SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

May 24, 2015

HII NI REKODI NYINGINE ALIYOIVUNJA RONALDO BAADA YA MCHEZO WA LEO

Mshambuliaji hatari wa Real Madrid ameivunja rekodi aliyoiweka mwenyewe ya misimu 3 iliopita baada ya kuibuka mfungaji bora wa ligi kuu ya Hispania na kufikisha magoli 61 kwa michuano yote ya msimu huu,amefikisha idadi hiyo baada ya kufunga Hat-trick mapema leo baada ya mchezo wao dhidi ya Getafe.
Matumaini ya kuifukuzia Barcelona katika mbio za ubingwa wa la liga yalifutwa wiki iliyopita lakini hiyo haikuwazui vijana wa Carlo Ancelotti kwa kuanza kwa stlye yaka mchezo wa leo baada ya krosi safi kutoka kwa Marcelo na Ronaldo kijitwisha kichwa safi na kufunga goli la kwanza dakika ya 13 na kuufanya ubao usomeke 1-0.
WAgeni walicharuka na walifunga magoli mawili ya haraka haraka na kuwafanya waongoze hata hivyo Hiyo haikutosha kwa wageni hao baada ya Ronaldo kiungia nyavuni kwa mpira wa adhabu ndogo na kufanya usawa wa magoli na kua 2-2 na kufanya Ronaldo kufikisha magoli 60 na kuifikia rekodi yake ya misimu wa 2011-12.
Lakini rekodi yake hiyo aliivunja dakika mbili baadae baada ya kupata mkwaju wa penati na kufunga na kufanya waongoze kwa goli 3-2 pale Santiago Bernabeu nakua goli lake la 313 katika mechi 300 alizocheza hadi sasa.
Hat-trick ya Ronaldo inamfanya kufikisha goli 48 za ligi msimu huu,hiyo inamfanya kuwa mfungaji bora wa ligi kuu ya Hispania na ulaya nzima kwa ujumla na kumfanya kuchukuia tuzo ya Pichichi,pia amebakisha magoli 10 kumfikia Raul na kuwa mfungaji wa muda wote wa Real Madrid.

NGASSA PUSHAPU 200 KILA SIKU, MAANDALIZI YA PSL SI MCHEZO

Mshambuliaji wa Free State Stars ya Ligi Kuu ya Afrika Kusini, Mrisho Khalfan Ngassa hupiga pushapu 200 kila siku asubuhi kabla ya kuingia kwenye programu nyingine za mazoezi kama kukimbia na kucheza na mpira. 
Mshambuliaji huyo wa zamani wa Yanga SC kwa sasa yupo mapumzikoni akijiandaa na msimu mpya katika klabu mpya, Free State Stars

Ngassa alikuwa kwenye kikosi cha Taifa Stars kilichoshiriki michuano ya Kombe la COSAFA nchini Afrika Kusini na kufanya vibaya, baada ya kufungwa mechi zote tatu za Kundi B