SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

May 27, 2015

HANS POPPE AMTOLEA UVIVU MENEJA WA MESSI, AMUAMBIA AWE MAKINI SANA

=

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe amemvulia uvivu meneja wa kiungo wao, Ramadhani Singano ‘Messi’ kwamba analazimika kuwa makini.

Hans Poppe amesema meneja huyo anapaswa kuwa makini kutokana na maneno aliyoyatoa kwamba mkataba wa mchezaji wake ‘umechezewa’.
“Kwa kweli anapaswa kuwa makini sana, maneno anayoyazungumza hayana ukweli na anapaswa awe na uhakika.
“Anaposema kuna ujanja umefanyika katika mkataba huo wakati uko TFF, maana yake TFF wanahusika kuufanyia ujanja.
“Tumegushi saini, tumegushi na dole gumba. Sidhani kama ni jambo zuri kuzungumza tu hayo mambo.
“Anapaswa kuwa makini, nasema hivi kumuasa lakini bado naweza kusema simtambui kwa kuwa sijui yeye Messi ana meneja na wala hajawahi kuutambulisha uongozi wa Simba,” alisema Hans Poppe.
Meneja huyo amekuwa akilalama kwamba mkataba wa Simba na Messi unapaswa kulazimika msimu huu lakini ulio TFF unaonyesha unamalizika mwakani yaani 2016.
Lakini ajabu Messi, ameshindwa kuonyesha nakala ya mkataba wake ambayo ingeweza kuonyesha kama kweli Simba wamekosea au la.

HARRY KANE ATOA MSIMAMO JUU YA KUSAJILIWA MAN UITED

harry-kane-tottenham-premier-league_3280053
Harry Kane:  aliifungia magoli 21 Tottenham  katika msimu wa 2014/2015 wa ligi kuu England.
Harry Kane amesisitiza kuwa ataendelea kuichezea  Tottenham baada ya tetesi kuenea kwamba Manchester United wanavutiwa naye.
Mchezaji huyo bora kijana wa mwaka wa PFA amekumbana na swali kuhusu hatima yake ya baadaye mara tu baada ya kuwasili Malaysia kuelekea mechi ya kirafiki ya Spurs dhidi Malaysia XI.
Nyota huyo mwenye miaka 21 ameweka wazi kuwa ana nia ya kuendelea kuichezea Spurs chini ya kocha Mauricio Pochettino ambaye alimnoa vizuri msimu uliopita na kufunga magoli 21 sambamba na kucheza mechi ya kwanza kwenye kikosi cha timu ya taifa ya England.