SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Dec 29, 2015

ALICHOSEMA AVEVA KUHUSU SIMBA KUJENGA UWANJA

 
Uongozi wa Simba umesema utaanza rasmi kujenga uwanja wao wa mazoezi mwezi ujao.

Rais wa Simba, Evans Aveva amesema watautumia uwanja wao wanaoumiliki kuanza kujenga uwanja wa mazoezi.

“Tutaanza kujenga uwanja kwa ajili ya mazoezi kwa ajili ya kupunguza gharama, kwa siku tunalazimika kulipa hadi laki tatu na nusu kwa mazoezi ya mara moja.
“Kulikuwa kuna mambo ya kupata hati ya umiliki, wakati tunaingia kulikuwa na deni kama la shilingi milioni kumi na mbili hivi,” alisema Aveva.


Uwanja huo ulio katika eneo la Bunju jijini Dar es Salaam, ulinunuliwa na uongozi chini ya Hassan Dalali aliyekuwa mwenyekiti wakati huo

ALICHOSEMA PLUIJM BAADA YA KUFUKUZWA KWA NIYOZIMA


KOCHA Mkuu wa Yanga SC, Mholanzi Hans van der Pluijm amesema kwamba amekwishamuondoa kiungo Haruna Hakizimana Fadhil Niyonzima katika mipango yake na sasa anasonga mbele bila yeye.
Akizungumza na BIN ZUBEIRY SPORTS – ONLINE leo mjini Dar es Salaam, Pluijm amesema kwamba anaunga mkono hatua iliyochukuliwa na uongozi, kwa sababu Haruna ameshindwa kujiheshimu kama mchezaji wa kulipwa.
Pluijm amesema kwamba sasa anakiandaa kikosi chake kwa ajili ya michuano ya Kombe la Mapinduzi na amekwishamfuta Haruna katika daftari lake la wachezaji.
Yanga SC jana imevunja Mkataba na kiungo huyo wa kimataifa wa Rwanda kwa madai ya mchezaji huyo wa Amavubi kukiuka vipengele.
Haruna Niyonzima alikuwa kipenzi cha Pluijm kabla ya matatizo haya

Na Pluijm anakuwa mtu mwingine muhimu ndani ya Yanga SC kuunga mkono adhabu hiyo, baada ya Milionea Abdallah Ahmed Bin Kleb aliyemleta Niyonzima Jangwani.
 “Mimi kwa kweli ninaunga mkono uamuzi uliochukuliwa na uongozi, kwa sababu suala la nidhamu ni la muhimu mno katika timu. Kama mchezaji ameshindwa kuheshimu Mkataba wake, hii ni hatua sahihi,”alisema Bin Kleb jioni ya jana.
Aidha, Bin Kleb ambaye alisajili nyota wengine kadhaa Yanga SC akiwemo kiraka Mbuyu Twite, amewataka wapenzi na wanachama wa klabu kuunga mkono uamuzi wa uongozi.
“Unajua Haruna ni mchezaji mwenye kipaji, ambaye ana wapenzi wengi pale Yanga SC, ambao najua hawataufurahia uamuzi huu. Lakini mimi napenda nichukue fursa hii kuwaomba wana Yanga wote tuungane na uongozi kuafiki hatua hii,”.
“Mchezaji kama ameshindwa kuheshimu thamani aliyopewa ndani ya klabu, wazi huyo hafai. Haruna tulimchukua kwa Mkataba wa miaka miwili awali, baadaye tukamuongeza miwili. Ikaisha na juzi ametoka kuongezewa mwingine wa miaka miwili,”. 
“Sasa nadhani amekwishajiona mwenyeji kwenye timu anafanya anavyotaka bila kuzingatia Mkataba wake unasemaje. Ni sahihi tu hatua iliyochukuliwa,”amesema Kleb.
Aidha, Bin Kleb alisema anaamini hatua iliyochukuliwa itakuwa fundisho kwa wachezaji wengine, ili waweze kuheshimu mikataba yao wakati wote.
Sakata la kufukuzwa kwa Niyonzima Yanga SC, linaanzia mwezi uliopita baada ya mchezaji huyo kuruhusiwa kwenda kuichezea Rwanda katika Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki, CECAFA Challenge nchini Ethiopia na akachelewa kurejea baada ya mashindano.
Kufuatia hali hiyo, klabu ilimsimamisha kwa muda usiojulikana Niyonzima kabla ya suala lake kupelekwa Kamati ya Nidhamu, ambayo hatimaye imekuja na maamuzi magumu.
Pamoja na Niyonzima kuwasilisha vielelezo vyote vya kumsafisha, lakini uchunguzi wa Kamati ya Nidhamu ulijiaminisha kiungo huyo amedanganya ili kukwepa hatua za kinidhamu.  
Ulibaini plasta gumu (PoP) alilofunga baada ya kurejea akiwa amechelewa ilikuwa ni ‘geresha’ na vielelezo vingine alivyowasilisha vilikuwa ‘feki’ pia.
Na ikamnasa kwenye picha za video siku za karibuni ‘akijirusha’ sehemu mbalimbali za starehe ikiwemo kwenye onyesho la mwanamuziki Ali Kiba.
Haruna aliyezaliwa Februari 5, mwaka 1990 Gisenyi nchini Rwanda, alijiunga na Yanga SC mwaka 2011 akitokea APR ya kwao, ambako aliwasili mwaka 2007 akitokea Rayon aliyoichezea kwa misimu miwili baada ya kujiunga nayo akitokea Etincelles iliyomuibua mwaka 2005.

