SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Feb 27, 2015

MESSI WA MBEYA CITY AREJEA DIMBANI


Messi-Wall1-630x360
BAADA ya kuwa nje kwa majeruhi muda mrefu, kiungo mshambuliji  wa Mbeya City Fc, Alex Seth ‘Messi’ amerejea kikosini tayari kuendeleza mapambano katika kindumbwendumbwe cha ligi kuu ya soka Tanzania Bara.
Seth amekaririwa na Tovuti ya Mbeya City fc akisema kuwa anamshukuru Mungu kwa kupona majereha yaliyokuwa yanamsumbua kwa kipindi kirefu na kumfanya kuikosa ligi  kwa kipindi kirefu.
“Nashukuru nimepona,nilikosa ligi kwa kipindi kirefu mara ya mwisho nilicheza dhidi ya Tanzania Prison msimu uliopita,narudi kuongeza nguvu kwenye kikosi, kama timu tulikuwa na wikiendi mbaya baada ya kupoteza mchezo dhidi ya Yanga lakini jumamosi  hii  naimani itakuwa ni sehemu nyingine ya furaha  kwetu hasa  kwa kuongeza pointi tatu muhimu dhidi ya Ruvu Shooting” alisema.
Akiendelea zaidi Seth alisema, hivi sasa kwenye kikosi imani ya kila mchezaji ni kucheza kwa nguvu ili kutafuta matokeo kwenye mchezo ujao huku akiamini kuwa hilo linawezekana hasa ukizingatia morali iliyopo hivi sasa miongoni mwa nyota wa City bila kujali nini kilikuwepo juma lililopita.
“Naomba mashabiki wawe na timu yao, bado iko vizuri na kwa uwezo wa mwenyezi mungu naimani tutashinda jumamosi, tunajua walikosa furaha baada ya mchezo uliopita lakini huu ni wakati wao na waamini kwenye soka inawezekana kushinda mchezo unaofuata  hata kama ulipoteza mchezo uliopita” alimaliza.

AZAM WAZIPOTEZA FITINA ZA WASUDANI

 10403629_918481188192238_6973291696561800103_n
MABINGWA watetezi wa ligi kuu soka Tanzania bara na wawakilishi wa nchi katika michuano ya ligi ya mabingwa Afrika, Azam fc wanaendelea kujifua nchini Sudan kuelekea mechi ya marudiano dhidi ya wenyeji Al Merrick itayopigwa kesho jumamosi usiku uwanja wa Odmarman, mjini Khartoum.
Azam fc wataingia katika mechi ya kesho wakiwa na faida ya mabao 2-0 waliyovuna februari 15 mwaka huu uwanja wa Azam Complex, Dar es salaam.
Mabao hayo yalifungwa na Didier Kavumbagu na Nahodha John Raphael Bocco ‘Adebayor’.
 Licha ya kufanyiwa fitina za hapa na pale, kocha mkuu wa Azam, Mcameroon, Joseph Marius Omog ameendelea na programu yake ya mazoezi leo.
Azam wanahitaji sare ya aina yoyote ile au kufungwa si zaidi ya goli 1-0 ili kusonga mbele.

MCHEZAJI SERBIA ATISHIWA KUUAWA KWA BUNDUKI KISA KUKOSA PENALTI

MCHEZAJI wa klabu ya Ligi Kuu ya Serbia, Novi Pazar ametishiwa kupigwa bastola na mashabiki baada ya kukosa penalti, taarifa ya chama cha Umoja wa Wachezaji Duniani, FIFPro imesema jana.
Ikiliita tukio hilo kama sheria mpya katika soka ya Serbia, FIFPro imesema kwamba mchezaji wa Novi Pazar, Zarko Udovicic alipaisha mkwaju wake wa penalti juu ya lango dakika ya 85 Jumamosi iliyopita katika mchezo dhidi ya FK Rad.
Siku mbili baadaye, mashabiki kadhaa wenye hasira walivamia chumba cha kubadilishia nguo cha wachezaji na kwenda kumuonyeshea mtutu wa bunduki usoni Udovicic, imesema taarifa ya FIFPro. Baada ya hapo, mchezaji huyo ameondoka kwenye klabu hiyo.
Zarko Udovicic has left Serbian club Novi Pazar after  fans threatened him with a gun for missing a penalty
Zarko Udovicic ameondoka Novi Pazar ya Serbia baada ya kutishiwa mtutu wa bunduki kwa kukosa penalti

Mirko Poledica, Rais wa Chama cha Wachezaji wa Kulipwa Serbia, Nezavisnost, amesema hakuna aliyechukua hatua baada ya tukio hilo kati ya Chama cha Soka Serbia au bodi ya Ligi.
"Nchini Serbia, hakuna shabiki aliyewahi kuchunguzwa au kutiwa hatiani baada ya kuwafanyia fujo wachezaji. Ndiyo maana wachezaji wanaogopa. Kila siku wanaishi kwa matumaini ifike wakati wasiwe na mashaka ya kugongewa milango na kupigwa na mashabiki, au kuchomewa moto gari zao,".
FIFPro imesema; "Kama ilivyo kwa mfanyakazi yeyote kitaaluma, kila mchezaji anastahili kuwekewa mazingira salama ya kufanyia kazi. Ni juu ya mamlaka za soka kuweka mazingira hayo salama,".
Udovicic had missed a penalty for Novi Pazar against FK Rad two days before the incident
Udovicic alivyopaisha penalty ya Novi Pazar dhidi ya FK Rad kabla ya kutishiwa mtutu wa bunduki siku mbili baadaye

