SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Mar 17, 2016

MAAMUZI MENGINE YA SIMBA KUHUSU HASSAN ISIHAKA


Na Haji balou
SIMBA SC imemfungia kwa mwezi mmoja pamoja na kumvua Unahodha, beki wake wa kati chipukizi, Hassan Isihaka baada ya kukutwa na hatia ya utovu wa nidhamu.
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Simba, Hajji Manara amewaambia Waandisji wa Habari leo kwamba hatua hiyo imefikiwa baada ya mchezaji huyo kukutwa na hatia ya kumtolea 'maneno machafu' kocha wa klabu, Mganda Jackson Mayanja.
Manara amesema adhabu hiyo kwa Isihaka ambaye pia ni beki wa kati wa timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars ni onyo kwa wachezaji wengine wa klabu hiyo wasifikirie kufanya vitendo vya utovu wa nidhamu katika timu.
Isihaka anadaiwa 'kumjibu utumbo' kocha Mayanja kabla ya mechi ya jana ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) dhidi ya Singida United Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam mwezi uliopita.
Inadaiwa Isihaka alimtukana Mayanja kwenye chumba cha kubadilishia nguo Uwanja wa Taifa kabla ya mchezo huo wa michuano ya Kombe la Azam Sports Federation ambao SImba ilishinda 5-1. 
Siku moja baada ya kudaiwa kufanya kitendo hicho, Isihaka alisimamishwa kwa muda usiojulikana kabla ya mchezaji huyo kuomba radhi siku mbili baadaye.

SIMBA WAMETOA MAAMUZI YAO KUHUSU VIPORO VYA YANGA NA AZAM FC

Image result for haji manara


Na Haji balou

Klabu ya Simba imeweka msisitizo kwamba mechi ya Jumamosi dhidi ya Coastal Union ni ya mwisho kwao hawatacheza tena hadi Yanga na Azam FC wacheze mechi zao za viporo.

Simba itakuwa Tanga Jumamosi kuivaa Coastal Union katika mechi ya Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Mkwakwani.

Mkuu wa kitengo cha habari cha Simba, Haji Manara ambaye jana alilizungumza hilo, leo amesisitiza kwamba watakuwa na msimamo huo kwa sababu kuu tatu.

“Moja, hakuna sababu ya timu nyingine kuwa na viporo hata baada ya kucheza mechi za kimataifa,” alisema Manara.

“Mbili, hakukuwa na sababu Yanga isicheze Jumatano. Baada ya sisi kucheza Tanga wao watakuwa na viporo vitatu, unafikiri tunaweza kumaliza ligi kugombea ubingwa kwa timu nyingine kuwa na michezo mitatu mkononi. Umewahi kuona kwenye ligi ipi makini duniani?”

“Tatu, kama zitabaki na viporo vitatu, timu nyingine zimeishacheza. Maana yake zipo ambazo zitakuwa zimeteremka daraja. Ushindani utakuwa hakuna tena, wakikutana nazo inakuwa ni rahisi sana kwao kushinda.”


Simba ndiyo ipo kileleni ikiwa na pointi 54, wakati Yanga na Azam FC ziko katika nafasi ya pili na tatu, kila moja ikiwa na pointi 50 na kila moja ina mechi mbili mkononi.