Dec 28, 2015

AVEVA AFUNGUKA SUALA LA KUIBINAFSISHA SIMBA

Image result for RAISI AVEVA SIMBA

Rais wa Simba, Evans Aveva amesema suala la kuibinafsisha klabu hiyo linahitaji ungalifu mkubwa katika mambo kadhaa.

Aveva amesema kuwa Simba inaweza kubinafsishwa lakini lazima uongozi uhakikishe na kujua thamani ya klabu  hiyo ikiwa imeishajiridhisha kama ubinafsishaji kweli una faida.

“Ni suala la kitaalamu, lazima kuliangalia na kutathmini. Kama tutapata uhakika basi ni suala la thamani ya klabu ya Simba. Hapa si kuangalia majengo, sijui magari na uwanja ambao tunataka tuanze kuujenga.

“Lakini kuna suala la maana ya thamani ya Simba kama klabu, hili linahitaji wataalamu waliotulia na kufanya tathmini ya uhakika. Baada ya hapo, litafuatia suala la wanachama kuelimishwa kuwa nini kinafanyika, zipi faida zake.

“Wanachama ndiyo wamiliki wa klabu, lazima waelimishwe na baada ya hapo kuna suala la katiba ambayo inasema wamiliki wa Simba ni wanachama. Ukiangalia hapa utaona hili si jambo dogo,” alisema Aveva.

Mfanyabiashara maarufu nchini, Mohammed Dewji maarufu kama Mo alikuwa ameeleza wazi nia yake ya kutaka kuinunua Simba kwa asilimia 51 na zilizobaki 49 zitaachwa kwa wanachama wengine wa Simba. Lakini uongozi wa Simba umekuwa ukisema unalisikia suala hilo kwenye vyombo vya habari tu.

BAADA YA MECHI ZA LEO JUMATATU MSIMAMO LIGI KUU ENGLAND UPO HIVI


HUU NDIO MSIMAMO WA LIGI KUU TANZANIA



Rnk
TeamMPWDLGFGA+/-Pts

1
Young Africans1310303052533

2
Azam1210202681832

3
Simba SC127321991024

4
Mtibwa Sugar11731147724

5
Mwadui136431612422

6
Stand United137151411322

7
Tanzania Prisons136341314-121

8
Toto African134541215-317

9
Mgambo JKT12345710-313

10
JKT Ruvu133371520-512

11
Mbeya City132561115-411

12
Majimaji13328823-1511

13
Ndanda12165914-59

14
Coastal Union13166614-89

15
Kagera Sugar13238416-129

16
African Sports132110314-117

WEGER AANZA KUMFUKUZIA CHICHARITO


Kocha Arsene Wenger wa Arsenal sasa anataka kuimarisha safe take ya ushambuliaji.

Wenger anataka kumsajili mshambuliaji nyota wa zamani wa Manchester United, Javier Harnandez maarufu kama Chicharito.

Chicharito sass anakipiga katika klabu ya Bayer Leverkusen ya Ujerumani na amekuwa aking’ara katika Bundesliga.

