SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Apr 29, 2015

VAN PERSIE ‘AFUFUKA’, APIGA MBILI MAN UNITED IKISHINDA 4-1 ENGLAND

MSHAMBULIAJI Robin van Persie usiku huu amefunga mabao mawili katika ushindi wa 4-1 wa  U21 ya Manchester United dhidi ya vijana wenzao wa Fulham Uwanja wa Craven Cottage.
Van Persie ambaye amekuwa nje ya Uwanja tangu Februari kutokana na majeruhi, alifunga mabao hayo katika dakika za 13 na 80, huku mabao mengine ya United yakifungwa na Joe Rothwell dakika ya 20 na 43.
Mholanzi huyo, Van Persie alirejea uwanjani kikosi cha kwanza cha United Jumapili timu hiyo ikifungwa 3-0 na Everton katika LIgi Kuu ya England.
Kikosi cha Fulham kilikuwa: Norman, Donnelly, Buatu, Baba, Sheckleford, Mesca, Edun/de la Torre dk67, Smile, Evans, Plumain, Redford/Humphreys dk60.
Manchester United: Lindegaard, Love, Blackett, Thorpe, Kellett, Rothwell/Willock dk81, Goss/Fletcher dk88, Grimshaw, Pereira, Van Persie/Weir dk81 na Januzaj.
Van Persie made an appearance for Manchester United Under 21s away at Fulham on Tuesday night
Van Persie akipongezwa na wenzake baada ya kufunga mabao mawili katika ushindi wa 4-1 wa U21 ya Manchester United dhidi ya Fulham usiku wa Jumanne

FERGUSON: RONALDO ANAWEZA KUNG'ARA POPOTE, HATA MILLWAL, QPR... MESSI NI WA BARCELONA TU

KOCHA wa zamani wa Manchester United, Sir Alex Ferguson ametaja sababu za wakati wote kumuona Cristiano Ronaldo yuko juu ya Lionel Messi wakati anazungumza na John Parrott wakicheza pool table, maarufu pia kama snooker.
Kocha huyo mwenye mafanikio makubwa zaidi katika historia ya soka ya Uingereza amezungumza na Parrott na mtangazaji Hazel Irvine katika mahojiano maalum ya BBC ya michuano ya Ubingwa wa Dunia Crucible.
Ferguson amesema wakati wote anaulizwa nani ni mchezaji bora duniani?, kabla ya kufafanua kwa nini humchagua mchezaji wake wa zamani United dhidi ya nyota wa Barcelona.
Former Manchester United amanger Sir Alex Ferguson (left) speaks with John Parrott over a frame of snooker
Kocha wa zamani wa Manchester United, Sir Alex Ferguson (kushoto) akizungumza na John Parrott kwenye meza ya snooker

Ferguson anaamini Cristiano Ronaldo ni mzuri zaidi ya Lionel Messi kwa sababu anaweza kufunga akiwa na timu yoyote

"Watu wengi kwa urahisi tu wanasema Messi na huwezi kukataa maoni yao,"alimuambia bingwa wa mwaka 1991 wa Snooker duniani.
"Ronaldo anaweza kuchezea Millwall, QPR, Doncaster Rovers, (timu moja) yoyote, na akafunga hat-trick. Sina uhakika kama Messi anaweza kufanya hivyo. Ronaldo yuko fiti mno, ana kasi, mzuri wa kurukia mipira ya juu kupiga kichwa na mkali.
"Nafikiri Messi ni mchezaji wa Barcelona,' amesema.
Kocha huyo wa zamani wa United wakati wote amekuwa na uhusiano mzuri na nyota huyo anayecheza Real Madrid kwa sasa tangu aondoke Old Trafford, na Ferguson anampa heshima Mreno huyo sambamba na Ryan Giggs na Paul Scholes kama wachezaji bora duniani aliowahi kuwafundisha.

MESSI, SUAREZ KILA MMOJA APIGA MBILI BARCA IKIUA 6-0

TIMU ya Barcelona imezidi kuukaribia ubingwa wa Ligi Kuu Hispania, La LIga baada ya leo kuifunga Getafe mabao 6-0 Uwanja wa Nou Camp na sasa inawazidi Real Madrid kwa pointi tanio.
Lionel Messi aliwafungia wenyeji bao la kwanza dakika ya 10 kwa mkwajunwa penalti baada ya Luis Suarez kuangushwa. 
Luis Suarez akaifungia Barca bao la pili dakika ya 25, kabla ya Neymar Jnr kufunga la tatu dakika tatu baadaye na hilo kuwa bao la 100 kwa timu yake hiyo msimu huu.
Xavi akaifungia bao la nne timu ya Luis Enrique dakika ya 30, kabla ya Suarez kufunga lake la pili katika mchezo huo na la tano kwa Barca dakika ya 40 na Messi akafunga bao lake la 48 msimu huu la sita kwa timu yake dakika mbili tu baada ya kuanza kipindi cha pili.
Kikosi cha Barcelona kilikuwa: Bravo, Alves/Montoya dk68, Bartra, Mathieu, Adriano, Busquets, Xavi/Pedro dk59, Rafinha, Suárez, Messi na Neymar.
Getafe: Guaita, Alexis, Lago, Velazquez, Lacen, Arroyo, Pedro Leon/Escudero dk76, Baba, Juan Rodriguez/Felip dk65, Freddy na Emi.
Neymar celebrates with Lionel Messi after giving Barcelona a 3-0 lead at the Nou Camp on Tuesday night
Neymar akisherehekea na Lionel Messi baada ya kuifungia Barcelona bao la tatu usiku huu