SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Mar 31, 2015

YAYA TOURE AFIKIRIA KUIVUA 'KIMOJA' JEZI YA IVORY COAST

KIUNGO Yaya Toure amesema anafikiria kustaafu soka ya kimataifa baada ya kutimiza malengo yake.
Toure aliiongoza nchi yake kama Nahodha kutwaa Kombe la Mataifa ya Afrika, hilo likiwa taji la kwanza kubwa baada ya zaidi ya miongo miwili na sasa anaweza kufuata nyayo za kaka yake, Kolo kuvua jezi Ivory Coast.
Toure amesema atachukua siku kadhaa kuamua mustakabali wake, lakini amependekeza, kizazi kipya sasa lazima kipewe nafasi kikosi cha Tembo.
Toure was in action during the draw with Equatorial Guinea in Abidjan, Ivory Coast, on Sunday 
Toure aliichezea Ivory Coast ikitoa sare na Equatorial Guinea mjini Abidjan Jumapili katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa

"Mustakabali wangu?' aliuliza, alipoulizwa na BBC. "Inabidi usubiri. Sasa, malengo yangu yametimia. Tunapaswa kusubiri kwa siku kadhaa na kuona tutafanya nini,".
"Kaka yangu amestaafu, na Copa (Barry, kipa wa muda mrefu wa Ivory Coast) naye pia. Muda wa nyota wanaochipukia utafika karibuni. Tunahitaji kuwaachia wao.
Maneno haya ya Toure yanaweza kuwa habari njema kwa klabu yake, Manchseter City, ambayo ilikuwa katika wakati mgumu kwa kumkosa mchezaji huyo alipokuwa kwenye Fainali za Mataifa ya Afrika nchini Equatorial Guinea.

DI MARIA AONGOZA MAUZO YA JEZI ENGLAND

HIZI ni habari njema ambazo zinaweza kumfariji Angel di Maria.
Mwanasoka huyo wa kimataifa wa Argentina amekuwa ana msimu mgumu Manchester United uwanjani, lakini kiwango chake hakijaathiri umaarufu wake nje ya Uwanja kutokana na jezi kuongoza kwa mauzo katika Ligi Kuu ya England.
Kwa mujibu wa muuzaji wa reja reja wa duka la Sports Direct, ambaye anauza jezi za timu za Arsenal, Aston Villa, Chelsea, Liverpool, United, Manchester City, Tottenham na Newcastle, jezi ya Di Maria inauliziwa na mtu mmoja karibu katika kila wanunua jezi tofauti 10. 
Manchester United's record summer signing Angel di Maria tops the list of SportsDirect player shirt sales 
Mchezaji ghali wa Manchester United, Angel di Maria anaongoza kwa kuuza jezi katika orodha ya SportsDirect
Di Maria, Sanchez and Costa make up with top three with a combined share of 15.66 per cent
Di Maria, Sanchez na Costa ndio wamo kwenye tatu bora wote kwa pamoja wakiwa na asilimia 15.66

Jumla ya asilimia yake ni 9.59 ambayo inamfanya aongoze sokoni, akifuatiwa na nyota wa Arsenal, Alexis Sanchez, mchezaji huyo wa Chile akiwa nafasi ya pili kwa asilimia 3.8.
Di Maria amekuwa katika wakati mgumu uwanjani tangu asajiliwe kwa dau la Pauni Milioni 59.7 kutoka Real Madrid.