Raia huyo wa Mexico, Chicharito ,27, alijiunga na klabu hiyo ya Ujerumani kwa ada ya pauni million 7 na tayari ametupia mabao 19 katika me chi 21 alizoichezea timu take msimu huu.

Kwa sass safe ya ushambuliaji ya Arsenal in a mshambuliaji mmoja tu wa kati ambaye ni Olvier Giroud aria wa Uafaransa huku wengine kama Danny Welbeck wakiwa majeruhi.


Hata hivyo, Wenger anaangalia upande mwingine kama ataweza kumpata bila ada, mshambuliaji nyota wa Leicester City, Riyad Mahrez raia wa Algeria ambaye hata hivyo tayari anatupiwa macho na klabu kibao zikiwemo Man United na Tottenham.

ALICHOSEMEA ABDALLAH BIN KLEB KUHUSU KUFUKUZWA KWA NIYONZIMA

MILIONEA Abdallah Ahmed Bin Kleb aliyemleta kiungo Haruna Hakizimana Fadhil Niyonzima Yanga SC, ameunga mkono uamuzi wa kufukuzwa kwa mchezaji huyo.
Yanga SC leo imevunja Mkataba na kiungo huyo wa kimataifa wa Rwanda kwa madai ya mchezaji huyo wa Amavubi kukiuka vipengele.
“Mimi kwa kweli ninaunga mkono uamuzi uliochukuliwa na uongozi, kwa sababu suala la nidhamu ni la muhimu mno katika timu. Kama mchezaji ameshindwa kuheshimu Mkataba wake, hii ni hatua sahihi,”amesema Bin Kleb akizungumza na BIN ZUBEIRY SPORTS – ONLINE jioni ya leo.
Abdallah Bin Kleb (kushoto) akimkabidhi jezi namba nane Haruna Niyonzima baada ya kukamilisha usajili wake kwa mara ya kwanza mwaka 2011 mjini Kigali, Rwanda

Aidha, Bin Kleb ambaye alisajili nyota wengine kadhaa Yanga SC akiwemo kiraka Mbuyu Twite, amewataka wapenzi na wanachama wa klabu kuunga mkono uamuzi wa uongozi.
“Unajua Haruna ni mchezaji mwenye kipaji, ambaye ana wapenzi wengi pale Yanga SC, ambao najua hawataufurahia uamuzi huu. Lakini mimi napenda nichukue fursa hii kuwaomba wana Yanga wote tuungane na uongozi kuafiki hatua hii,”.
“Mchezaji kama ameshindwa kuheshimu thamani aliyopewa ndani ya klabu, wazi huyo hafai. Haruna tulimchukua kwa Mkataba wa miaka miwili awali, baadaye tukamuongeza miwili. Ikaisha na juzi ametoka kuongezewa mwingine wa miaka miwili,”. 
“Sasa nadhani amekwishajiona mwenyeji kwenye timu anafanya anavyotaka bila kuzingatia Mkataba wake unasemaje. Ni sahihi tu hatua iliyochukuliwa,”amesema Kleb.
Aidha, Bin Kleb amesema anaamini hatua iliyochukuliwa itakuwa fundisho kwa wachezaji wengine, ili waweze kuheshimu mikataba yao wakati wote.
Sakata la kufukuzwa kwa Niyonzima Yanga SC, linaanzia mwezi uliopita baada ya mchezaji huyo kuruhusiwa kwenda kuichezea Rwanda katika Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki, CECAFA Challenge nchini Ethiopia na akachelewa kurejea baada ya mashindano.
Kufuatia hali hiyo, klabu ilimsimamisha kwa muda usiojulikana Niyonzima kabla ya suala lake kupelekwa Kamati ya Nidhamu, ambayo hatimaye imekuja na maamuzi magumu.
Pamoja na Niyonzima kuwasilisha vielelezo vyote vya kumsafisha, lakini uchunguzi wa Kamati ya Nidhamu ulijiaminisha kiungo huyo amedanganya ili kukwepa hatua za kinidhamu.  Image result for NIYONZIMA
Haruna ni mchezaji kipenzi cha mashabiki Yanga SC kama anavyoonekana hapa akitunzwa fedha baada ya mechi
Ulibaini plasta gumu (PoP) alilofunga baada ya kurejea akiwa amechelewa ilikuwa ni ‘geresha’ na vielelezo vingine alivyowasilisha vilikuwa ‘feki’ pia.
Na ikamnasa kwenye picha za video siku za karibuni ‘akijirusha’ sehemu mbalimbali za starehe ikiwemo kwenye onyesho la mwanamuziki Ali Kiba.
Haruna aliyezaliwa Februari 5, mwaka 1990 Gisenyi nchini Rwanda, alijiunga na Yanga SC mwaka 2011 akitokea APR ya kwao, ambako aliwasili mwaka 2007 akitokea Rayon aliyoichezea kwa misimu miwili baada ya kujiunga nayo akitokea Etincelles iliyomuibua mwaka 2005.

