SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Apr 12, 2016

HII NDIO DROO YA NUSU FAINAL KOMBE LA FA

Na Haji balou
YANGA SC itamenyana na Coastal
Union katika Nusu Fainali ya
michuano ya Shirikisho la Soka
Tanzania (TFF), maarufu kama
Kombe la Azam Sports Federations
Cup 2016.

Mchezo huo utafanyika Uwanja wa
Mkwakwani mjini Tanga Aprili 24,
mwaka huu, siku ambayo Azam FC
itamenyana na Mwadui FC Uwanja wa Mwadui Complex, Tanga Aprili 24,
mwaka huu pia.

Hiyo inafuatia droo iliyopangwa leo
studio za Azam TV, wadhamini wa
michuano hiyo, Tabata, Dar es
Salaam na kuhudhuriwa na Katibu wa TFF, Selestine Mwesigwa.

Mshambuliaji wa zamani wa timu ya
taifa ya wanawake, Twiga Stars,
Esther Chabruma ndiye aliyechagua
timu za kumenyana katika Nusu
Fainali katika droo hiyo, akisimamiwa na Ofisa Habari wa TFF, Baraka Kizuguto.

Coastal Union iliingia Nusu Fainali
baada ya kuitoa Simba SC kwa
kuifunga mabao 2-1, wakati Azam FC iliitoa Prisons kwa kuifunga 3-1,
Mwadui FC iliitoa Geita Gold kwa
kufunga 3-0 na Yanga SC iliwafunga
Ndanda FC 2-1.

Bingwa wa Kombe la ASFC, michuano iliyoanza na timu 64 Novemba mwaka jana, ataiwakilisha Tanzania kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika mwakani.

Katika hatua ya awali, kila timu
ilipatiwa fedha za usafiri Sh Milioni 3,
na vifaa vya mashindano kutoka kwa
wadhamini, Azam TV ikiwa ni sehemu ya udhamini wa Bilioni 3.3.

Bingwa wa Kombe la ASFC
atajinyakuliwa kitita cha Sh. Milioni
50, Fainali inatarajiwa kuchezwa wiki
moja baada ya Ligi Kuu ya Vodacom
Tanzania Bara kumalizika.

Mara ya mwisho michuano hiyo
ilifanyika mwaka 2002 na JKT Ruvu
ikaifunga Baker Rangers ya
Magomeni katika fainali, wakati
ikijulikana kama Kombe la FAT
(Chama cha Soka Tanzania).

AZAM YAMZUIA FARID NA HIMID MAO KWENDA ULAYA SABABU IPO HAPA

Na Haji balou
UONGOZI wa Azam FC umezuia safari ya kiungo wake Farid Mussa  kwenda Ubelgiji kwa majaribio
ya kucheza soka ya kulipwa hadi
amalize mchezo wa marudiano wa
hatua ya 16 Bora Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Esperance ya Tunisia Aprili 19.

Awali, makubaliano kati ya wakala wa Farid na Azam ilikuwa ni mchezaji huyo aondoke baada ya mchezo wa kwanza na Esperance uliofanyika Jumapili Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.

Farid alifunga bao moja na kuseti
moja katika ushindi wa 2-1 na baada
ya hapo, benchi la Ufundi chini ya
kocha Muingereza, Stewart Hall
limeona linamuhitaji kinda huyo kwa
mchezo wa marudiano.

Mbali na Farid, kiungo Himid Mao pia
anatarajiwa kwenda Denmark kwenda kujaribu bahati yake.
Mtendaji Mkuu wa Azam FC, Saad
Kawemba, amesema kwamba
wameiomba klabu inayomtaka Farid
kwa majaribio imsubiri kwa wiki moja
zaidi.

“Awali Farid Mussa alitakiwa
kuondoka mara moja kwa ajili ya
majaribio hayo, lakini tumewaomba
wenzetu wanaomtaka wamuache hadi amalizie mechi yetu ya pili dhidi ya Esperance na wamekubali, hivyo Farid ataondoka baada ya mechi hiyo,” alisema.

HUYU NDIYE MWAMUZI ATAKAYE CHEZESHA MECHI YA ATLET VS BARCA REKODI YAKE INAIBEBA ATLETI

Na Haji balou
Mwamuzi wa mechi kali ya Jumatano yenye
ushindani mkubwa sana Ligi ya Mabingwa Uefa, ameteuliwa, ni yule aliyechezesha fainali Kombe la Dunia 2014 Mwamuzi wa Kiitaliano Nicola Rizzoli amepangwa na UEFA kuchezesha mechi ya Ligi ya Mabingwa baina ya Atlético Madrid na Barcelona katika uwanja wa Vicente Calderón timu hizo zikiwa zinawania kutinga nusu fainali ya michuano hiyo.

Hii itakuwa mechi ya saba kwa Rizzoli kuchezesha Ligi ya Mabingwa katika toleo la 2015/16.
Mwamuzi huyo mwenye umri wa miaka 44 anatambulika kwa ubora wake katika kazi yake, si bora tu, ni zaidi ya bora katika ulimwengu wa soka la leo.

Akiwa na uzoefu wa miaka 14 katika Serie A na FIFA tangu 2007, Rizzoli amejizolea sifa kubwa kwa kutenda haki na uwezo wa kuchezesha mechi kubwa.

Kwa mfano, Muitaliano huyo ndiye
aliyepuliza kipyenga fainali ya Kombe la Dunia 2014 Ujerumani dhidi ya Argentina.

Barca na Atlético zina historia ya mechi zilizochezeshwa na Rizzoli. Alikuwa mwamuzi Atletico iliposhinda 2-0 hatua ya makundi dhidi ya Olympiakos dimbani Calderón, hali kadhalia
Atletico iliposhinda 1-0 dhidi ya Bayer Leverkusen msimu uliopita raundi ya 16.