SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Feb 24, 2015

SWALI MAN CITY NDIO WAFALME WAPYA WA JIJI LA MANCHESTER??

SWALI LIMEULIZWA KUPITIA KATIKA MTANDAO WA DAILYMAIL WA UINGEREZA. KWAMBA WAKATI MAN CITY WAKO BUSY WAKIJIANDAA NA MECHI YA LIGI YA MABINGWA ULAYA, JIRANI ZAO MAN UNITED, WAKO BUSY WANACHEZA NA WATOTO. JE, MAN CITY NDIYO WAFALME WAPYA WA JIJI LA MANCHESTER KAMA ILIVYOKUWA MAN UNITED WAKATI WA ALEX FERGUSON?

AZAM KUWAFUATA AL MERREIKH LEO USIKU


azamNa. Richard Bakana, Dar es salaam
MABINGWA watetezi wa ligi kuu ya Tanzania bara na wawakirikishi kwenye michuano ya klabu bingwa barani Afrika, Azam FC, leo wanatarajia kukwea pipa moja kwa moja kuwawinda Al Merreikh katika mchezo wa marudiano huko Sudan.
Akizungumza na Shaffihdauda.com Afisa habari wa Azam, Jafar Idd Maganga, amesema kuwa kikosi hicho kitaondo katika uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Mwl Julius Nyerere,  jijini Dar e salaam majira ya saa mbili usiku kwa ndege ya Kenya Airways.
“Mipango imekamilika na leo usiku tunatarajia kuondoka kwa usafri wa ndege ya Kenya, kikubwa tunajua tunaenda kucheza mchezo wa marudiano, tumejiandaa tokazamani” Amesema Jafar Idd.
Kama utakuwa na kumbukumbu, kwenye mchezo wa kwanza kati y Azam FC na Al Merreikh uliopigwa Februari 15 katika Uwanja wa Chamazi, Dar es salaam, Wanalambalamba waliweza kuibuka na ushindi wa bao 2-0 mabao yakifungwa na Didier Kavumbagu pamoja na nahodha John Bocco.
Ili Azam FC iweze kusonga mbele katika michuano hiyo, siku ya Jumamosi Februari 28 majira ya saa mbili usiku ambapo mchezo huo ndio utaanza, Watanzania hao itawalazimu wapate ushindi au sare.
Na. Richard Bakana, Dar es salaam
MABINGWA watetezi wa ligi kuu ya Tanzania bara na wawakirikishi kwenye michuano ya klabu bingwa barani Afrika, Azam FC, leo wanatarajia kukwea pipa moja kwa moja kuwawinda Al Merreikh katika mchezo wa marudiano huko Sudan.
Akizungumza na Shaffihdauda.com Afisa habari wa Azam, Jafar Idd Maganga, amesema kuwa kikosi hicho kitaondo katika uwanja wa Ndege wa kimataifa wa Mwl Julius Nyerere,  jijini Dar e salaam majira ya saa mbili usiku kwa ndege ya Kenya Airways.
“Mipango imekamilika na leo usiku tunatarajia kuondoka kwa usafri wa ndege ya Kenya, kikubwa tunajua tunaenda kucheza mchezo wa marudiano, tumejiandaa tokazamani” Amesema Jafar Idd.
Kama utakuwa na kumbukumbu, kwenye mchezo wa kwanza kati y Azam FC na Al Merreikh uliopigwa Februari 15 katika Uwanja wa Chamazi, Dar es salaam, Wanalambalamba waliweza kuibuka na ushindi wa bao 2-0 mabao yakifungwa na Didier Kavumbagu pamoja na nahodha John Bocco.
Ili Azam FC iweze kusonga mbele katika michuano hiyo, siku ya Jumamosi Februari 28 majira ya saa mbili usiku ambapo mchezo huo ndio utaanza, Watanzania hao itawalazimu wapate ushindi au sare.

STAND NA SIMBA ZAINGIZA MIL 31, MBEYA CITY, YANGA MIL 74


Mchezo uliokuwatanisha wenyeji timu ya Stand United kwenye Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga dhidi ya timu ya Simba umeingiza jumla ya Sh milioni 31.

Juma la watazamaji 5,439 waliingia uwanjani kushuhudia mchezo huo, ambao timu ya Stand imepata mgao wa tsh. 6,564,268.22 na Simba wakipata mgao wa tsh. 4,661,581.78.

