SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Mar 4, 2016

HIVI NDIO VIWANGO VIPYA VYA SOKA MWEZI MARCH

Na Haji balou

List ya viwango vipya vya soka ulimwenguni imetangazwa March 3 2016, FIFA imetangaza viwango hivyo vya FIFA na nchi ya Ubelgiji
ambayo anacheza soka la kulipwa mtanzania Mbwana Samatta ipo nafasi ya kwanza ikufuatiwa na Argentina.

Tanzania ipo nafasi ya 125 ukilinganisha na miezi miwili nyuma ilikuwa 126 huku kwa upande wa nchi za Afrika Mashariki Uganda imeendelea kuongoza kwa kushika nafasi ya 67 , Rwanda ipo nafasi ya 85 na Kenya ipo 103 ambapo kwa
Afrika nzima Ivory Coast ndio wanaongoza huku kwenye list ya dunia wakishika nafasi ya 36.
Hii hapa ndiyo orodha ya Fifa ya mataifa bora Afrika Machi 3 2016:

1. Visiwa vya Cape Verde
2. Ivory Coast
3. Algeria
4. Ghana
5. Tunisia
6. Senegal
7. Misri
8. DR Congo
9. Congo
10. Cameroon

MESSI APIGA TATU BARCA YAUWA 5-1 LA LIGA

NA Haji balou
BARCELONA imezidi kukimbia kivuli
chake katika Ligi Kuu ya Hispania,
maarufu kama La Liga baada ya
ushindi wa mabao 5-1 usiku huu dhidi ya wenyeji Rayo Vallecano Uwanja wa Rayo Vallecano mjini Madrid.

Mwanasoka bora kabisa kuwahi
kutokea duniani, Lionel Messi
amefunga mabao matatu peke yake
usiku huu katika dakika za 23, 53 na
72, huku mabao mengine ya Barca
yakifungwa na Ivan Rakitic dakika ya
22 na Arda Turan dakika ya 86.
Lionel Messi akishangilia baada ya
kuifungia mabao matatu peke yake
barceloma ikishinda 5-1 dhidi ya Rayo Vallecano katika La Liga.

Bao pekee Rayo Vallecano
limefungwa na mshambuliaji wa
kimataifa wa Angola, Manucho
Goncalves dakika ya 57 na sasa
Barca inafikisha pointi 66 baada ya
kucheza mechi 26 na kuendelea
kujinafasi kileleni mwa La Liga,
ikifuatiwa na Atletico Madrid yenye
pointi 61 za mechi 27 na Real Madrid
yenye pointi 57 za mechi 27 pia.
Rayo Vallecano inabaki na pointi zake 26 za mechi 26 na kuendelea kushika nafasi ya 16 katika ligi ya timu za 20.

Katika mchezo huo, Rayo
iliwapoteza wachezaji wake wawili
waliotolewa kwa kadi nyekundu, Diego Llorente aliyemchezea vibaya Rakitic dakika ya na Manuel Iturra
aliyemuangusha Luis Suarez kwenye
boksi. Lakini Suarez alikosa penalti
iliyotolewa baada ya kuangushwa
kwake.