SIMBA KUCHEZA NA URA YANGA NA AZAM FC MAPINDUZI CUP

 Image result for timu ya simba
Mabingwa watetezi, Simba SC wamepangwa Kundi A pamoja na URA, Jamhuri na JKU Na Ali Bakari, ZANZIBAR
MABINGWA watetezi, Simba SC wamepangwa Kundi A katika Kombe la Mapinduzi 2016 pamoja na URA ya Uganda, Jamhuri ya Pemba na JKU ya Unguja.
Katika ratiba iliyotolewa leo na Chama cha Soka Zanzibar (ZFA), mabingwa wa Bara, Yanga SC wamepangwa kundi moja, B pamoja na mabingwa wa Afrika Mashariki na Kati, Azam FC, Mtibwa Sugar ya Morogoro na Mafunzo ya Zanzibar.
Simba SC itafungua dimba na Jamhuri Januari 2, 2016 mchezo ambao utatanguliwa na mechi kati ya JKU na URA Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Yanga SC watashuka dimbani siku inayofuata, Januari 3, 2016 kumenyana na Mafunzo, mchezo ambao utatanguliwa na mechi kati ya Mtibwa Sugar na Azam FC.
Nusu Fainali zinatarajiwa kuchezwa Januari 9, wakati Fainali itachezwa Januari 13, Uwanja wa Amaan katika kilele cha sherehe za Mapinduzi.

Oct 16, 2015

BRENDAN RODGERS APATA KAZI MPYA BAADA YA KUFUKUZWA LIVERPOOL

rod
Ukishafanya kazi ya kuiongoza taasisi kubwa kama Liverpool mambo yako hayawezi kuwa mabaya hata kama umeachishwa kazi. Hivyo ndivyo imemtokea Brendan Rodgers ambae siku kadhaa zilizopita alifukuzwa kazi na club ya Liverpool na sasa hivi taarifa zimetoka kwamba ameshapata kazi mpya.
Kazi ya ukocha kwa sasa sio rahisi kwasababu club zote ndio kwanza zimeanza ligi na makocha wao. Kazi aliyopata Brendan Rodgers ni ya kuwa mchambuzi kwenye TV ya beIN Sports ya huko Qatar.
Rodgers anategemewa kuwa mmoja kati ya wachangiaji wa mechi za EPL ambazo zinaonyeshwa na channel hiyo aki ripoti kutoka kwenye studio zao huko Qatar. Mambo sio mabaya kwa Rodgers kwasababu warabu huwa hawana tabu kwenye swala la kuweka mzigo mzito kwa ajili ya watu wanaofanya kazi zao.

SIMBA SC WAILAUMU TFF WAMEJAA NA UYANGA

Na Princess Asia, DAR ES SALAAM
KLABU ya Simba SC imelalamika kwamba, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) haliwatendei haki kwa sababu uongozi wake umesheheni watu wa Yanga SC.
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe ameiambia BIN ZUBEIRY SPORTS- ONLINE leo kwamba, imefikia TFF wamekata kabisa mawasiliano na klabu yao.
Poppe amesema kwamba TFF sasa hawajibu hata barua za Simba SC wanapoandika kuhoji au kuomba ufafanuzi wa jambo lolote.
Kapteni huyo wa zamani wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) amesema kwamba imefikia wakati wanashindwa hata kujua namna gani wanaweza kupata haki zao nyingine za msingi, kutokana na ‘kuchuniwa’ na TFF.
Hans Poppe amesema TFF haiwatendeo haki kwa sababu viongozi wengi ni Yanga SC 

