SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Mar 8, 2015

MANCHESTER UNITED KUMUUZA DI MARIA

Di Maria
Di Maria hajaonyesha umahiri wake tangu aliposajiliwa katika kilabu ya Manchester united kutoka Real Madrid na inaaminika kwamba yeye na mkewe hawajazoea maisha ya Manchester baada ya jaribio la wizi katika nyumba yao.
Wiki iliopita raia huyo wa Argentina ,mkewe Jorgelina Cardoso na mwanawe wa mwaka mmoja wamehamia katika nyumba ya aliyekuwa mchezaji wa Manchester United Phil Nevile iliopo ghorofa ya 45.
Wamekodisha nyumba hiyo kwa kuwa Di Maria ana mpango m'badala wa maisha yake swala ambalo kilabu ya Manchester United inalifahamu.
Gareth Bale
Hatua hiyo inadaiwa kushinikiza harakati za kilabu hiyo kutaka kumsajili mchezaji wa Real Madrid Gareth Bale.
Ijapokuwa Bale amekuwa akisema kuwa hataki kuondoka katika kilabu ya Real Madrid ili kurudi katika ligi ya Uingereza,United inahisi kwamba inaweza kum'bembeleza ili kubadilisha msimamo wake iwapo watakubaliana na mabingwa hao wa Ulaya.

OKWI APELEKA SHEREHE MSIMBAZI

Mshambuliaji  wa Simba Emmanuel Okwi ameibuka shujaa katika mchezo wa leo baada ya kuisaidia timu yake kuibuka na ushindi mwembamba wa goli 1-0 dhidi ya Yanga jioni hii. Okwi alifunga goli hilo dakika ya 52 baada ya kumchungulia kipa wa Yanga Barthez aliye toka langoni mwake.Hawa ni baadhi ya mashabiki waliojitokeza katika mchezo wa leo. 

HAWA NDIO WACHEZAJI AMBAO UMRI WAO UNAFANANA

PicMonkey-Collage1111111111Na Amplifaya Amplifaya
Mara nyingi binadamu kama viumbe hai siku zote huwa tunapenda kuangalia muonekano wa mtu kiujumla na kukadiria miaka ya mtu husika kuwa huyu atakuwa na umri huu,  wengi huangalia sura au ukomavu wa mwili halikadhalika umbo la mtu.
Leo nimekuletea wachezaji ambao huwezi ukadhania kabisa kama umri wao upo sawa mtu wangu na kumekuwa na malalamiko ya wengi kuwa walidanganya umri na wengi hawaamini miaka yao kama ipo sahihi.
1. Diego Costa na Nzuri Sahn (26 miaka)
Mshambuliaji ambaye yupo katika kiwango cha upachikaji wa mabao kwa Chelsea hivi sasa Diego Costa wengi wa watu hawaamini kabisa umri wake alionao sababu ya muonekano wake kiujumla hasa muonekano wa sura yake ambayo inaobekana kuwa ni ya kiutu uzima sana. Diego Costa alizaliwa mwaka 1989 huko Brazil na hadi sasa ana miaka 26.
Achilia mbali mshambuliaji huyo tunaye mwingine ambaye ni kiungo kutoka Borussia Dortmund Nzuri Sahn naye ana miaka 26 na alizaliwa mwaka mmoja sawa na Diego Costa wakiwa wote wana miaka 26.
2. Fernando Torres na Arjen Robben (30 miaka)PicMonkey-Collage1112
Mshambuliaji aliyekuwa katika kiwango mathubuti na cha hatari zaidi Fernando Torres wakati huo akiwa katika majogoo wa Liverpool na baadae kutimkia Chelsea kisha kurejea tena katika timu yake ya mwanzo Athletico Madrid alizaliwa mnamo mwaka 1985.
Umri huo hakuna tofauti na mshambuliaji mwingine ambaye amekuwa katika kiwango kizuri sana akiwa na Club ya Bayern Munich kwasasa Arjen Robben, amezaliwa pia mwaka 1985 ila jinsi muonekano wake ulivyo hauwezi ukaamini kirahisi kama ana miaka hiyo 30 maana wengi wa mashabiki na wachezaji wenzie wanadhania anaweza akawa anafikisha miaka 40 na kuendelea ila mwisho wa siku ukweli utabakia palepale ana miaka 30 hadi sasa.

