SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Mar 7, 2016

AZAM KUIFUATA BIDVEST SAUZI

NA Haji balou
Azam FC inatarajia kuondoka nchini
Jumatano ya keshokutwa kuelekea Afrika Kusini ‘Sauz’ kupambana na Bidvest Wits lakini kocha wa timu hiyo, Muingereza, Stewart Hall ametamba kuwa anaondoka akiwa ameshanasa siri nyingi za kiufundi
za wapinzani wake hao.

Pamoja na hayo, Stewart amesema kuwa anafahamu ubora wa timu hiyo inayoshikilia nafasi ya pili kwa sasa katika Ligi Kuu ya Sauz lakini amegundua silaha pekee ya kuwapunguza nguvu na pengine
kuwashinda kabisa ni kupata mabao ya ugenini kabla ya mchezo wao wa hapa nyumbani.

Azam itavaana na Wits Jumamosi hii huko Sauz katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika kabla ya mchezo wa marudiano utakaopigwa wiki mbili baadaye nchini Tanzania.

“Tutakwenda kule nikiwa tayari
nimeshaisoma Wits, nafahamu ni timu nzuri ikiwa ndani ya moja ya ligi bora za Afrika lakini nimefanikiwa kuona DVD zao tano pamoja na kutuma mtu akawaangalie kwenye mechi zao za ligi hivi karibuni,
kwa hiyo nimeshawasoma vizuri tu,”
alisema Stewart.