VAT (18%) tshs. 4,763,135.59 huku FA  mkoa wakipata tsh.665,940.25, FDF tsh. 1,141,611.86, Bodi ya Ligi Sh 1,522,149.15, Gharama za mchezo tsh. 1,617,283.47, Uwanja tsh. 2,854,029.66, Gharama ya tiketi Sh 1,593,000,00, FDF tsh. 2,921,000.00, TFF tsh.2,921,000.00

Katika uwanja wa Sokoine mbeya jumla ya Sh 74,600.000.00, zilipatikana kutokana na watazamaji 14,920 waliokata tiketi kushuhudia mchezo huo,  VAT(18%) tsh.11,379,661.02, CDRB (5%)  Sh 3,730.000.00.

FDF Sh 5,222,000,00, TFF Sh 2,238,000.00, Uwanja Sh 7,804,550,85, Gharama za mchezo tsh 4,442,578.81, Bodi ya Ligi Sh 4,162,427,12. Chama cha soka mkoa (FA) Mbeya kimepata Sh1,821,061.86, FDF(TFF) Sh 3,121,820.34, wenyeji timu ya Mbeya city wakipata Sh 17,950,466.95 na klabu ya Yanga tsh. 12,747,438.98

RONALDO AINGIA KWENYE LIST YA MASHUJAA WA TATU REAL MADRID


criiii
Mreno Cristiano Ronaldo ni staa wa soka Duniani ambaye kutokana na ubora wake mara nyingi kwenye kurasa za story za michezo huwa zinaandika kuhusu yeye.
Neema imeendelea kubaki upande wake, siku chache zilizopita ameongoza kikosi cha Real Madrid kwenye ushindi mzuri walioupata, goli 2-0 ambapo walikuwa wakicheza na timu ya Elche, leo Christiano Ronaldo anaingia kwenye taarifa nyingine ya kuwa staa ambaye anashika nafasi ya tatu kwa kuifungia timu ya Real Madrid magoli mengi zaidi katika historia ya soka la Hispania na timu yake pia.
Katika mchezo wa juzi Jumapili Ronaldo alihitimisha ushindi wao kwa kufunga goli la pili na kumfanya kufikisha jumla ya magoli 290.
Ronaldo ambaye pia mshindi wa tuzo ya Ballon d’Or  ya mchezaji bora wa kiume wa mpira wa miguu kwa mara ya tatu ameshika nafasi hiyo akiwa amecheza michezo 289 huku nafasi ya pili ikishikwa na Alfredo Di Stefano ambaye alicheza michezo 392 na kuwa na magoli 307 huku nafasi ya kwanza ikishikwa na Raul Gonzalez mwenye magoli 323 katika michezo 741.

MANDAWA, MSUVA WAMBANA MBAVU KAVUMBAGU

Rashid Mandawa anamfukuzia kwa mabao Didier Kavumbangu
Na Princess Asia, DAR ES SALAAM
MBIO za kuwania kiatu cha dhahabu cha ufungaji bora wa Ligi Kuu Tanzania Bara, zimezidi kunoga ambapo kwa sasa Rashid Mandawa wa Kagera Sugar na Simon Msuva wa Yanga wanamfukuza kwa kasi ya ajabu Didier Kavumbagu anayeongoza mbio hizo.
Kavumbagu hadi sasa ameshafunga mabao nane, wakati Mandawa na Msuva kila mmoja amecheka na nyavu mara saba, hivyo kuonekana kuwa katika nafasi nzuri ya kumpiku Mrundi huyo.
Kwa misimu miwili iliyopita, tuzo hiyo imekuwa ikichukuliwa na wachezaji wa kigeni, Kavumbagu akitaka kuendeleza wimbi hilo msimu huu.
Msimu wa 2012/13, tuzo hiyo ilichukuliwa na Muivory Coast Kipre Tchetche aliyeipora kutoka kwa mzawa John Bocco na msimu uliofuata, 2013/14, Amissi Tambwe wakati huo akiwa Simba (sasa Yanga), ndiye aliyeibuka kidedea.
Na kutokana na kasi ya Mandawa pamoja na Msuva, kuna uwezekano mkubwa wa kutwaa tuzo hiyo msimu huu, lakini iwapo Kavumbagu ambaye ameonekana kutokuwa na mzaha katika kucheak na nyavu, atateleza.
Akizungumza na BIN ZUBEIRY, Madawa alisema lengo lake kubwa ni kuhakikisha anasaidia timu yake hiyo kufanya vizuri katika ligi pamoja na kuibuka mfungaji bora.
“sitaki kusema mengi lengo langu ni kuhakikisha nasaidia timu yangu inafanya vizuri huku nikiwanyamazisha wale wanaopenda kuzungumza,” alisema.