PICHA: ALI KIBA ALIVYO PAGAWISHA MASHABIKI WAKE ARUSHA #CHEKETOUR JANA

9kbbbbUsiku wa March 07 ilikua ni zamu ya mkoa waArusha nao kufikiwa na ile tour ya Ali Kiba inayoitwa Chekecha Cheke tour,hii ilikua ndani ya viunga vya Triple A,kama ilivyokuwa kwa Moshi Ali Kiba pia usiku huo.
Leo March 08 Ali Kiba ataimalizia kanda ya kaskazini kwa show kwenye mpaka Tanzania na Kenya sehemu inaitwa Namanga,hizi ni baadhi ya picha.
3kbbbb
2kbbbb
1kbbbb
8kbbbb
6kbbbb
5kbbbb
10kbbbb
12kbbbb

32kbbbb
31kbbbb
30kbbbb
29kbbbb
28kbbbb
27kbbbb
26kbbbb
25kbbbb
24kbbbb
21kbbbb
22kbbbb
23kbbbb
20kbbbb
19kbbbb
18kbbbb
17kbbbb
16kbbbb
15kbbbb
14kbbbb
13kbbbb

HIZI NI KURASA ZA MWANZO NA ZA MWISHO MAGAZETI YA MICHEZO LEO MARCH 8



.
.
.
.

TEGETE: TUTAIFUNGA SIMBA LEO

???????????????????????????????Na Baraka Mbolembole, Dar es Salaam
Kuelekea mchezo wa mahasimu wa kandanda nchini Simba SC v Yanga SC kesho Jumapili katika uwanja wa Taifa, Dar es Salaam mshambulizi aliyefunga mabao matano katika michezo iliyopita Jerson Tegete ameuambia  mtandao huu kuwa mechi hiyo itakuwa ngumu kwa kuwa kila timu inahitaji kushinda ili kujiweka katika nafasi nzuri katika msimamo wa ligi kuu Tanzania Bara.
“ Itakuwa ni mechi ngumu ambayo kila timu inahitaji kushinda, kwa upande wetu ( Yanga) tunahitaji ushindi ili kuelekea katika njia sahihi ya ubingwa, lakini kwa upande mwingine ni mchezo huu ni sehemu ya sisi kujiandaa na mchezo wa kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Platinum ya Zimbabwe. Simba pia watahitaji kushinda ili kusogea juu ya msimamo lakini naamini Yanga tutashinda´anasema Tegete.
Yanga ndiyo vinara wa ligi kuu hadi sasa, wakiwa na alama 31 watahitaji kuishinda Simba ili kuwazidi mahasimu wao hao kwa alama 11. Katika michezo minne iliyopita timu hizo zimetoka  sare huku Yanga ikiwa haijafunga goli lolote katika michezo miwili mfululizo dhidi ya Simba ( ukiwemo mchezo wa Nani Mtani Jembe-2). Tegete ambaye amepoteza nafasi yake katika kikosi cha kwanza cha Yanga cha Yanga ana imani hali hiyo itatoweka mara baada ya kumalizika kwa dakika 90.
“ Naamini kila kitu kitakuwa sawa, tutafunga safari hii, kikubwa tunaenda uwanjani ili kufunga magoli na kuisaidia timu yetu kushinda. Kutokufunga huwa ni hali ya kawaida, hutokea tu lakini tumejipanga kushinda. Niko fiti kama nitapata nafasi nitacheza. Yanga hatuna hofu kuhusu game hiyo, tuko vizuri hivyo ushindi ni hitaji letu. Natamani kucheza kwa mara nyingine katika pambano la mahasimu hao” anamaliza kusema Tegete wakati alipofanya mahojiano na mwandishi wa habari hii.

