SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Mar 6, 2015

HERRERA: TUNAIHESHIMU ARSENAL


ander HerreraNa Amplifaya Amplifaya
Mchezaji kutoka Manchester United Ander Herrera amesema kuwa wanaisubiri Arsenal kwa nguvu zote hapo jumatatu katika kombe la FA huku akisema kwa mkazo kuwa hawaiogopi bali wanaiheshimu.
Mara baada ya mechi ya mwisho kuisha na Manchester United kupata point 3 dhidi ya Newcastle jana jumatano Herrera na kikosi chake kwa ujumla sasa nguvu zao zimebakia kwenye mechi ijayo dhidi ya Arsenal kwenye kombe la FA tu katika uwanja wa Old Trafford.
Herrera ambaye amekuwa katika kiwango kizuri hasa katika siku hizi za usoni inampa picha nzuri katika muelekeo wa mechi ijayo kukutana na washika bunduki hao na huku Kocha wake akiwa na matarajio ya kufika fainali itakayochezwa katika uwanja wa Wembley huko huko England mnamo May 5.
” Sasa hivi tunaangalia mbele zaidi hasa mechi yetu ijayo dhidi ya Arsenal, sababu ndiyo nafasi nzuri zaidi ya kutwaa kombe”  Alisema hayo wakati anaongea na MUTV.
Herrera aliongezea kwa kusema kuwa ” Inatakiwa tuwaheshimu sana Arsenal sababu wanacheza vizuri, sisi ni Manchester United na hatuogopi, tunaenda kucheza mbele ya mashabiki wetu na hatuna budi kushinda” alisema Herrera.
Arsenal Wenger alifanikiwa kushinda pia katika mechi yake ya mwisho dhidi ya Crystal Palace wa 2-1 huku ukiwa ni ushindi wake wa 8 katika mechi 10 za ligi.

KIINGILIO SIMBA NA YANGA SC SH. 7,000 BEI NAFUU

Na Baraka Kizuguto, DAR ES SALAAM
SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limetangaza viingilio vya mchezo wa siku ya jumapili kati ya Simba SC na Young African utakaofanyika kwenye dimba la Uwanja wa Taifa kuanzia majira ya saa 10 kamili za jioni.
Mchezo huo utachezeshwa na mwamuzi Martin Saanya kutoka Morogoro, akisaidiwa na Soud Lila (DSM) mshika  kibendera wa kwanza, Florentina Zabron (Dodoma) mshika kibendera wa pili, Mwamuzi wa akiba Israel Mjuni (DSM), na kamisaa wa mchezo ni Ame Santimeya (DSM).
Viingilio vya mchezo huo,  VIP A sh. 40,000, VIP B sh. 30,000, VIP C sh. 20,000, Rangi ya Machungwa (Orange) sh. 10,000, huku Rangi ya Bluu na Kijani ikiwa ni sh. 7,000.

Tiketi zitaanza kuuzwa keso (jumamosi) saa 2 kamili asubuhi katika vituo vya,  Karume (Ofisi za TFF), Mgahawa wa Steers (Posta Mpya), Oilcom (Buguruni), BigBon (Kariakoo),  Olicom (Ubungo), Dar Live (Mbagala), Uwanja wa Uhuru, Kivukoni (Ferry) na Makumbusho (kituo cha mabasi).
Magari yenye vibali maalum ndiyo yatakayoruhusiwa kuingia ndani ya uwanja siku ya jumapili kwa kupitia barabara ya Mandela na Uwanja wa Uhuru, barabara ya Chang'ombe itafungwa kuanzia saa 12 kamili asubuhi.
TFF inawaomba, wapenzi, washabiki na wadau wa mchezo kununua tiketi katika vituo vilivyotajwa ili kuepuka kuuziwa tiketi bandia, ili kuimarisha ulinzi na usalama wa mchezo, mashabiki wenye mabegi, silaha, vilevi na chupa za maji hawataruhusiwa kuingia navyo uwanjani.
Aidha katika mchezo huo TFF itatoa ujumbe maalum kupitia kwa wachezaji kuhamasisha juhudi za Taifa za kuzuia mauaji dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi (Albino).

TAIFA STARS KUIVAA MALAWI

TIMU ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) itashuka dimbani Machi 29 mwaka huu, kucheza mchezo wa kirafiki na timu ya Taifa ya Malawi (The Flames) katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Mchezo huo wa kirafiki ambao upo katika kalenda ya FIFA kwa timu za Taifa (Machi 23-31) na utatarajiwa kuanza majira ya saa 10 na nusu jioni kwa saa za Afrika Mashariki.


RAIS KIKWETE AZINDUA STUDIO ZA KISASA ZA AZAM TV TABATA LEO


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete akifunua jiwe la msingi la jengo la Azam TV, Tabata Relini, Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa studio za kisasa kampuni hiyo.

Rais Kikwete akikata utepe wa jengo la studio za Azam FC. Kulia ni Mwenyekiti wa makampuni ya Bakhresa Group, wamiliki wa Azam Media Limite, ambao ndiyo wamiliki wa Azam TV, Alhaj Sheikh Said Salim Awadh Bakhresa na kushoto ni Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk Fenella Mukangara. 

