SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Apr 15, 2015

RONALDO NA MESSI KUCHEZA TIMU MOJA, NI KATIKA 'GEMU' LA UEFA ALL STAR

WANASOKA wawili mahasimu, Lionel Messi na Cristiano Ronaldo wanaweza kujikuta katika kikosi kimoja kucheza mechi ya UEFA All-Star itakayohusisha wachezaji bora zaidi Ulaya, kwa mujibu wa taarifa kutoka Hispania.
Wanaweza kuchezea 'Team South', nyota wa Ulaya Kusini ambao watatoka katika Ligi za La Liga ya Hispania, Serie A ya Italia na Ligue 1 ya Ufaransa dhidi ya 'Team North', nyota wa Ulaya Kaskazini wanaotoka Ligi Kuu ya England, Bundesliga ya Ujermani na Ligi Kuu ya Urusi.
Gazeti la Mundo Deportivo limeripoti kwamba kampuni ya Masoko imeiomba UEFA juu ya mchezo huo na kupendekeza ifanyike kila mwaka baada ya kuvutiwa na na mechi ya NBA All-Star baina ya Western na Eastern Conferences (Kanda ya Mashariki na Magharibi).
Messi and Ronaldo would be the star attractions in the 'North vs South' All-Star fixture
Messi na Ronaldo wanaweza kuungana katika kikosi kimoja kucheza mechi kati ya 'North dhidi ya South' All-Star

WANAOTARAJIWA KUWAMO VIKOSI VYA ALL-STAR YA UEFA 

South: Buffon; Danilo, Sergio Ramos, Pique, Thiago Silva; Messi, Pogba, Koke, Neymar; Cristiano Ronaldo, Ibrahimovic
North: Neuer; Terry, Hummels, Alaba; Robben, Di Maria, Silva, Reus; Alexis, Aguero, Hazard
Wachezaji wa kuchezea timu hizo watachaguliwa kwenye mitandao kutokana na kura za mashabiki na klabu moja haitapewa fursa ya kutoa zaidi ya wachezaji watatu.
Lakini pamoja na ukweli huo, uhondo wa mecbi hiyo utaletwa na nyota wa Barcelona, Messi na Neymar kuungana na mahasimu wao wa Real Madrid, Ronaldo na Gareth Bale.
Nyota wengine wa Kusini wanaopewa nafasi kubwa ya kuwamo kwenye kikosi cha 'Team South' ni pamoja na mshambuliaji wa Paris Saint-Germain, Zlatan Ibrahimovic na kiungo wa Juventus, Paul Pogba.
Upande wa 'Team Kaskazini' bila shaka nyota kama washambuliaji wa Manchester City, Sergio Aguero, Man United, Wayne Rooney, winga wa Chelsea, Eden Hazard, winga wa Manchester United, Angel di Maria na kipa wa Bayern Munich, Manuel Neuer wanatarajiwa kuwamo.

KURASA ZA MAGAZETI YA YA MICHEZO LEO APRIL 15 ZIPO HAPA

DSC01342
DSC01343
DSC01344
DSC01345