YANGA SC YAMUACHA COUTINHO SAFARI YA BOTSWANA

Na Pince Akbarm DAR ES SALAAM
KIUNGO Andrey Coutinho raia wa Brazil hatakuwemo katika kikosi cha kikosi cha Yanga SC kinachoondoka kesho Dar es Salaam kwenda Botswana kwa ajili ya mchezo wa marudiano dhidi ya BDF XI.
Yanga SC wanatarajiwa kuwa wageni wa BDF Ijumaa wiki hii katika mchezo wa marudiano, Raundi ya Awali Kombe la Shirikisho la Soka Afrika (CAF) na Mbrazil huyo hayumo safarini kwa sababu ya majeruhi.
Yanga SC inatarajiwa kuondoka na msafara wa wachezaji 20 na viongozi saba mjini Gaborone, tayari kwa mchezo ambao tayari wanaongoza kwa mabao 2-0.
Andrey Coutinho hatakwenda Botswana kwa sababu ni majeruhi 

Maana yake, Yanga SC wanatakiwa japo kulazimisha sare ugenini ili kutinga Raundi ya Kwanza ya michuano hiyo.
Katibu wa Yanga Dk Jonas Tiboroha amesema kikosi chao kitaondoka na wachezaji wote waliopitishwa na kocha wao Hans Pluijm.
Tibohora ambaye pia kitaaluma  ni kocha amesema kikosi chao kitaondoka na Ndege ya Shirika la Kenya tayari kwa mchezo huo wa kombe la Shirikisho utakaopigwa Ijumaa nchini humo ambapo Yanga itarejea Jumapili baada ya mchezo huo.
Wachezaji wanaitarajiwa kuondoka kesho ni Ally Mustafa ‘Barthez,’ Deo Munish ‘Dida, Mbuyu Twite, Juma Abdul, Oscar Joshua, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondani, Rajab Zahir, Pato Ngonyani, Salum Telela, Dilunga, Haruna Niyonzima, Mrisho Ngasa, Simon Msuva,Amissi Tambwe, Kpah Sherman na Danny Mrwanda

KIPA WA MBEYA CITY AONDOLEWA KIKOSINI

bu

 ki

ALICHOSEMA KOCHA WA SIMBA BAADA YA KUFUNGWA NA STAND UNITED

Pamoja na kupoteza nafasi nyingi za kufunga, Kocha Mkuu wa Simba, Goran Kopunovic amesema kweli Ligi Kuu Bara ni ngumu.

Kopunovic amekubali hilo baada ya ile mechi waliyolala kwa bao 1-0 mjini Shinyanga dhidi ya wenyeji Stand United.


Ameiambia SALEHJEMBE kwamba kulikuwa na makosa mengi kwa mwamuzi, pia wachezaji wake kutotumia nafasi, lakini akasisitiza, ligi ni ngumu.

"Ukiangalia mechi utaona tulicheza vizuri tu, lakini kuna makosa kadhaa ya sisi kutotumia nafasi na hata mwamuzi hakuwa mzuri kwetu.

"Lakini bado naweza kusema ligi ni ngumu sana na ushindani uko juu. Kupoteza mechi hiyo na Stand, kweli imeniumiza.

"Najua hata wachezaji wameumia lakini ni suala la kuangalia mechi ipi inafuatia na nini cha kufanya," alisema Kopunovic.

KURASA ZA MWANZO NA ZA MWISHO ZA MAGAZETI YA MICHEZO LEO FEB 24,

.
.
.
.
.
.
.
.

