SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

May 9, 2015

MAYWEATHER AMGEUZIA KIBAO PACQUIAO, AMUITA MWOGA NA HATAKI KUPIGANA NAYE TENA


BONDIA Floyd Mayweather amemuita mpinzani wake Manny Pacquiao mwoga na amekataa pambano la marudiano.
Mayweather alishinda kwa pointi katika 'Pambano la Karne' la utajiri wa Pauni Milioni 300 mjini Las Vegas mwishoni mwa wiki iliyopita.
Pacquiao baadaye akasema kwamba aliumia bega wiki mbili na siku kadhaa kabla ya pambano akiwa mazoezini na tayari amesema amefanyiwa upasuajji Jumatano.
Manny Pacquiao revealed a shoulder injury in the aftermath of his fight with Floyd Mayweather
Manny Pacquiao baada ya mechi alisema aliumia bega wiki kadhaa kabla

Baada ya pambano hilo, Mayweather alimtumia ujumbe wa maandishi mtangazaji wa ESPN kwamba atajiandaa kwa pambano la marudiano na Pacquiao atakapopona majeruhi yake.
Lakini sasa amegeuza kibao na hataki tena kukutana ulingoni na Mfilipino huyo badala yake anaelekeza nguvu zake kwenye pambano la 49 Septemba mwaka huu na mpinzani mwingine.
"Nilimtumia ujumbe Stephen A Smith kumuambia nitapigana naye (Pacquiao)? Ndiyo, nimebadilisha mawazo," amesema. 
"Kwa wakati huu sasa, hapana, kwa sababu ni kibonde na mwoga. Kama umepigwa, kubali kupigwa na sema, 'Mayweather, ulikuwa mpiganaji bora.' 
Mayweather had initially suggested that he would be willing to fight Pacquiao again but has changed his mind 
Mayweather awali alikubali kurudiana Pacquiao, lakini amebadilisha mawazo