SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Apr 10, 2016

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOOL AKIUA 4-1

Na Haji balou
Mshambuliaji Divock Origi akikimbia
kushangilia baada ya kuifungia
Liverpool bao la tatu katika ushindi
wa 4-1 dhidi ya Stoke City kwenye
mchezo wa Ligi Kuu ya England jioni
ya leo Uwanja wa Anfield. Origi
alifunga mabao mawili, wakati
mengine yamefungwa na Alberto
Moreno na Daniel Sturridge na la
Stoke limefungwa na Bojan Krkic

VARDY APIGA MBILI LEICSTER YAZADI KUKAA KILELENI

Na Haji balou
Leicester imeitungua Sunderland kwa mabao 2-0, yote mawili yakiwa
yamefungwa na mshambuliaji wake hatari Jamie Vardy.

Vardy amefikisha mabao 21 akiwa
anakimbilia ufungaji bora, huku Leicester iliyobakiza mechi tano tu za Ligi Kuu England ikiwa imeanza kusikia harufu ya ubingwa.

Ushindi huo unaifanya ifikishe pointi 72, nafasi ya pili Tottenham wakiwa na pointi 62 na Arsenal katika nafasi ya tatu wakiwa na pointi 59.

BARCA YAPIGWA YAWEKA UBINGWA REHANI

Mikel Oiarzabal aliifungia Sociedad bao pekee dakika ya 5 kipindi cha kwanza lililowapa pointi tatu huku Barca ikishindwa kusawazisha goli hilo hadi dakika 90 zinamalizika.

Kichapo hicho kimewafanya Barca kusogelewa na Atletico Madrid kwenye mbio za ubingwa ambapo sasa Barcelona inaididi Atletico kwa pointi tatu, Barcelona ambao ndiyo vinara wa ligi wanapointi 76 wakifuatiwa na Atletico yenye pointi 73 huku Madrid ikiwa nyuma yao na pointi zake 72 wakati huo timu zote zikiwa zimecheza mechi 32 na kusaliwa na mechi sita pekee ili msimu kumalizika.