“Inafahamika kwamba Rais wa TFF (Jamal Malinzi), Katibu wake (Mwesigwa Selestine) wote ni Makatibu wa zamani wa mahasimu wetu, Yanga SC. Na bado wapo wengine wengi pale TFF ambao wametoka Yanga akina Baraka Kizuguto.
“Lakini kwa sababu wanaongoza chombo cha kitaifa, wanapaswa kutenda haki, yaani inaonekana kabisa TFF wanaikandamiza Simba na wanaibebea Yanga,”amelalamika Poppe.
Akifafanua, mfanyabiashara huyo maarufu nchini, amesema TFF hawajajibu barua yoyote ya Simba SC kwa mwaka huu na hawaelewei sababu ni nini.
“Watuonyeshe wao, ni barya ipi ya Simba SC wamejibu mwaka huu, malalamiko yetu ya mchezo dhidi Yanga hawakujibu, Suala la Messi (Ramadhani Singano) hawakujibu. Hata tunapojibu barua zao za adhabu wanazotuandika ili kuomba ufafanuzi, pia hawatujibu. 
“Labda watuambie basi kwamba barua zetu tunatakiwa kuzipitishia Yanga SC ndiyo watujibu, tutafanya hivyo, tutaandika na kuwapelekea Yanga waweke muhuri wao ipelekwe TFF, tujibiwe, hiyo ndiyo shida yetu,”amesema.
Hans Poppe amesema kwamba mchezaji wao Ramadhani Singano ‘Messi’ amehamishiwa Azam FC kinyume cha utaratibu na kila wapodai haki yao hawasikilizwi. “Mchezaji wa Yanga (Donald Ngoma) alimpiga kichwa mchezaji wetu (Hassan Kessy) na tukapeleka ushahidi wa picha za video, hakuchukuliwa hatua na wala hatukujibiwa,”. 
“Lakini Juma Nyosso (wa Mbeya City) alimdhalilisha John Bocco (wa Azam FC) akachukuliwa hatua baada ya saa 24 kwa ushahidi wa picha,”amesema.
Aidha, amesema kwamba Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), limeiamuru klabu ya Etoile du Sahel ya Tunisia iilipe Simba SC dola 300,000 za Kimarekani za manunuzi ya mshmbauliaji Emmanuel Okwi, lakini wanashindwa kufuatulia kwa sababu TFF haiwasikilizi tena.
“Kwa kweli tupo wakati mgumu mno, tunashindwa hata kuelewa tunacheza hii ligi kwa sababu gani, inaonekana tunawasindikiza watu ambao tayairi wameandaliwa kwa namna yoyote wawe mabingwa,”amesema

NIYONZIMA HATARINI KUIKOSA AZAM KESHO



Haruna Niyonzima akiwa na mkewe leo Kigali, Rwanda baada ya kufunga ndoa ya Kiserikali 
Na Prince Akbar, DAR ES SALAAM
UWEZEKANO wa kiungo Haruna Hakizimana Niyonzima kuichezea klabu yake, Yanga SC Jumamosi Dar es Salaam dhidi ya Azam FC ni mdogo.
Nahodha huyo wa Rwanda, amefunga ndoa na mkewe leo Kigali, baada ya kurejea kutoka Morocco kuichezea timu yake ya taifa.
Katibu wa Yanga SC, Dk. Jonas Tiboroha ameithibitishia BIN ZUBEIRY SPORTS- ONLINE usiku huu kwamba, Niyonzima bado hajawasili.
“Niyonzima hajawasili, nadhani anaweza kuja kesho, kwa sababu walikuwa Morocco na timu yao ya taifa,”amesema Dk. Tiboroha.
Katibu huyo wa Yanga SC amesema mshambuliaji Mrundi, Amissi Tambwe amewasili tangu juzi na leo amefanya mazoezi na wenzake Uwanja wa Boko Veterani, Dar es Salaam.
Yanga SC imeweka kambi hoteli ya Kiromo, Bagamoyo mkoani Pwani na inafanya mazoezi, uwanja wa Boko Veterani nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam kujiandaa na mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Azam FC Jumamosi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. 
Aidha, kiungo Mnyarwanda wa Azam FC, Jean Baptiste Mugiraneza naye pia hajarejea Dar es Salaam, hivyo yuko hatarini kuikosa mechi hiyo ya kukata na shoka.
Niyonzima akiwatoka wachezaji wa Azam FC, Erasto Nyoni (kulia) na Khamis Mcha (kushoto) katika moja ya mechi zilizopita kuzikutanisha timu hizo

BOBAN ATAMBA SIMBA ITAFIA SOKOINE KESHO


Na Mwandishi Wetu, Mbeya
Mbeya City inatarajiwa kuikaribisha Simba, kesho Jumamosi katika Ligi Kuu Bara lakini ujio wa kiungo Haruna Moshi ‘Boban’ umeongeza nguvu kwenye kikosi cha Mbeya City ambapo amesema anaamini timu yake itaibuka na ushindi.


Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mazoezi ya timu
 yake hiyo, jana kwenye Uwanja wa Sokoine, Boban alisema kwa 
jinsi alivyowaona wenzake katika muda mfupi, anaamini
 ushindi utapatikana.

“Hii imekuwa siku nzuri kwangu, nimegundua timu yetu ina
 kikosi bora, vijana wana vipaji na uwezo mkubwa wa kucheza
 soka, binafsi hili limenishangaza na kunipa imani kuwa Simba
 hawana nafasi kwetu Jumamosi, tutawafunga,” alisema Boban.

Wakati huohuo, mchezo huo wa Ligi Kuu Bara utakaochezwa 
kwenye Uwanja wa Sokoine, umesababisha kuwe na gumzo
 kubwa mkoani hapa, ambapo umekuwa ukizungumzwa katika
 vijiwe vingi vya soka.

Kutokana na hali hiyo, ulinzi ulikuwa mkali katika mazoezi ya Mbeya City ambayo ipo chini ya Kocha Meja Abdul Mingange.

Jul 29, 2015

KAZIMOTO ALITAKAA KWENDA MISRI AKAAMUA KURUDI SIMBA


KAZIMOTO AKIWA QATAR...
Kiungo Mwinyi Kazimoto amejiunga tena na Simba akitokea Al Markhiya ya Qatar.


Mwinyi amerejea Simba baada ya kujiunga na Al Markhiya akitokea Msimbazi. 

Ameichezea timu hiyo ya daraja la pilim misimu miwili, lakini ikashindwa kupanda daraja.
AKISAINI KUREJEA SIMBA.

Kutokana na hali hiyo, uongozi wa Al Markhiya ukaamua kubadili asilimia kubwa ya wachezaji ilionao ili kuleta mabadiliko iweze kupanda daraja. Fagio likamkumba Kazimoto, lakini alikuwa na bahati.

Kwani wakati mabadiliko yanafanyika, yeye tayari alikuwa amepata ofa ya kujiunga na Petrojet inayoshiriki Ligi Kuu Misri.
HANS POPPE AKIPOKEA MKWANJA WA KUMUUZA KAZIMOTO NCHINI QATAR.

Licha ya juhudi za kutaka kiungo huyo ajiunge na Petrojet, yeye alisisitiza anataka kurejea nyumbani na mwisho, amejiunga na Simba!

"Ni kweli tumefanya juhudi kumshawishi kwamba Petrojet ingekuwa changamoto nzuri kwake. Lakini alikataa katakata na akasisitiza anataka kurejea nyumbani, hatukuwa na ujanja.

"Kibaya kwa wachezaji wa Tanzania, wengi wanataka kubaki Tanzania, ni waoga wa changamoto," kilieleza chanzo cha uhakika kutoka ndani ya al Markhiya huko Qatar.

Jul 25, 2015

SIKIA CANNAVARO ALIVYOWAAMBIA SIMBA KAMA WATAMSAJILI MICHAEL OLUNGA

OLUNGA (KULIA) AKISHANGILIA NA WENZAKE WA GOR MAHIA...
Simba inapambana muda wote kuhakikisha inamsajili straika Michael Olunga wa Gor Mahia, lakini nahodha wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ ni kama anataka kutibua dili hilo aliposema; “Huyo Olunga hana lolote, isipokuwa ana bahati tu.”


Cannavaro alienda mbali kwa kusema, siku Yanga ilipocheza na Gor Mahia ni kweli Olunga aliwasumbua na kufanikiwa kufunga bao moja katika ushindi wa mabao 2-1 walioupata, lakini hana uwezo wa kusumbua katika ligi.
CANNAVARO
Cannavaro amesema: “Ujue siku ile tulipocheza na Gor Mahia, Olunga alikuwa na bahati na kweli alitusumbua lakini sidhani kama ana uwezo mkubwa kiasi cha kututisha.”

“Kwa kweli alibahatisha tu, nasikia Simba wanataka kumsajili. Waache wamsajili halafu tukutane naye katika ligi (Ligi Kuu Bara) ndipo watakapoona kama wanamsajili mchezaji wa kawaida tu.”


