SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Apr 11, 2016

FARID KUWAKOSA ESPERANCE MECHI YA MARUDIO ANAENDA ULAYA KUTAFUTA ULAJI

Na Haji balou
KLABU ya Azam FC itamkosa kiungo
Farid Mussa Malik (pichani kushoto)
katika wa mchezo wa marudiano
hatua ya 16 Bora Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Esperance nchini  Tunis wiki ijayo.

Baada ya kufunga bao la kusawazisha katika ushindi wa 2-1 kwenye mchezo wa kwanza jana Uwanja wa Azam Complex, Chamazi,   Farid sasa anajiandaa kwa safari ya majaribio Ulaya.

Bado wakala wa Farid hajaweka wazi basi anampeleka wapi kijana huyo, lakini inaelezwa atampeleka au
Ubelgiji, Scotland au Hispania ambako kote kuna timu za kumjaribu.

MANARA APATA AJALI

Na Haji balou
Mkuu wa Kitengo cha Habari na
Mawasiliano cha Simba, Haji Manara
amepata ajali mbaya.

Manara amepata ajali baada ya
kuchomoka tokea ndani ya Bajaj na
kuanguka barabarani.
Kuanguka huko kumesababisha Manara kupata majeraha sehemu za mkononi na usoni hukua kisema amenusurika kifo kutokana na ajali hiyo.

Manara ameelezea tukio hilo:
“Nilikuwa nakwenda kumuona shangazi yangu, nikaamua kuacha gari nichukue Bajaj. Sasa tukio hilo limetokea hivi; Bajaj ilipiga tuta wakati nikiwa sijashika, ndiyo nikachomoka.

“Hakika nimeumia na nina maumivu
makubwa sana, lakini namshukuru Mungu kwa kuwa ilikuwa ni ajali mbaya sana hasa kama kungekuwa na gari nyuma.”

HARAKATI ZA SOKA  INATOA POLE KWA MANARA NA KUMUOMBEA APATE NAFUU MAPEMA NA KUPONA KABISA.