SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Mar 20, 2015

VAN GAAL AKUALI YAISHE ATANGAZA KUJIENGUA


Meneja wa klabu ya Man Utd, Louis van Gaal ametangaza kustahafu kufanya kazi aliyo nayo sasa mara atakapomaliza mkataba wake na klabu hiyo ya nchini England.
Van Gaal, sanjari na wachezaji wake mwishoni mwa juma hili watakabiliwa na mchezo muhimu katika ligi ya nchini England dhidi ya mahasimu wao wakubwa nchini humo Liverpool katika uwanja wa Anfield.
Meneja huyo kutoka nchini Uholanzi amethibitisha kukaa kwake pembeni katika mchezo wa soka kama meneja mara baada ya kumalizana na Man utd mwaka 2017, alipozungumza na vyombo vya habari kuelekea katika mchezo huo wa ligi uliopangwa kucheza siku ya jumapili.
Van Gaal, amesema kazi ya kukiongoza kikosi cha Man Utd ni ya mwisho kwake na hafikirii kuendelea kutokana na kuhitaji muda wa kupumzika baada ya kuutimikia mchezo wa soka kwa zaidi ya miaka 20 sasa.
'Nimeshazeeka sasa, hii Itakua kazi yangu ya mwisho' Alisema Van Gaal katika mkutano na waandishi wa habari.
'Nimeshazungumza na familia yangu na kuweka wazi msimamo huu, ambao utanisaidia kuwa karibu na watoto, wajukuu pamoja na mke wangu ambaye kwa kipindi kirefu amekua mpweke kutokana na shughuli nizifanyazo.' Aliongoza Van Gaal
Van Gaal alikubali kukichukua kikosi cha Man Utd baada ya kutimuliwa kwa David Moyes mwishoni mwa msimu uliopita, na alitarajiwa kuwa na mtazamo wa kukibadilisha kikosi cha klabu hiyo msimu huu, lakini mambo yamemuendea kombo.
Kabla ya kuikubali kazi ya Man Utd, Van Gaal alikua kocha mkuu wa timu ya taifa ya Uholanzi ambayo ilishiriki fainali za kombe la dunia huko nchini Brazil na kuishi katika hatua ya nusu fainali, kabla ya kushika nafasi ya tatu kwa kuwafunga wenyeji.

CANNAVARO AREJEA MZIGONI, YU TAYARI KWA MGAMBO KESHO

CANNAVARO (WA TATU KUSHOTO) AKIWA NA WENZAKE WAKIJIFUA KWENYE UWANJA WA MKWAKWANI MJINI TANGA, LEO.
Nahodha wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ amerejea mazoezini na kuungana na wenzake mjini Tanfa.

Cannavaro ambaye alishonwa nyuzi saba baada ya kupasuka usoni wakati wa mechi ya watani wao Simba, leo amejifua na wenzake kwenye Uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga.
Akionekana yuko fiti, Cannavaro amejifua na wenzake hali inayoonyesha ana nafasi ya kuitumikia Yanga itakapokuwa ikiivaa Mgambo, kesho.

Yanga ipo Tanga, tayari kuwavaa Mgambo ambao mechi iliyopita waliishinda Simba kwa mabao 2-0.

RATIBA ROBO FAINALI UEFA HII HAPA


Shirikisho la Soka Ulaya (Uefa) leo limekamilisha upangaji wa ratiba ya mechi za robo fainali huku Real Madrid ikipewa Atletico Madrid.


Wapinzani hao wakubwa kutoka nchini Hispania walicheza fainali ya mwaka jana ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na Real Madrid kuibuka na ushindi, tena katika dakika za mwisho.

Barcelona wao watakutana na kiboko ya Chelsea, yaani PSG.

FC Porto wanakutana na mzigo wa Bayern Munich na Juventus wao watapambana na AS Monaco ya Ufaransa iliyoitoa Arsenal.

Mechi:
PSG Vs Barcelona
Atletico Madrid Vs Madrid
Porto Vs Bayern

Juve Vs Monaco

SSERUNKUMA YUPO SIMBA MILELE, WAKALA ASEMA

Na Vincent Malouda, NAIROBI
WAKALA wa straika la Simba SC Dan Sserunkuma, Ken Joseph, amesisitiza kuwa mteja wake yungali mchezaji wa Wekundu wa Msimbazi hadi mkataba wake utakapomalizika mwishoni mwa mwaka 2016.
Kumekuwepo na tetesi kuwa raia huyo wa Uganda tayari amewaandikia viongozi wa Simba barua akielezea azma ya kusitisha mkataba wake mwishoni mwa msimu huu kufuatia kutoridhishwa kwake kukalishwa kwenye benchi.
Sserunkuma hajarejea kambini baada ya kupewa ruhusa ya muda kushughulikia maswala ya kifamilia. Alitarajiwa kurejea Dar Jumamosi iliyopita baada ya kuondokea kwao Uganda pindi tu Simba ilipolazwa na Yanga taifa Machi 8.
Dan Sseunkuma kulia akiichezea Simba SC katika Ligi Kuu