Cannavaro alisema anatamani wakutane tena na Gor Mahia katika mechi zijazo za Kombe la Kagame ili kuthibitisha kauli yake na kuwahakikishia Simba kwamba wanataka kusajili mchezaji wa kawaida.

Jul 16, 2015

KIBURI CHAMUONDOA VALDEZ MAN UNITED

Victor-Valdes-training
Hatimaye kocha wa Manchester United, Louis Van Gaal amefumbua kile kilichokua kimejificha baada ya kushuhudia golikipa Victor Valdez akiachwa katika safari ya ‘Pre-season’ nchini Marekani.

Akiongea kwa mara ya kwanza na vyombo vya habari katika ‘tour’ hiyo ya nchini Marekani, pamoja na mambo mengine, Van Gaal alithibitisha kuwa klabu inajiandaa kumuuza mchezaji huyo wa zamani wa Barcelona.

Van Gaal akatoboa kwamba, Valdez aligoma kucheza katika mechi za U21 ikiwa ni utaratibu wa kujijenga kurudi katika fomu yako ya kawaida.

Van Gaal amesema, Valdez alienda kinyume na aliichoita ‘philosophy’ yake. Van Gaal huwamuru wachezaji kujiunga na timu ya vijana ya U21 katika hali ya kuwafanya warudishe fitness zao, lakini Valdez alikataa imefahamika.

Pamoja na sintofahamu ya golikipa David de Gea, lakini Van Gaal anasema hawawezi kumvumilia mchezaji kama Valdez na kumshangaa kwamba walimsaidia kurudi katika hali yake, ikiwa ni pamoja na kumpa mkataba lakini amekiuka masharti.

Alipoulizwa kuhusu mustakabali wa De Gea, kocha huyo alisema ni upuuzi kuuliza swali hilo kwani De Gea anaonesha ‘commitment’ na ueledi mkubwa kikosini hapo.

Kuhusu DiMaria, Van Gaal alisema, mchezaji huyo ni mali yao lakini akasisitiza kuwa soka ni mchezo usiotabirika na kwamba mashabiki wasubiri kuona hadi mwisho itakuwaje.

Aidha katika mkutano huo na waandishi wa habari, wachezaji wapya walitambulishwa huku wakiulizwa pia maswali na waandishi katika utaratibu wa kawaida kabisa wa media.

Kwingineko tetesi zinasema kuwa Manchester United inamuwinda golikipa Romero wa timu ya taifa ya Argentina huku Real Madrid nao wakiingilia dili hilo.

STEWART ASEMA MESSI,TCHETCHE, AME, WAWA WOTE ‘WAPO UNGA’

Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
NYOTA wa Azam FC, Serge Wawa Pascal Kipre, Miachel Balou, Kipre Herman Tchetche wote raia wa Ivory Coast pamoja wazalendo Ramadhani Singano ‘Messi’ na Ame Ali ‘Zungu’ wote hawako fiti.
Hayo yamesemwa na kocha Mkuu wa timu hiyo Muingereza, Stewart John Hall katika mahojiano na BIN ZUNBEIRY SPORTS- ONLINE jana jioni Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
Pamoja na hao, Stewart amesema wachezaji wawili pia waliokuja majaribio kipa Vincent Atchouailou de Paul Angban kutoka Ivory Coast na kiungo Ryan Burge kutoka England, pia hawako fiti.
Na wakati michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, Kombe la Kagame inaanza Jumamosi Dar es Salaam, Stewart amesema kwamba wachezaji wake kadhaa tegemeo hawako tayari. 
Hawako fiti; Kipre Tchetche (kulia) na Ramadhani Singano 'Messi' kushoto wakifanya mazoezi maalum baada ya kumaliza programu ya timu jana Uwanja wa Azam Complex, Chamazi

