SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Jan 26, 2016

MAKOCHA KUMI WA KIHISTORIA LIGI KUU ENGLAND

Makocha 10 bora katika historia
ya Ligi Kuu ya England
Ligi Kuu ya England huchukuliwa kama ligi bora katika ulimwengu wa soka, ambapo utakuta vilabu kabambe kama Manchester United,
Chelsea, Liverpool na Arsenal na nyingine zenye uwezo katika mchuano. Ni ligi ya kupendeza kwa
watu wengi duniani ambapo kila klabu yaweza kuipika ingine.
Hapa kuna mameneja 10 walioweza kuvutia mioyo ya watazamaji wa soka katika ligi ya
England.

10. Roy Evans( Liverpool)
Ni mwingereza aliyefunza Liverpool tangu 1994 hadi 1998, licha ya kushinda Ligi Kuu ya England
katika awamu ya yake akiwa Anfield, Evans alisaidia klabu ya Merseyside kumaliza katika timu nne za kwanza mara nne mfululizo.

Mechi alifunza: 244
Michezo aliyoshinda: 123
Michezo aliyoshindwa: 58
Michezo aliyotoka sare: 63
Kiwango cha ushindi: 50.41%
Mataji aliyoshinda:
League Cup(1): 1994–95

9. Gerard Houllier ( Liverpool )
Mfaransa alichukuwa klabu mnamo 1998 baada
ya Roy Evans kustaafu alipopigwa kimbwa 3-1 katika League Cup na Tottenham Hotspur katika
Anfield.
Houllier alifurahia mafanikio aliyopata kwa
kushinda mataji 4 muhimu katika misimu mitano
kama meneja wa Liverpool.
Mechi alifunza: 307
Michezo aliyoshinda: 160
Michezo aliyoshindwa: 74
Michezo aliyotoka sare: 73
Kiwango cha ushindi: 52.12%

Mataji aliyoshinda:
FA Cup (1): 2000–01
League Cup (2): 2000–01, 2002–03
FA Community Shield (1): 2001
UEFA Cup (1): 2000–01
UEFA Super Cup (1): 2001

8. Rafael Benitez ( Liverpool and
Chelsea )
Mhispania alikuwa katika Liverpool tangu mwaka 2004 hadi 2010 ambapo alishinda mataji mawili
muhimu likiwemo la Ligi ya Mabingwa baada ya kushinda AC Milan kwa mikwaju ya penalti.
Alirudi tena katika England kama meneja wa Chelsea mnamo 2012, na kusaidia klabu kushinda
Kombe la Europa League.
Mechi alizofunza: 350 (Liverpool)
Michezo aliyoshinda: 196
Michezo aliyoshindwa: 79
Michezo aliyotoka sare: 75
Kiwango cha ushindi: 56%

Mataji aliyoshinda:
FA Cup: 2005–06
FA Community Shield: 2006
UEFA Champions League: 2004–05
UEFA Super Cup: 2005

7. Carlo Ancelotti( Chelsea )
Mwitaliano mwenye uzoefu katika kazi ya ukufunzi alichukua Chelsea kwa muda kumrithi meneja Guus Hiddink mwaka 2009. Baada ya
miezi miwili tu katika West London, Ancelotti aliinua kombe la Community Shield baada ya
kumpiga Sir Alex Furguson wa Manchester United kwa mikwaju ya penalti, baada ya kumaliza dakika za kawaida kwa sare ya 2-2.
Pia aliongoza klabu ya Stamford Bridge kwa ushindi wa Ligi Kuu ya England na Kombe la FA
katika msimu wake wa kwanza katika klabu hiyo.

Michezo aliyofunza: 109
Mechi alizoshinda: 67
Mechi alizoshindwa: 22
Michezo aliyotoka sare: 20
Kiwango cha ushindi: 61.47%
Mataji aliyoshinda:
Premier League: 2009–10
FA Cup: 2009–10
FA Community Shield: 2009

6. Kenny Dalglish (Blackburn
Rovers, Liverpool and Newcastle
United )
Raia wa Scotland alifanya kazi ya ukufunzi katika
klabu tatu tofauti, awamu mbili katika Liverpool,
miaka minne katika Blackburn Rovers tangu 1991
hadi 1995 na kumrithi Kevin Keegan katika
Newcastle mnamo 1997.
Kenny Dalglish aliongoza Blackburn Rovers
kwenye taji la Ligi Kuu ya England mnamo
1994/95, na kusaidia Newcastle United kumaliza
msimu ikiwa kwenye nafasi ya pili mnamo
1996/97. Lakini hakufanikiwa katika awamu yake
ya pili katika Liverpool.

