SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

May 4, 2015

KOPUNOVIC; NIMEMALIZA UBISHI, SIMBA NDIYO TIMU BORA TANZANIA, HAKUNA CHA AZAM WALA YANGA


REKODI YA GORAN KOPUNOVIC SIMBA SC

Simba SC 1-0 Mafunzo (Kombe la Mapinduzi)
Simba SC 1-0 JKU (Kombe la Mapinduzi)
Simba SC 4-0 Taifa Jang’ombe (Robo Fainali Kombe la Mapinduzi)
Simba SC 1-0  Polisi (Nusu Fainali Kombe la Mapinduzi)
Simba SC 0-0  Mtibwa Sugar (Simba ilishinda penalti 4-3 Fainali Kombe la Mapinduzi)
Simba SC 2-0  Ndanda FC (Ligi Kuu)
Simba SC 1-1 Azam FC (Ligi Kuu)
Simba SC 1-2 Mbeya City (Ligi Kuu Taifa)
Simba SC 2-1 JKT Ruvu (Ligi Kuu)
Simba SC 0-0 Coastal Union (Ligi Kuu)
Simba SC 2-0 Polisi Moro (Ligi Kuu) 
Simba SC 0-1 Stand United (Ligi Kuu)
Simba SC 5-0 Prisons (Ligi Kuu)
Simba SC 1-0 Yanga SC (Ligi Kuu)
Simba SC 1-0 Mtibwa Sugar (Ligi Kuu)
Simba SC 0-2 Mgambo Shooting (Ligi Kuu)
Simba SC 3-0 Ruvu Shooting (Ligi Kuu)
Simba SC 2-1 Kagera Sugar (Ligi Kuu)
Simba SC 3-0 Toto Africans (Kirafiki Mwanza)
Simba SC 0-2 Mbeya City (Ligi Kuu)
Simba SC 4-0 Mgambo JKT (Ligi Kuu)
Simba SC 3-0 Ndanda FC (Ligi Kuu)
Simba SC 2-1 Azam FC (Ligi Kuu) 
Na Princess Asia, DAR ES SALAAM
KOCHA wa Simba SC, Goran Koponovic amesema kwamba amemaliza ubishi juu ya timu ipi bora kati yao, Yanga na Azam FC.
Kauli ya Mserbia huyo inafuatia jana kuwafunga waliokuwa mabingwa watetezi, Azam FC mabao 2-1 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Na kwa kuwa tayari aliwafunga mabingwa wapya, Yanga SC 1-0 katika Ligi Kuu- Kopunovic amesema hiyo inatosha Simba SC kuwa bora zaidi ya wapinzani wake hao.
Alisema licha ya kutotwaa ubingwa, huku akiiombea mabaya Azam ipoteze mechi zake mbili zilizobaki, lakini anajivunia kikosi bora kuliko timu zote za Ligi Kuu Bara. 
“Leo nimemaliza ubishi wa kipi kikosi bora, nimemaliza leo kwamba timu yangu ni bora, hivyo Jumatano nikiwa katika mazoezi akili yangu itakuwa Taifa kwa kuiombea Azam ipoteze mchezo (dhidi ya Yanga) huo ili ipoteze mwelekeo wa nafasi ya pili,'' alisema Goran.
Kocha huyo amesema anaipongeza Yanga kwa kutwaa ubingwa na pia akawapa pole kwa kutolewa katika Kombe la Shirikisho kufuatia kufungwa 1-0 juzi na Etoile du Sahel nchini Tunisia.
Kufuatia ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Azam FC jana Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Simba SC imefikisha pointi 44 baada ya kucheza mechi 25. Azam inabaki na pointi zake 45 za mechi 24 katika nafasi ya pili, wakati tayari Yanga SC imejihakikishia ubingwa baada ya kufikisha pointi 55 za mechi 24.
Simba SC sasa inaiombea dua mbaya Azam FC ipoteze mechi zake zote mbili zilizobaki dhidi ya Yanga na Mgambo- na wenyewe (Simba SC) washinde mechi yao ya mwisho, ili kumaliza katika nafasi ya pili waweze kucheza Kombe la Shirikisho Afrika mwakani.
Tangu atue Msimbazi Januari mwaka huu, Kopunovic ameiongoza Simba SC katika mechi 23 kati ya hizo, imeshinda 17, imefungwa tatu na sare tatu.

