SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Apr 9, 2015

JUMA KASEJA HUYOOO SHINYANGA

Na Alex Sanga, SHINYANGA
STAND United ya Shinyanga inainyatia saini ya kipa wa zamani wa kimataifa wa Tanzania, Juma Kaseja, imeelezwa.
Mkurugenzi wa benchi La Ufundi wa Stand United, Muhibu Kanu ameiambia BIN ZUBEIRY jana kwamba, wana mipango ya kumsajili kipa huyo wa zamani wa Simba na Yanga, Juma Kaseja kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
“Kaseja ni kipa mzuri, mzoefu ambaye tunaamini bado ana uwezo mkubwa na atatusaidia tukiwa naye,”amesema.
Kwa sasa, Juma K Juma ni mchezaji huru baada ya kujiondoa katika klabu yake, Yanga SC akiishutumu kukiuka vipengele vya Mkataba baina yao. Hata hivyo, Yanga SC imemfungulia kesi Kaseja ambayo inaendelea Mahakama ya Kazi. 

Kwa upande wake, kocha wa Stand United, Mganda Mathias Lure amesema kwamba ushindi wa 1-0 dhidi ya Mtibwa Sugar Jumapili umeamsha morali ya wachezaji wake na sasa watapambana zaidi wasishuke.
"Mechi yetu ijayo itakuwa siku ya Jumapili na tunacheza na Polisi Morogoro, kisha tunabakiza mechi sita, dhidi ya Ruvu Shooting, JKT Ruvu
tukiwa nyumbani na ugenini tutacheza na Azam, Yanga na Coastal Union,”amesema Luren ambaye timu yake ipo katika nafasi ya 11 kwenye msimamo wa ligi ikiwa na pointi 24.

HANS POPPE: KESSY HAJITAMBUI WALA HAJIJUI

Na Princess Asia, DAR ES SALAAM
MWENYEKITI wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe amesema kwamba beki Hassan Ramadhani Kessy hajatumia busara kususa wakati anaidai klabu hiyo Sh. Milioni 5, baada ya kulipwa Sh. Milioni 15 za usajili wake.
Akizungumza na BIN ZUBEIRY leo Dar es Salaam, Poppe amesema kwamba walimsajili Kessy kwa dau la Sh. Milioni 20 Desemba mwaka jana na wakampa Sh. Milioni 15, wakiahidi kummalizia Milioni 5 baadaye.
Hata hivyo, Poppe amesema ni jambo la ajabu hata mwaka mmoja kati ya miaka miwili ya Mkataba wake haujamalizika, mchezaji huyo anagoma.
Amegoma; Hassan Kessy amejitoa kikosini Simba SC kwa sababu hajamaliziwa fedha za usajili na hajapatiwa nyumba ya kuishi
Amekoma naye; Zacharia Hans Poppe (kushoto) amesema hana hamu na mchezaji huyo chipukizi

“Huu ndiyo utaratibu wetu. Wachezaji wote tunaowasajili huwa hatuwapi malipo yote, mara nyingi tunawapa nusu, tunawamalizia baadaye. Tena yeye alikuwa ana bahati kupewa zaidi ya nusu,”.
“Na kuna wenzake wanadai fedha nyingi kuliko yeye, lakini hawajagoma. Kwa kweli huyu mchezaji si mfano bora na mimi amenikera sana. sina hamu naye,”amesema Poppe.
Aidha, Kapteni huyo wa zamani wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), amesema kwamba mshahara ambao Kessy anapata hivi sasa Simba SC ni zaidi ya mishahara sita aliyokuwa analipwa Mtibwa Sugar, lakini inashangaza bado anagoma.
“Kasajiliwa Desemba, kapewa Milioni 15 kati ya 20, kufika Machi anagoma, huyu mchezaji mzima kweli?”amehoji Poppe.
Hata hivyo, Poppe amesistiza suala la mchezaji huyo litapelekwa Kamati ya Nidhamu ya klabu na atachukuliwa hatua kwa sababu sheria ziko wazi.
Alipoulizwa kuhusu kutopatiwa nyumba, Poppe alijibu; “Klabu iliahidi kumpatia makazi, na hadi sasa bado tunahangaika kumtafutia makazi. Suala si makazi tu. Ni makazi bora na eneo salama. Sasa papara zake alitaka tumpeleke akaishi Tandale? Maana huko vyumba vinapatikana hata saa nane usiku,”. 
“Na kwa kawaida mchezaji anaposajiliwa Simba kabla ya kupatiwa nyumba, huwa anaishi hoteli na analipiwa na klabu. Huyu mtu ana matatizo tu yeye mwenyewe, asitake kuwachafua watu hapa,”amesema.  
Mbaya zaidi, Poppe amesema mchezaji huyo badala ya kupeleka malalamiko kwa uongozi, akakimbilia kwenye magazeti. “Ina maana lengo lake aipake matope klabu, basi kafanakikiwa,”amesema Poppe.

KURASA ZA MWANZO NA ZA MWISHO ZA MAGAZETI YA MICHEZO LEO APRIL 9, 2015

DSC01112
DSC01113
DSC01114
DSC01115
DSC01116
DSC01117

COUTINHO AIPELEKA LIVERPOOL NUSU FAINALI KOMBE LA FA


Philippe Coutinho akishangilia baada ya kufunga bao pekee zikiwa zimesalia dakika 20 mchezo kumalizika katika ushindi wa 1-0 wa Liverpool dhidi ya Blackburn Rovers Uwanja wa Ewood Park, mchezo wa marudiano wa Robo Fainali Kombe la FA. Mchezo wa kwanza timu hizo zilitoka sare ya bila kufungana Uwanja wa Anfield mwezi uliopita. Liverpool sasa itamenyana na Aston Villa katika Nusu Fainali Uwanja wa Wembley Jumapili ya Aprili 19.

SUAREZ APIGA MBILI, MESSI MOJA...BARCELONA YAUA 4-0 LA LIGA

Suarez leaps into Messi's arms after the pair's sensational opening strikes put the hosts in control
Mshambuliaji wa Barcelona, Luis Suarez akiwa amemrukia mchezaji mwenzake, Lionel Messi baada ya wawili hao wote kufunga mabao katika ushindi wa 4-0 kwenye mchezo wa La Liga dhidi ya Almeria Uwanja wa Camp Nou usiku huu. Messi alifunga moja, Suarez mawili na lingine Marc Bartra.

RONALDO AFUNGA BAO LA 300 REAL MADRID IKISHINDA 2-0 LA LIGA

Cristiano Ronaldo scored the 300th goal of his Real Madrid career to see off Rayo Vallecano and remain four points behind Barcelona

Cristiano Ronaldo akifunga bao lake la 300 katika mechi ya 288 tangu aanze kuchezea Real Madrid katika mchezo wa La Liga dhidi ya Rayo Vallecano usiku huu Uwanja wa Teresa Rivero. Bao lingine la Real lilifungwa na James Rodriguez.
Ronaldo turns to his trademark celebration after scoring the 300th goal of his Real Madrid career
Ronaldo akishangilia bao lake la 300 pamoja na Gareth Bale