5. Manuel Pellegrini ( Manchester
City )
Raia wa Chile alitangazwa kama meneja wa
Manchester City mnamo 2013 baada ya Roberto
Mancini kuondoka. Manuel Pellegrini alipata
kuwa kocha wa kwanza kutoka nje ya Ulaya
aliyeshinda Ligi Kuu ya England katika msimu wa
kwanza katika Etihad Stadium.
Mechi alizofunza: 112
Mechi alizoshinda: 73
Mechi alizoshindwa: 24
Michezo aliyotoka sare: 15
Kiwango cha ushindi: 65.18%
Mataji aliyoshinda:
Premier League (1): 2013–14
Football League Cup (1): 2013–14

4. Roberto Mancini ( Manchester
City )
Kocha Mwitaliano alikuja kumrithi Mark Hughes
katika Manchester City tangu 2009 hadi 2013.
Katika msimu wake wa kwanza, Mancini
aliisaidia City kumaliza msimu katika nafasi ya
tano, nafasi nzuri kwa mara ya kwanza katika
miaka 44.
Alishinda pia FA Cup na FA Community Shield
kwa Manchester City wakati wa awamu yake
katika Ligi Kuu ya England.
Mechi alizofunza: 119
Mechi alizoshinda: 113
Mechi alizoshindwa: 40
Michezo aliyotoka sare: 38
Kiwango cha ushindi: 59.16%
Mataji aliyoshinda:
Premier League: 2011–12
FA Cup: 2010–11
FA Community Shield: 2012

3. Arsene Wenger ( Arsenal)
Kocha Mfaransa aliwasili katika
Arsenal mnamo 1995, lakini tangu wakati huo
klabu Kasikazini mwa London haijashindwa
kufuzu kwa Ligi ya Mabingwa.
Mechi alizofunza: 1,071
Mechi alizoshinda: 616
Mechi alizoshindwa: 205
Michezo aliyotoka sare: 250
Kiwango cha ushindi: 57.52
Mataji aliyoshinda:
Premier League (3): 1997–98, 2001–02,
2003–04
FA Cup (6): 1997–98, 2001–02, 2002–03,
2004–05, 2013–14, 2014–15
FA Community Shield (6): 1998, 1999, 2002,
2004, 2014, 2015

2. José Mourinho (Chelsea)
Kocha Mreno ni mmoja wa mameneja wachache
walioweza kuchinda vikombe vitatu vya Ligi Kuu
ya England katika misimu 5 ya awamu mbili,
huchukuliwa kama mmoja wa mameneja bora wa
sasa katika ulimwengu wa soka, alishinda mataji
ya ligi katika nchi nne tofauti.
Kiwango cha ushindi: 70%
Mataji aliyoshinda:
Premier League(3): 2004–05, 2005–06, 2014–15
FA Cup(1): 2006–07
Football League Cup(3): 2004–05, 2006–07,
2014–15
FA Community Shield(1): 2005

1. Sir Alex Furguson ( Manchester
United )
Mskoti mwenye historia ndefu tena ya ajabu
katika ulimwengu wa soka, alidumu miaka 27
katika Manchester United kati ya 1986 na 2013,
aliandika rekodi ya kushinda Ligi Kuu ya England
mara 13 vile vile na mataji mengine ya Ulaya na
vikombe kadhaa vya England.
Ferguson, aliyestaafu kutoka soka mnamo 2013,
ndiye kocha pekee aliyewahi kushinda mataji 3
ya Ligi Kuu ya England kwa mfululizo. Alivifanya
kati ya 1998/99 na 2000/01, alivifanya tena kati
ya 2006/07 na 2008/09.
Mechi alizofunza: 1500
Mechi alizoshinda: 895
Mechi alizoshindwa: 267
Michezo aliyetoka sare: 338
Kiwango cha ushindi: 59.67
Mataji aliyoshinda:
Premier League (13): 1992–93, 1993–94, 1995–
96, 1996–97, 1998–99, 1999–2000, 2000–01,
2002–03, 2006–07, 2007–08, 2008–09, 2010–
11, 2012–13
FA Cup (5): 1989–90, 1993–94, 1995–96, 1998–
99, 2003–04
League Cup (4): 1991–92, 2005–06, 2008–09,
2009–10
FA Charity/Community Shield (10): 1990
(shared), 1993, 1994, 1996, 1997, 2003, 2007,
2008, 2010, 2011
UEFA Champions League (2): 1998–99, 2007–08
UEFA Cup Winners' Cup (1): 1990–91
UEFA Super Cup (1): 1991
Intercontinental Cup (1): 1999
FIFA Club World Cup (1): 2008