SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Jan 22, 2016

KUMBE KIPRE KWAO ANAJULIKANA NA MAJIRANI TU

Unaweza kudhani ni utani, lakini ukweli ni
kwamba kati ya Waivory Coast
wanaocheza soka hapa nchini ni Pascal
Wawa (Azam FC) na Vincent Angbani
(Simba) wanaojulikana kuwa wanacheza
soka Tanzania, lakini upande wa
mwenzao fowadi wa Azam, Kipre
Tchetche kuna kitu ambacho
kinashangaza kidogo.

Kwa hapa nchini Kipre ni staa mkubwa
tangu mwaka 2011 alipojiunga na timu
hiyo na ndiyo maana ndiye straika
anayelipwa fedha ndefu zaidi nchini
akipokea dola 12,000 (Sh milioni 24) kwa
mwezi.

Angbani amesema kuwa utapotea njia
iwapo utafika Ivory Coast na kuulizia kina
Tchetche kwani hawajulikani, zaidi ya
umaarufu wao kuishia kwa majirani zao
tu.
“Mara ya kwanza nilishangaa sana kukuta
Kipre ni staa kiasi hiki hapa Bongo, ujue
kwetu tofauti na majirani hakuna anayejua
kuwa anacheza soka huku, wao wanamjua
Wawa na mimi,” alisema kipa huyo.
Akifafanua zaidi alisema umaarufu wake
na Wawa ni kutokana na kuwahi
kuichezea timu ya taifa ya vijana ya nchi
yao.
SOURCE: CHAMPIONI