Jumatatu MAY 4 2015 kurasa za #Magazeti zimeamka na hizi

DSC02127 DSC02128 DSC02129 DSC02130 DSC02131 DSC02132 DSC02133 DSC02134

PAC MAN: ILIBAKI KIDOGO TU NIJITOE PAMBANO NA MAYWEATHER

BONDIA Manny Pacquiao amesema kwamba alikaribia kujitoa katika pambano aliloliingiza dola za KImarekani Milioni 180 leo dhidi ya Floyd Mayweather, ambalo amepoteza kwa pointi.
PacMan amesema kwamba aliumia bega mazoezini na Kamisheni ya Michezo Nevada ilimkatalia ombi la kusogeza mbele pambano hilo la utajiri mkubwa zaidi kihistoria duniani.
Pacquiao aliamua kupanda ulingoni leo licha ya Kamisheni hiyo kukataa hata la kuchoma sindano ya ganzi katika chumba chake cha kuvalia kuzuia maumivu.
Manny Pacquiao revealed he had suffered an injury three weeks before the fight took place

Kamisheni pia ilikanusha kuwa na taarifa za mapema juu ya maumivu ya bondia huyo wa Ufilipino. 
Pacquiao amesema: "Maumivu yalirudi kwemnye raundi ya tatu na baada ya hapo sikuweza kutumia vizuri mkono wangu wa kulia,".
Kocha wake, Freddie Roach amesema: "Maumivu ya zamani ya bega hilo yalirudi kiasi cha wiki mbili na nusu kabla ya pambano. Yalivuruga mazoezi. Alifanyiwa vipimo (MRI), akapewa ruhusa ya matibabu, bega likaanza kupata nafuu siku hadi siku na tukaamua kupanda ulingoni,".
Mayweather addresses the media after taking his record to an unbeaten 48-0 against Pacquiao

Mayweather amejibu madai hayo ya mpinzani wake akisema; "Nilipata maumivu pia. Mikono yangu yote iliumia. Hizo ndiyo ngumi. Na kama angeshinda ningesema alikuwa bora katika usiku huo,".
Pacquiao amepoteza pambano kwa pointi mbele ya Maywether na hakupiga ngumi nyingi kama ilivyotarajiwa, ingawa mwenyewe awali alisema ni kwa sababu ya mpinzani wake kukimbia kimbia ulingoni.

TYSON: MAYWEATHER AMESHINDA KIHALALI

BINGWA wa zamani wa dunia uzito wa juu, Mike Tyson amemaliza ubishi kwa kusema Floyd Mayweather amemshinda kihalali Manny Pacquiao.
"Tumelisubiri kwa miaka mitano, nafikiri (Mayweather) ameshinda pambano, alimzidi ngumi Manny. Manny alikuwa ana mwanzo mzuri, lakini (Mayweather) akaimudu hiyo,"amesema Tyson.
"Alilimudu pambano, alikuwa ana nguvu (na) na amefanya kazi haswa," amesema.
"Ni zama zake, wakati wake. ni mtu babu kubwa sasa- hakuna mmoja anayeweza kusimama naye kwa wakati huu,"amesema. 
Former heavyweight world champion Mike Tyson at the MGM Grand on Saturday night to watch the fight

SAMATTA, ULIMWENGU ‘WAIPELEKA MBELE’ TP MAZEMBE LIGI YA MABINGWA

TANZANIA itaendelea kutajwa katika michuano ya Afrika licha ya timu zake zote kutolewa- kufuatia TP Mazembe kufuzu hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa jioni ya leo kwa ushindi wa jumla wa 4-3 dhidi ya Stade Malien.
Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) yenye washambuliaji wawili Watanzania, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu imeshinda mabao 2-1 leo Lubumbashi dhidi ya timu ya Mali. 
Mabao ya TP Mazembe yamefungwa na Jean Kasusula dakika ya 20 na Roger Claver Assale dakika ya 63.
Timu zote za Tanzania, KMKM, Polisi, Azam FC zimetolewa Raundi ya kwanza tu katika michuano ya Afrika.
Yanga SC ilijitutumua hadi raundi ya tatu kabla ya kutolewa jana na Etoile du Sahel ya Tunisia.