SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Jun 27, 2016

HAYA NDIO MAAMUZI MAGUMU ALIYOYAFANYA LIONEL MESSI

Na Haji balou
MAUMIVU ya moyo
yamemshinikiza Mwanasoka
Bora wa Dunia, Lionel Messi
kustaafu kuichezea timu
yake ya taifa ya Argentina
baada ya jana kufungwa
katika fainali ya tatu
mfululizo ya Copa America
ndani ya miaka mitatu.

Messi si mgonjwa wa moyo,
bali ameumizwa n a kitendo
cha kukosa penalti ya
kwanza Argentina ikifungwa
kwa penalti 4-2 katika
fainali ya Copa America
Centenario baada ya sare
ya 0-0 ndani ya dakika 120.

Messi ambaye alimwaga
machozi na kilio baada ya
mechi hiyo alizungumza na
Televisheni ya Argentina
baada ya mechi na
kufafanua uamuzi wake. "Ni
hivyo. Mimi baso na timu ya
taifa,"alisema.

"Si kwangu. Hii ni fainali ya
nne. Uamuzi umefanyika,
nafikiri hivyo. [kushinda]
ndicho ninachoitaka zaidi.
Sikuja. nafikiri ni hivyo.
Hivyo ndivyo ninavyojisikia
kwa sasa, ninachofikiria. ni
maumivu makubwa,".