SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

May 18, 2016

SIDO FC YATOKA SARE DHIDI YA WAKAANGA SUMU KUBOTA NA ZFC ZAFUNGIWA

Na Haji balou
Mchezo kati ya Sido fc dhidi ya Wakaanga sumu umemalizika katika uwanja wa shule ya msingi muungano kwa sare ya goli 2-2.

Katika kipindi cha kwanza magoli ya Sido fc walifungwa namo dakika ya 7 na 15 yote yakipachikwa na Haikosi Mpwate na goli la Wakaanga Sumu likufungwa na  Bocho Shabani dakika ya 24.

Katika kupindi cha pili Wakaanga Sumu walisawazisha goli dakika ya 70 goli lililofungwa na Stamili Abduli
Mpaka dakika 90 zinakamilika matokeo yalikuwa Wakaanga sumu 2-2 Sido fc.

Nimezungumza na kamisaa wa mashindano ya ligi Shamte Mohamedi Shamte kuzungumzia sakata la mechi mbili za juzi kati ya Kubota fc Vs Kubota fc na Jana Z fc Vs Kigamboni fc kutokumalizika uongozi uliamua haya.

Timu zote ambazo zimeanzisha fujo katika mechi ya Jana Na juzii zimefungiwa katika mashindano hayo ya Kombe la mbuzi timu hizo ni Vijuso fc Na Zfc.

ORODHA YA TOP 10 WAFUNGAJI BORA ULAYA MESSI CHALIII

Na Haji balou
Luis Suarez (29) kwa mara ya kwanza alipata tuzo hiyo mwaka 2014 baada ya kufungana magoli na
Cristiano Ronaldo wakati huo akiwa Liverpool akifunga magoli 31 na kuwa mfungaji bora pia wa EPL.

Suarez amekuwa ni mchezaji wa kwanza La Liga mbali ya Messi na Ronaldo kushinda tuzo ya ufungaji bora tangu mwaka 2009.

Ukiwa msimu wa 2015-15 ukielekea ukingoni huku ukiwa umeisha kwa baadhi ya ligi, hii ndiyo orodha ya wafungaji 10 bora wa Ulaya msimu
huu:

CANNAVARO AMEFUNGUKA KUHUSU YEYE KUCHEZA TAIFA STARS KAMA ATAITWA NA MKWASA

Na Haji balou
Baada ya headlines za muda mrefu kuhusu aliyekuwa nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania Nadir Haroub Cannavaro kutangaza kustaafu kuchezea timu ya taifa ya Tanzania
kutokana na kuvuliwa unahodha bila kupewa taarifa rasmi, tuliwahi kusikia kocha wa Taifa Stars Boniface Mkwasa akisema kuwa bado Cannavaro yupo katika mipango yake.

Cannavaro amefunguka haya kuhusu yeye kucheza Taifa Stars kama kocha Mkwasa akimuita katika kikosi cha Taifa Stars kitakachocheza na Kenya May 29 “Kwanza ieleweke sina tatizo na kocha Mkwasa hata kidogo ni kocha ambaye napenda kufanya nae kazai
akiniita nitamtafuta tutakaa chini kushauriana kiutu uzima halafu nitamwambia mimi naomba tu kwa
sasa niendelee kupumzika kuchezea Stars”