“Naweza kukuthibitishia kwamba Dan Sserunkuma ni mchezaji wa Simba SC. Dan alipewa ruhusa ya siku chache na klabu kwenda nyumbani kisha arejee kambini. Ninachojua ni kwamba hakuna tatizo lolote kati ya Sserunkuma na Simba wala hajaniambia jambo lolote kuhusu kuondoka klabu hiyo, “ wakala huyo mzawa wa Uingereza na mwenye uraia wa Nigeria aliliambia BIN ZUBEIRY.
“Pia ijulikane kuwa Sserunkuma ni mchezaji mwenye hadhi ya juu jinsi wasifu kazi wake unavyosoma.”
Sserunkuma alisajiliwa Simba mwezi Desemba kutokea Gor Mahia ya Kenya alipomaliza mfungaji bora wa ligi kuu Kenya kwa magoli 16 na hadi kufikia sasa amecheka na nyavu mara tatu tu.
Amewahi kuzichezea Express FC na Victors FC za Uganda na vile vile Nairobi City Stars ya Kenya na pia kufanya majaribio nchini Armenia na Denmark.

ALICHOSEMA SSERUNKUMA KUHUSU UCHAWI SIMBA

http://shaffihdauda.co.tz/wp-content/uploads/2015/03/dan-serunkuma.jpg

Mshambuliaji wa klabu ya Simba pamoja na Timu ya Taifa ya Uganda, Dan Sserunkuma, amefunguka ya moyoni kuhusiana na ushirikina na kusema kuwa, Hajawahi kuambiwa na uongozi wa timu juu ya kutumia maswala hayo licha yakuwa Imani yake hairuhusu Ushirikina. 
Nyota huyo ambaye alikuwa ni mfungaji bora wa ligi kuu ya Kenya kwa misimu miwili iliyopita mfululizo akiwa Gor Mahia, Amesema hayo leo kupitia akaunti yake ya Twitter na kusema kuwa bado anaipenda Simba wala hafikilii kuondoka Msimbazi.
“Napenda kusema yafuatayo, Ninafuraha kuwa Simba, Sitaki kuondoka Simba, Sijawahi kulalamika kubaguliwa Simba, Sijawahi kulazimishwa na uongozi kutumia Uchawi kama ambavyo siamini” Ameandika Sserunkuma kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter.
facebook_1426798862337

KOCHA ENGLAND ATOA YAMOYONI KUHUSU HARRY KANE

 

Kocha wa timu ya taifa ya England Roy Hodgson amesema ingeshangaza sana kama mchezaji kinda wa klabu ya Tottenham Harry Kane asingejumuishwa katika kikosi cha Nchi hiyo kinachotarajiwa kumenyana na Lithuaniana na Italy.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21, ni miongoni mwa wachezaji 24 wa kikosi cha England ambacho kimetajwa na Hodgson kucheza dhidi ya Lithuania mchezo ambao utapigwa katika dimba la Wembley mnamo march ,27 mwaka huu kwaajili ya mechi za kufuzu katika mashindano katika mataifa ya Ulaya yanayotarajia kufanyika mwakani. Kikosi hicho pia kinatarajia kuumana na Italy katika mchezo wa kirafiki utakaopigwa mjini Turin huko Italy tarehe 31 mwezi huu.

KILICHOANDIKWA KWENYE KURASA ZA MBELE NA ZA NYUMA MAGAZETI YA MICHEZO LEO IJUMAA.

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

HANS POPPE: KANUNI MPYA ‘HATUJABUGI’, ACHENI UMBEYA


Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
MWENYEKITI wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe amesema kwamba anashangazwa na habari za upotoshaji zinazoenezwa kuhusu kanuni mpya ya adhabu za kadi, kwamba klabu yao ilipotoshwa.
Akizungumza na BIN ZUBEIRY jana Dar es Salaam, Hans Poppe amesema watu wamekuwa wakieneza uvumi kwamba kanuni ya kumuombea mchezaji mwenye kadi kucheza mchezo unaofuata ili akose mwingine baadaye haikupitishwa.
Hans Poppe amesema huo si ukweli, kwani kanuni hiyo ilipitishwa na Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) katika kikao chake cha Februari 8, mwaka huu. 
Hans Poppe akiwa na Makamu Mwenyekiti wa Yanga SC, Clement Sanga kulia

Amesema baada ya hapo, klabu zilisambaziwa barua iliyosainiwa na Katibu wa TFF, Selestine Mwesigwa kujulishwa juu ya kanuni hiyo mpya na Simba SC walifikishiwa waraka huo.
“Sisi tulipoipata hiyo barua, tukatumia fursa hiyo kwa kuwaombea wachezaji wetu ambao walikuwa kwenye mazingira hayo, ajabu sasa watu wanaanza kuleta mizengwe,”amesema Hans Poppe.
Kumekuwa na madai kwamba, kanuni hiyo ilijadiliwa tu katika kikao cha Kamati ya Utendaji ili ianze kutumika msimu ujao, lakini Mjumbe mmoja wa Kamati ya Utendaji ya TFF, ambaye pia ni kiongozi wa Simba SC akaenda kuipotosha klabu yake.
Wazi anayelengwa hapo ni Makamu wa Rais wa Simba SC, Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ ambaye ndiye Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF na Hans Poppe amesema; “Sisi hatukuambiwa na Kaburu, tuliletewa barua na TFF na nakala tunayo,”amesema.

