwenye mabao 10 pekee ikilinganishwa na Diego Costa na Sergio Aguerro ambao wamefunga mabao 17 kila mmoja wao.
Radamel falcao
''Ni kweli'',alisema Van Gaal.
''Robin van Persie hawezi kukataa,Falcao naye hawezi kupinga na Rooney hachezi katika safu ya mashambulizi.
Van Persie
MKufunzi huyo wa Old Trafford amekuwa akikosolewa kwa kumchezesha Wayne Rooney katika kiungo cha kati,huku Radamel Falcao akipewa fursa chache kwa madai kwamba hayuko shwari.
Van Gaal alisema:''Kwa sasa hatuna mshambuliaji ambaye anaweza kufunga mabao 20''.

KAPTENI JOHN KOMBA ALIYEIMBA 'MGENI' AFARIKI DUNIA


MBUNGE wa Mbinga Magharibi na mkurugenzi wa Tanzania One Theatre (TOT) Kapten John Komba amefariki dunia muda huu.
Katibu mipango wa TOT, Gasper Tumaini ameithibitishia BIN ZUBEIRY jioni hii kwamba, Komba amefari na taarifa zaidi zitatoka hapo baadaye.
Kwa muda mrefu tangu amestaafu jeshi, Komba amekuwa Mkurugenzi wa kikundi cha sanaa cha Chama cha Mapinduzi (CCM), kiitwacho TOT na miaka ya karibuni amekuwa akitamba na wimbo Mgeni, unahusu ugonjwa hatari wa Ukimwi.