Rais Kikwete akizundua studio za Azam TV kwa kutangaza pamoja na mzee Bakhresa kushoto
Mkurugenzi Mkuu wa Azam Media Limited, Yussuf Bakhresa katika hafla hiyo  

Rais Kikwete akijibu maswali ya mtangazaji mkongwe nchini, Tido Mhando (kushoto) ambaye ni Naibu Mtendaji Mkuu wa Azam Media Limited 

Rais Kikwete akielekezwa jambo na wahusika ndani ya studio hizo

Mtendaji Mkuu wa BIN ZUBEIRY Blog, Mahmoud Zubeiry (kulia) akiwa na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Alhadi Mussa Salim na wanasiasa, Mwigulu Mchemba na Ibrahim Lipumba katika hafla hiyo
Wakuu wa Azam TV wakifurahia hotuba ya Rais Kikwete

Rais Kikwete katika picha ya pamoja na Watangazaji wa Azam TV

Mkurugenzi wa Azam TV, Yussuf Bakhresa kulia akiwa na Waziri Fenella, Rais Kikwete na baba yake, mzee Bakhresa katika meza kuu

Wasanii Mwasiti na Barnaba wakitumbuiza katika shughuli hiyo      

KURASA ZA MWANZO NA ZA MWISHO ZA MAGAZETI YA MICHEZO LEO MARCH 6

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

ALICHOSEMA SCHOLES KUHUSU MAN UNITED

KIUNGO wa zamani wa klabu ya Manchester United, Paul Scholes (pichani) amesema kuwa timu hiyo inaonekana kucheza katika kiwango cha chini kwa msimu huu kuliko msimu uliopita licha ya kuwa kocha Louis Van Gaal ametumia kiasi kikubwa katika kufanya usajili.
Kiungo huyo ambaye kwa sasa ni mchambuzi wa soka katika kituo kimoja cha televisheni huko nchini Uingereza amesema kuwa kocha huyo mholanzi anaonekana kuridhika na kufurahishwa kwa timu yake kushika nafasi ya nne katika msimamo wa ligi nchini humo.
Scholes ambaye alitundika daruga mwaka 2013 baada kucheza kwa muda mrefu aliyasema hayo jana mara baada ya Manchester United kuibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya Newcastle United huku pia akionekana kutoridhishwa na aina ya ufundishaji ya kocha Louis Van Gaal.
"Anaonekana anafuraha kushika nafasi ya nne lakini timu hii inahitaji kuwepo katika mbio za ubingwa kwa sababu ametumia paundi milioni 150 katika usajili " alisema Scholes.
Aidha Scholes amesema kuwa haipaswi kumlaumu sana kocha huyo kwa msimu huu kwani ndiyo msimu wa kwanza lakini kwa msimu ujao inabidi awaridhishe mashabiki wa timu hiyo ambao wamekuwa wanyonge tangu Sir Alex Ferguson astaafu mwaka 2013.

PICHA; MWONEKANO WA STUDIO ZA AZAM TV ZILIZOGHARIMU BILIONI 56

Mwonekano wa studio mpya na kisasa za Azam TV zilizopo Tabata Relini, Dar es Salaam ambazo ujenzi wake umegharimu zaidi ya dola za Kimarekani Milioni 31 ambazo ni zaidi ya Sh. Bilioni 56 za Tanzania.

Ni studio zenye hadhi ya kimataifa

Naibu Mtendaji Mkuu wa Azam Media Limited, Tido Mhando (kushoto) akimuelekeza jambo Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Yussuf bakhresa (kulia) jana 

Studio hizi zinatarajiwa kuzinduliwa leo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete

HAWA NDIO WACHEZAJI MATAJIRI DUNIANI

MRENO Cristiano Ronaldo ndiye mwanasoka tajiri zaidi duniani akiwa na utajiri wenye thamani ya Pauni Milioni 152, ikiwa ni Pauni Milioni 7 zaidi ya hasimu wake mkubwa, Muargentina Lionel Messi.
Baada ya msimu mzuri wa 2014, ambao ilishuhudiwa Ronaldo akiiwezesha Real Madrid kutwaa taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya naye akishinda tuzo ya Mwanasoka Bora wa Dunia, maarufu kama Ballon d'Or, ameongeza idadi ya utajiri anaomzidi nyota wa Barcelona na Argentina.
Kwa mujibu wa Orodha ya Matajiri ya Goal.com, ilitotolewa leo, Ronaldo na Messi bado ndiyo wanasoka wanaofurahia zaidi kazi hiyo kuliko wenzao wote duniani.
The Portuguese retained his Ballon d'Or accolade in Zurich back in January
Cristiano Ronaldo akiwa na tuzo yake ya Ballon d'Or baada ya kukabidhiwa mjini Zurich, Uswisi Januari mwaka huu


ORODHA YA WACHEZAJI 10 TAJIRI ZAIDI DUNIANI 

1. Cristiano Ronaldo £152.3
2. Lionel Messi £145m
3. Neymar £97.9m
4. Zlatan Ibrahimovic £76.1m
5. Wayne Rooney £74.6m
6. Kaka £69.6m
7. Samuel Eto'o £63.1m
8. Raul £61.6m
9. Ronaldinho £60.2m
10. Frank Lampard £58m 
Barcelona's Lionel Messi was second on the Rich List with a personal wealth of £145m
Lionel Messi anashika nafasi yaa pili kwa utajiri wa thamani ya Pauni Milioni 145