Simba SC ilitumia fursa hiyo mara mbili, kwanza kwa mchezaji Abdi Banda iliyemtumia katika mchezo dhidi ya Stand United mjini Shinyanya, japo ilifungwa 1-0 na baadaye Ibrahim Hajibu katika mchezo dhidi ya Prisons.
Simba SC iliifunga Prisons 5-0 na tangu hapo kumekuwa kuna malalamiko juu ya Hajibu kucheza akiwa ana kadi tatu za njano, licha ya klabu hiyo kutoa ufafanuzi wa kutumia fursa ya kanuni mpya.

AIBU HII HAIJAWAHI KUTOKEA ENGLAND!

EVERTON imekuwa timu ya mwisho ya England na Uingereza kwa ujumla kutolewa katika michuano ya Ulaya, baada ya kufungwa mabao 5-2 Dynamo Kiev usiku wa Alhamisi.
Everton inatolewa katika hatua ya 32 Bora kwa jumla ya mabao 6-4, baada ya awali kushinda 2-1 nyumbani.
Romelu Lukaku gave his side hope but his equaliser proved to be a false dawn for Everton, who subsequently conceded four
Romelu Lukaku akishangilia baada ya kuifungia Everton ikilala 5-2 mbele ya wenyeji Dynamo Kien nchini Ukraine usiku wa Alhamisi

KLABU ZA ENGLAND ZILIVYOVURUNDA ULAYA MSIMU HUU

Liverpool, (February 26, Europa League last 32): Baada ya kushika nafasi ya tatu katika makundi Ligi ya Mabinhgwa, LIverpool ilitolewa na Besiktas kwa penalti.
Tottenham (February 26, Europa League last 32): Ilitolewa na Fiorentina kwa kufungwa 2-0 mechi ya marudiano.
Chelsea (March 11, Champions League last 16): Came a cropper against 10-man Paris Saint-Germain in extra time.
Arsenal (March 17, Champions League last 16): Ilitolewa kwa mabao ya ugenini licha ya kushinda  2-0 mjini Monaco.
Manchester City (March 18, Champions League last 16): Mabingwa wa England walifungwa nyumbani na ugenini na Barcelona.
Everton (March 19, Europa League last 32): Ilifungwa 5-2 na Kiev nchini Ukraine.
Hii inakuwa mara ya kwanza tangu kuanzishwa kwa Ligi Kuu ya England, nchi hiyo inakosa timu katika hatua ya Robo Fainali ya michuano ya Ulaya.
Hiyo inafuatia kutolewa kwa timu za Arsenal, Manchester City na Chelsea katika hatua ya 16 Bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Man City juzi ilifungwa 1-0 na Barcelona, bao pekee la Ivan Rakitic dakika ya 31, akimalizia krosi ya Lionel Messi na kutolewa kwa kipigo cha jumla cha mabao 3-1, baada ya awali kufungwa 2-1 England.
Katika mchezo huo, mshambuliaji wa Manchester City, Sergio Aguero alikosa penalti dakika ya 78 ambayo iliokolewa na kipa Marc-Andre ter Stegen. Penalti hiyo ilitolewa baada ya yeye mwenyewe kuangushwa na Gerard Pique.
Arsenal ilitolewa kwa sheria ya mabao ya ugenini, baada ya kushinda 2-0 dhidi ya Monaco nchini Ufaransa na kufanya sare ya jumla ya 3-3, kufuatia awali kufungwa 3-1 nyumbani.
Chelsea ilitupwa nje kwa mabao ya ugenini pia, baada ya sare ya jumla ya 3-3 na PSG ya Ufaransa. Hiyo ilifuatia Chelsea kutoa sare ya 2-2 nyumbani baada ya awali kulazimisha sare ya 1-1 ugenini na timu hiyo ya Ufaransa.


EVERTON NAYO NJE MICHUANO YA ULAYA

A disconsolate Everton attempt to come to terms with the glut of goals they conceded, but were made to play for defensive errors
Wachezaji wa Everton wakiwa hoi jana Uwanja wa NSK Olimpiyskiy mjini Kiev, baada ya kufungwa mabao 5-2 na wenheji Dynamo Kiev katika mchezo wa marudiano hatua ya 16 Bora Europa League hivyo kutolewa kwa jumla ya mabao 6-4, baada ya awali kushinda 2-1 nyumbani.