SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Mar 1, 2015

ROONEY AWAPA RAHA MAN UNITED, APIGA ZOTE MBILI ‘SHETANI’ LIKIUA 2-0 OLD TRAFFORD

TIMU ya Manchester United imeifunga Sunderland mabao 2-0 katika mchezo wa Ligi Kuu ya England jioni ya leo Uwanja wa Old Trafford.
Ikiongozwa na washambuliaji Wayne Rooney na Radamel Falcao, timu hiyo ya Louis van Gaal ilicheza vizuri na kupata ushindi huo kwa mabao ya kipindi cha pili..
Refa Roger East alikuwa kituko pale alipomuonyesha kadi nyekundu Wes Brown badala ya John O'Shea aliyemuangusha kwenye eneo la hatari Radamel Falcao na kusababisha penalti.
Nahodha wa England, Rooney akaenda kuifungia bao la kwanza kwa penalty United dakika ya 66, kabla ya kufunga la pili kwa kichwa dakika ya 84 na sasa United inafikisha pointi 50 baada ya kucheza mechi 27. 
Kikosi cha Manchester United kilikuwa: De Gea, Valencia, Smalling, Evans, Rojo, Blind; Herrera, Young, Di Maria/Januzaj, Rooney/Mata na Falcao/Fellaini.
Sunderland: Pantilimon; Reveillere, van Aanholt, Brown, O’Shea, Cattermole, Larsson, Gomez, Johnson/Fletcher, Wickham/Fletcher na Defoe/Fletcher.

 Rooney (right) misses Manchester United's opening chance with header from Angel di Maria's corner

SUAREZ AENDELEZA MOTO WA MABAO BARCA IKIPIGA MTU 3-1 LA LIGA

TIMU ya Barcelona imeifunga Granada mabao 3-1 katika La Liga jioni ya leo na kupunguza pengo la pointi dhidi ya vinara Real Madrid hadi kubaki moja. 
Ivan Rakitic aliwafungia wageni bao la kuongoza dakika ya 26, kabla ya Luis Suarez kuongeza la pili dakika ya kwanza kipindi cha pili.
Fran Rica akaifungia bao la kufutia machozi Granada dakika tano baadaye kwa penalti baada ya Marc Bartra kumuangusha Lass Bangoura- kabla ya Lionel Messi kuifungia timu ya Luis Enrique bao la tatu zikiwa zimebaki dakika 20.
Granada: Oier; Nyom, Babin, Cala, Foulquier; Iturra, Rico, Marquez/Rochina dk67, Bangoura/Candeias dk79, Ibanez na Cordoba/Isaac 78.
Barcelona: Bravo; Alves, Bartra, Mathieu/Busquets dk75, Alba, Mascherano, Xavi/Rafinha dk65, Rakitic, Messi, Neymar na Suarez/Pedro dk79.
Suarez wheels away in celebration after doubling the lead for Luis Enrique's side minutes after half time on Saturday
Suarez akikimbia kushangilia baada ya kuifungia timu ya Luis Enrique leo
Suarez leaps for joy after scoring his fifth goal in his last seven games for Luis Enrique's side
 Suarez is congratulated by team-mate Lionel Messi after the Uruguay international scored his third goal in two games

COASTAL YAIPIGA 1-0 MGAMBO, MVUA YAVUNJA MECHI YA STAND UTD NA KAGERA KAMBARAGE

BAO pekee la Mganda Yayo Kato Lutimba limeipa ushindi wa 1-0 Coastal Union dhidi ya Mgambo JKT jioni ya leo Uwanja wa Mkwakwani, Tanga.
Mganda huyo alifunga bao hilo dakika ya 88 akimalizia pasi ya Suleima Kibuta, baada ya kuingia akitokea benchi dakika ya 56 kuchukua nafasi ya Ayoub Yahya. 
Ushindi huo katika mechi ya kwanza Coastal ikiwa chini ya kocha wa muda, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ unaifanya ifikishe pointi 22 mechi 17.

Mechi nyingine za Ligi Kuu leo, Mbeya City imelazimishwa sare ya 1-1 na Ruvu Shooting Uwanja wa Sokoine, wakati mchezo kati ya Stand United na Kagera Sugar ulisitishwa dakika ya 80 kutokana na mvua kubwa.
Hadi mchezo unasitishwa, Stand walikuwa wanaongoza 1-0 na sasa mechi hiyo itamaliziwa kwa dakika 10 kesho.

FITINA ZA MAREFA ZAITUPA NJE AZAM FC LIGI YA MABINGWA

AZAM FC imeaga mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika, baada ya kufungwa mabao 3-0 na El Merreikh ya Sudan katika mchezo wa marudiano wa Raundi ya Awali uliofanyika Uwanja wa Marreikh mjini Khartoum.
Marefa wa mchezo huo kutoka Zambia Wellington Kaoma aliyesaidiwa na Romeo Kasengele na Amos Nanga walionekana wazi kuiuma Azam FC katika mchezo huo.
Pamoja na kupewa penalti ambayo iliokolewa na kipa Aishi Manula, Merreikh ilimaliza dakika 45 za kwanza inaongoza 1-0.
Refa wa Zambia Wellington Kaoma leo ameimaliza Azam FC Sudan kwa kuibeba Merreikh

Kipindi cha pili marefa wa Zambia waliongeza mbeleko kwa Merreikh na ikafanikiwa kupata mabao mawili zaidi yaliyofungwa na Ahmed Abdallah dakika ya 85 na Alan Wanga dakika ya 90.
Azam FC inatolewa kwa jumla ya mabao 3-2 baada ya awali kushinda 2-0 katika mchezo wa kwanza nyumbani, Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam.
Kwa kujua mbinu walizopanga na marefa hao, Merreikh walizuia mchezo huyo usionyeshwe na Televisheni yoyote.