ALICHOSEMA JULIO BAADA YA JANA KULAZIMISHWA SARE NYUMBANI


kagera sugarNa. Richard Bakana
Kocha msaidizi wa klabu ya Coastal Union, kutoka Tanga, Jamhuri Kihwero ‘Julio’ ameangushia zingo la lawama safu yake ulinzi na kusema kuwa wamecheza kipuuzi kitu kilichopelekea kugawana pointi moja moja na Kagera Sugar kwenye mchezo wa ligi kuu ya Tanzamia bara uliomalizika kwa sare ya 2-2 Mkwakwani.
Akizugumza na Shaffihdauda.com baada ya mchezo huo,  alisema kuwa tayari mchezo huo walikuwa wameuweza, lakini kutokana na makosa yaliyofanywa na mabeki, Kagera Sugar waliweza kusawazisha licha ya Coastal Union, kuongoza kwa bao moja  hadi dakika 45 za mwanzo zinamalizika, kufatia kazi safi ya Seleman Kibuta aliyemalizia mpira uliokuwa ukizagaa katika lango la Kagera ikiwa ni dakika ya 6 ya mchezo.
“Mimi nasema hapa hakuna swala la Ufundi kwasababu wamepoteza umakini, Mchezo tulikuwa tumeshinda tayari, zilikuwa zimebaki dakika kama saba wameruhusu goli la kipuuzi ambalo kila mtu kwa kweli limemuuzi, Na hii ni kukusekana kwa umakini kwa sababu Kagera hawakuweza kukata tamaa, wameweza kushambulia wakitaka kurudisha na wamewez, Kwahiyo ni uzembe wa mabeki wetu, Mara ya kwanza walikuwa wanalalamika kuwa hawafungi kwahiyo kama wanafunga basi mabeki ndio watakuwa na matatizo, Tutalifanyia kazi ili kuona kwanini wanaruhusu magoli ya kizembe” Amesema Julio ambaye ni Kocha mkuu wa Mwadui FC ambayo imepanda ligi kuu msimu huu lakini Costal Union akifundisha kwa muda.
Baada ya Coastal kufanikiwa kuongoza kwa dakika 45 za mwanzo, Kagera walirudi katika Uwanja wa Mkwakwani Tanga wakiwa na presha kubwa wakisaka bao ndipo Mshambuliaji Atupele Green akaisawazishia timu yake bao akiunganisha kwa kichwa krosi safi kutoka kwa Salum Kanoni na kumuacha mlindamlango wa Coastal Union Shaaban Kado akiwa hana cha kufanya ikiwa ni dakika ya 52 ya mchezo.
Katika Dakika ya 60, mwamuzi wa mchezo huo kutoka Mtwara, David Paul, aliizawadia Coastal Union, penati ambayo ilizamishwa kambani na Rama Salum, Raia wa Kenya, baada ya Abuu Mtilo kuunawa mpira ndani ya chumba cha kupigia penati, na kufanya Wagosi hao wa kaya kufikisha bao 2-1.
Pongezi ziende kwa Rashid Mandawa aliyeisawazishia Kagera Sugar bao 2 na kufanya kibao kiwe 2-2 ikiwa ni dakika ya 84 akitumia makosa wa mabeki wa Coastal Union ambao walishindwa kuosha mbele mpira uliokuwa unazagaa katika lango lao.
Hata hivyo hadi kipenga cha mwisho kinapigwa kuashiria mtanange huo kumalizika timu hizo zikigawana pointi moja moja kwa kutoa sare ya 2-2, Wenyeji wa mchezo huo Coastal Union walimaliza wakiwa Pungufu kufatia mchezaji Othuman Tamimu kuzawadiwa kadi Nyekundu katika dakika ya 73 kwa kosa la kuchelewesha mpira ambapo tayari awali alikuwa na kadi ya njano.

REAL YAFA 1-0 SAN MAMES, BARCA YAWEZA PANDA KILELENI LEO LA LIGA IKIICHAPA VALLECANO

TIMU ya Real Madrid imefungwa 1-0 na Athletic Bilbao Uwanja wa San Mames usiku huu na maana yake iwapo Barcelona itaifunga Rayo Vallecano kesho mchana itapanda kileleni mwa La Liga.
Gareth Bale aligongesha mwamba akiwa umbali wa mita 50 kabla ya Aritz Aduriz kufunga kwa kichwa dakika 26, bao tosha kabisa kuipa ushindi mwembamba Athletic.
Kikosi cha Athletic Bilbao kilikuwa: Iraizoz, Iraola, Balenziaga, Etxeita, Gurpegui, Benat, Mikel Rico/Toquero, dk91, De Marcos, Muniain/Susaeta dk64, Aduriz na Williams/Fernandez Hierro dk75).
Real Madrid: Casillas, Carvajal, Varane, Pepe, Marcelo, Illarramendi/Jese dk71, Isco, Kroos/Borges dk76, Ronaldo, Bale na Benzema/Hernandez dk80.
Karim Benzema (left) and Cristiano Ronaldo look on as the Bilbao team celebrate scoring in the first half
Karim Benzema (kushoto) na Cristiano Ronaldo wakiwa hawaamini macho yao huku wachezaji wa Bilbao wakishangilia bao lao