Stewart amevutiwa na Burge na amempa programu maalum ya kumuweka fiti pamoja na Wawa, Balou, Tchetche, Messi na Ame ambao wote wamekuwa wakifanya mazoezi ya ziada kabla na bada ya mazoezi ya timu kwa ujumla.
“Siku chache zimebaki kabla ya Kagame, lakini wachezaji wengi tegemeo katika kikosi cha kwanza hawako fiti. Messi, Kipre Tchetche, Balou, Ame, Serge Wawa na Ryan wote hawako fiti kwa sababu walichelewa kujiunga na wenzao kwa maandalizi ya mwanzo wa msimu,”amesema.
Hata hivyo, mtaalamu huyo amesema atafanya jitihada zinazowezekana kuhakikisha kwa siku chache zilizobaki wachezaji hao wanakuwa fiti angalau kwa asilimia 50.
Stewart Hall (katikati) akijadiliana na Meneja wa Azam FC, Luckson Kakolaki na kipa wa timu ya vijana, Metacha Boniphace
Kipre Michael Balou hayuko fiti
Serge Wawa Pascal pia hayuko fiti

“Napambana kupata angalau asilimia 50, kama wakizidi hapo itakuwa vizuri. Lakini lengo ni kufanya vizuri katika haya mashindano, ikibidi kuchukua Kombe,”amesema. 
Aidha, Stewart amepongeza usajili wa kiungo wa kimataifa wa Rwanda, Jean Baptiste Mugiraneza ‘Migi’ kutoka APR ya kwao, akisema ni mchezaji mzuri kwa ujumla.
Migi anakuwa mchezaji wa sita wa kigeni wa Azam kati ya saba wanaotakiwa- na wa kwanza kabisa mpya kusajiliwa msimu huu. Wachezaji wa kigeni waliopo Azam FC ni beki Serge Wawa Pascal, kiungo Kipre Michael Balou, mshambuliaji Kipre Tchetche wote kutoka Ivory Coast, winga Brian Majwega kutoka Uganda na mshambuliaji Didier Kavumbangu wa Burundi ambao wote walikuwepo msimu uliopita.
Jean Baptiste Mugiraneza amefikisha idadi ya wachezaji sita wa kigeni waliosajiliwa Azam FC

Lakini pia, kuna wachezaji wengine wanne wa kigeni wanawania kusajiliwa Azam FC katika nafasi moja iliyobaki, ambao ni makipa Nelson Lukong kutoka Cameroon, Vincent Atchouailou de Paul Angban kutoka Ivory Coast, kiungo Ryan Burge kutoka England na mshambuliaji Allan Wetende Wanga kutoka Kenya.
Lukong na Wanga wamegoma kufanya majaribio na kocha Muingereza Stewart Hall amesema hatasajili mchezaji ambaye hajamuona mazoezini- hivyo nafasi hiyo inaweza kuchukuliwa na Burge anayaendelea na majaribio, kwani hata kipe mwingine Angban anaonekana wa kawaida.
Awali, Azam FC ilisajili wazalendo tu wawili ambao ni kiungo Ramadhani Singano ‘Messi’ kutoka Simba SC na Ame Ali ‘Zungu’ kutoka Mtibwa Sugar.
Azam imepangwa Kundi C pamoja na Malakia ya Sudan Kusini, Adama City ya Ethiopia na KCCA ya Uganda, wakati Kundi A kuna wenyeji wengine, Yanga SC, Gor Mahia ya Kenya, Telecom ya Djibout, KMKM ya Zanzibar na Khartoum-N ya Sudan na Kundi B kuna APR ya Rwanda, Al-Shandy ya Sudan, LLB AFC ya Burundi, Heegan FC ya Somalia.

SIMBA WATUMIA MUDA WAO KUWALIWAZA WATOTO YATIMA WA LUSHOTO


Pamoja na maandalizi ya kambi mjini Lushoto, Simba wametumia muda wao mchache kutembelea kituo cha watoto yatima cha Irente.


Wakiongozwa na Kocha Dylan Kerr, Simba na kikosi chao kizima walitua katika kituo hicho kilichopo Lushoto pia na kuzungumza na watoto hao ikiwa ni pamoja na kuwaliwaza.
Kerr alionekana kufurahishwa na suala hilo na kusema lilikuwa jambo zuri.


“Kama watu wanaoaminika au wanaotazamwa na jamii, ni jambo jema kuungana na wanajamii wengine kama tulivyofanya,” alisema Kerr raia wa Uingereza.

CHELSEA WALIVYOTUA NCHINI CANADA TAYARI KWA MAANDALIZI YA MSIMU MPYA

CHELSEA WAMETUA JIJINI MONTREAL NCHINI CANADA KWA AJILI YA MAANDALIZI YA MSIMU MPYA WA LIGI KUU ENGLAND. CHEKI WALIVYOWASILI.