SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Apr 17, 2016

SIMBA CHALI KESSY AONESHWA NYEKUNDU

Na Haji balou
Leo April 17 uwanja wa Taifa
Dar es Salaam Simba wamekubali kipigo cha goli 1-0 kutoka kwa Toto Africans na kuendeleza rekodi yao ya kusumbuliwa na Toto kila mara
wanapokutana.
Simba kabla ya

MSIMAMO WA LIGI KUU TANZANIA BARA

Baada ya Jana Yanga kuibuka Na ushindi wa 1-0 dhidi ya Mtibwa sugar huu ndio msimamo wa ligi kuu ya Vpl.

PLUIJIM ATOA LAWAMA KWA WAANDISHI WA HABARI

 
Na Haji balou
Kocha mkuu wa Yanga amelalamika juu ya waandishi ambao wamekuwa wakiandika vitu ambavyo yeye hajazungumza kwasababu
vinamletea matatizo na waajiri wake.
Hans amesema hivyo baada ya gazeti moja kutoa habari ambayo inasababisha mazingira magumu, anasema yeye ni mwajiriwa hivyo
anatarati zake za kazi na badala yake amewaomba waandishi kuchukua na kufanyia kazi kile ambacho anakuwa amekizungumza
mwenyewe.
“Mimi huwa zizungumzi kuhusu kuhusu makocha, timu nyingine wala TFF, kuna gazeti linasema mimi nilienda TFF kujaribu kubadilisha
tarehe za baadhi ya mechi lakini kulikuwa hakuna uwezekano juu ya hilo kwahiyo nikawa nimekasirishwa na TFF na kuanza kuwashutumu
kwamba hawajui kufanya mambo yao, sijawahi kuzungumza kuhusu federation watu wanatakiwa
kujua hilo”, amesema Hans ambaye anaonekana kuchukizwa na habari hiyo.
Kuhusu mchezo wao wa kiporo dhidi ya Mtibwa Sugar ambao Yanga walishinda kwa bao 1-0 na kukwea hadi kileleni mwa ligi, Hans
amekimwagia sifa kikosi chake kuwa kimecheza vizuri kwenye mchezo huo licha ya kupoteza nafasi nyingi za kufunga magoli.
“Tulicheza vizuri sana kitu kimoja
kilichotuangusha ni kutotumia nafasi
tulizozipata, na wakati mechi inaelekea kumalizika kulikuwa na ‘tension’ kubwa kwa wachezaji wangu na hiyo ilisababishwa na kuwa na goli moja tu mkononi lakini kama unamagoli zaidi ya mawili unakuwa huna presha”.
“Tumecheza dhidi ya timu ngumu na tulilijua hilo kabla ndiyo maana mwanzoni tulianza na mfumo wa 3-5-2 lakini kwasababu tupo nyumbani na ni lazima tushinde mechi ndiyomaana tukamtoa beki mmoja nje na kuongeza mshambuliaji mwingine”.

SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1UGENINI

Na Haji balou
NYOTA ya Nahodha wa Tanzania,
Mbwana Samatta imeendelea
kung’ara Ulaya baada ya leo kuifungia tena klabu yake, KRC Genk katika ushindi wa 2-1 ugenini dhidi ya wenyeji SV Zulte-Waregem.

Katika mchezo huo wa Ligi Kuu ya
Ubelgiji uliofanyika Uwanja wa
Regenboogstadion mjini Waregem,
Samatta alifunga bao la kwanza
dakika ya saba tu kwa kichwa
akimalizia kona ya mkongwe wa umri wa miaka 25, Mbelgiji Thomas Buffel.

Beki wa Kongo mzaliwa wa Ufaransa, Marvin Baudry akajifunga katika harakati za kuokoa dakika ya 15 kuipatia Genk bao la pili, kabla ya
mshambuliaji Msenegali, M'Baye Leye kuifungia SV Zulte-Waregem bao la kufutia machozi kwa penalti dakika ya mwisho ya kipindi cha kwanza.

Hilo linakuwa bao la nne kwa Samatta katika mechi tisa alizocheza tangu ajiunge na Genk Januari mwaka huu akitokea TP Mazembe ya DRC.