MAMBO KUMI KUHUSU KOCHA WA MTIBWA SUGAR MECK MEXIME


Mkasi V
Salama Jabir.
Jina lake linafanana na aliyekuwa Kocha wa Timu ya Tafa TZ, Marcio Maximo, yeye anaitwa Mecky Mexime, amesikika kwenye show ya Mkasi, katika aliyoyaongea kuna haya kumi kutoka kwake, safari yake kwenye soka, uchawi na soka, shule…
Hivi ndivyo safari yake kwenye soka ilivyoanza; “Tangu shuleni nilikuwa madarasa ya chini lakini timu ya shule nilikuwa nacheza.. Nikapata bahati ya kwenda Mtibwa, nilikuta watu kibao wako kwenye majaribio, lakini nilivyofika jioni, asubuhi nimeenda ofisini wakasema huyu tunamfahamu haina haja ya majaribio.. Asubuhi yake nikasaini fomu nikapewa chenji kidogo tu, sio kama sasa hivi watu wanapewa mahela makubwa
Mkasi II
Kocha wa Timu ya Mtibwa, Mecky Mexime.
Safari yake ya soka ilianzia Mtibwa kama mchezaji na ikaishia Mtibwa kama kocha; “Viongozi wa Simba au Yanga tumekuja hivi tunaongea bwana tunakutaka.. lakini kati yenu watatu mmoja ananipigia simu, ‘Mecky tumekaa kwenye mazungumzo lakini mi’ naona wewe bora ubaki Mtibwa usije huku
Kingine ni hiki cha umuhimu wa Makocha kusomea mpira; “Kusoma ni muhimu zaidi kwa sababu unavyoenda kusoma unaambiwa mazoezi jinsi ya kufanya.. wachezaji afya zao.. muda wa kupumzika.. Kila hatua unayoenda na muda wa kupumzika either mrefu au mfupi..
Mkasi III
Salama, John, Muba na Mexime kwenye show ya Mkasi.
Nini kilimfanya amekuwa Kocha?; “Sikuwa na wazo la kuja kuwa mwalimu, Maximo  ndio alionipa kipindi kile nacheza timu ya taifa nilikuwa namsaidia mambo mengi sana, alionna kipaji changu akanishauri akaniambia hapa bado unacheza zikitokea kozi nenda hata mimi naweza nikakusapoti. Nilipostaafu timu ya taifa lakini nikawa nacheza Mtibwa kozi zikatoka nikawa naenda lakini huku bado nacheza
Ishu ya wachezaji wa TZ kuwa na majina ya wachezaji wa nje; “Haya majina mashabiki ndio wanatoa huwezi kukataa, wewe mwenyewe huwezi tu ukajipa tu kwa mfano Nadir Haroub Cannavaro..
Nafasi ya makocha wazawa kwenye timu za TZ; “Makocha sisi wazawa kwanza sisi wenyewe tu hatuaminiani, halafu angalia nani anaeleta Kocha, ana taaluma ile ya mpira au kwa sababu mtu ana helka zake basi analeta Kocha.. Jana tu nimesoma gazeti ‘Matola afukuzwa Simba’, Simba wamefanikiwa kwa sababu wana vijana wengi na yeye ndio ambaye amewakuza, tunaenda Mapinduzi ‘Mzungu’ kaja sijui mechi tatu za mwisho sijui.. wakachukua Ubingwa lakini timu alikuwa nayo Matola. Angalia Mbeya City ilifanya vibaya watu wakaleta kelele lakini angalia sasa hivi Mbeya City iko wapi..
Mkasi I
Imani za kishirikina na soka; “Mi’ sizani Mtanzania atokeze hapa hana imani hizo.. zipo watu hela wanaliwa kutokana tu na imani..
Ana hiki cha kusema kuhusu mpira wa TZ; “Inatakiwa tuimarishe ligi yetu, tuhakikishe wachezaji wanaperform kwenye ligi yetu Tanzania na isiwe ligi ya magumashi.. akina Samatta wanatakiwa wawe wengi hapo tunaweza tukapiga hatua
Anauchukuliaje utendaji wa viongozi TFF; “Uongozi unajitahidi, siwezi kuzungumzia sana kwa sababu siko huko.. Mimi nimechezea timu ya Taifa zamani ilikuwa ina shida sana tunakaa Salvation army, mchezaji umelala juu wanapita wadudu wale nguchiro
Mkasi IV
Hapa anataja kikosi ambacho anatamani angecheza nacho timu moja; “Namba moja anakaa Mwameja, mbili Kassim Issa.. tatu Alphonse Modest.. nne na tano walikuwepo akina George Masatu, Boniface Pawasa, Waziri Mahazi, Suleiman Matola.. sita Hussein Masha.. saba Steven Mapunda, nane Salvatory Edward, tisa Monja Liseki, (10) Amir Maftah, (11) Edibili Lunyami