PLUIJM AWAPA UHAKIKA YANGA SC WANALING’OA JESHI LA BOTSWANA AFRIKA

Na Mwandishi Wetu, GABORONE
KOCHA Mkuu wa Yanga SC, Mholanzi Hans van der Pluijm amewatoa hofu wapenzi wa timu hiyo kuelekea mchezo wa leo dhidi ya BDX XI, akisema kwamba; “tiketi ya kusonga mbele ipo”.  
Yanga SC wanatarajiwa kuwa wageni wa timu hiyo ya Jeshi la Botswana katika mchezo wa marudiano, Raundi ya Awali Kombe la Shirikisho Afrika utakaofanyika Uwanja wa Lobetse kuanzia Saa 1:00 usiku kwa saa za huko na Saa 2:00 kwa saa za Afrika Mashariki.
Akizungumza na BIN ZUBEIRY jana mjini hapa katika mahojiano maalum kuelekea mchezo wa leo, Pluijm amesema kwamba vijana wake wako tayari kwa kazi nzuri leo. 
Hans van der Pluijm akiwa na Msaidizi wake, Charles Boniface Mkwasa

Kocha huyo ambaye jana asubuhi alifanya mazoezi na kikosi chake katika Uwanja wa Lobetse utakaotumika kwa mcheo huo wa leo, amesema wataingia na akili ya kutaka kuthibitisha ubora wa timu yao.
Pluijm amesema wameuona Uwanja wa mchezo na kwake hauna sababu ya kuifanya timu yake kukosa ushindi na akawaambia wachezaji wake kufanya kweli kwa kupata ushindi lengo likiwa kuthibitisha ubora wa timu yao.
Pluijm amesema wataingia katika mchezo huo kupigana kwa nguvu zao zote ili wapate ushindi mzuri na kusonga mbele.
"Tunataka kuthibitisha ubora wetu kuwa sisi ni Yanga, nimewaambia vijana watulie wacheze kama tulivyokubaliana, kama tutadumisha nidhamu ya mchezo, ushindi upo,"amesema Pluijm.
Yanga SC inahitaji hata sare leo ili kusonga mbele, baada ya awali kushinda mabao 2-0 katika mchezo wa kwanza Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. 

WAZIRI WA KIKWETE ATUA SUDAN KUIPA ULINZI AZAM FC


Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Vijana na Michezo, Alhaj Juma Nkamia (kushoto) akizungumza na wachezaji wa Azam  FC mazoezini Uwanja wa Jeshi mjini Khartoum, Sudan usiku wa jana. Anayezungumza naye kulia ni mshambuliaji Mrundi, Didier Kavumbangu. Azam FC watacheza na wenyeji El Merreikh kesho mchezo wa marudiano Raundi ya Awali Ligi ya Mabingwa Afrika. Mechi ya kwanza, Azam FC ilishinda 2-0 Dar es Salaam.
Wachezaji wa Azam FC wakifanya mazoezi mepesi Sudan jana
Kocha wa makipa, Iddi Abubakar kulia na vijana wake wakifanya dua
Wachezaji wa Azam FC wakiteremka kwenye basi wanalotumia mjini Khartoum ambalo wanajilipia wenyewe baada ya kukataa basi walilopewa na wenyeji wao

KURASA ZA MWANZO NA ZA MWISHO MAGAZETI YA MICHEZO LEO 27 FEB

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.

NTAMPATA WAPI YA DIAMOND YASHIKA NAMBA 1 UFARANSA


.
.
Kama wewe ni shabiki wa muziki wa Africa unaweza kuwa na hamu ya kufahamu ni single gani ambayo iko juu kwenye chati za muziki huu duniani…. kwa sababu kazi yangu ni kukusogezea zote muhimu, nakusogezea na hii kwamba video ya ‘Nitampata wapi’ ya Diamond Platnumz kupitia kituo cha TraceTV ya Ufaransa imeicheza video hiyo kama namba 1.
.
.
Mbali na video hiyo kuchezwa kama namba 1 kwenye kituo hicho cha Trace TV, Diamond Platnumz ana sababu nyingine ya kufurahi mafanikio ya kuwa msanii wa kwanza wa Tanzania kupitia video yake ‘Nitampata wapi’  kufikisha views milioni 2 tangu iwekwe Nov 20, 2014.
.
.
.
.
.
.

INTER MILAN NAYO YASONGA MBELE EUROPA LEAGUE

Van Dijk contests for the ball alongside Inter Milan striker Mauro Icardi in the Europa League game
Van Dijk wa Celtic akigombea mpira na mshambuliaji wa Inter Milan, Mauro Icardi katika mchezo wa Europa League usiku huu mjini Milan. Inter walishinda 1-0 ma kusonga mbele kwa ushindi wa jumla wa 4-3, baada ya sare ya 3-3 awali nchini Scotland.

MCHEZAJI WA CHELSEA AIADHIBU SPURS NA KUITUPA NJE ULAYA

Former Basle forward Salah was booked after taking his shirt off in celebration of his goal on Thursday
Mshambuliaji wa Chelsea, Mohammed Salah anayecheza kwa mkopo Fiorentina ya Italia, akishangilia baada ya kuifungia timu yake ya mkopo bao la pili katika ushindi wa 2-0 dhidi ya Totenham Hotspur usiku nchini Italia katika mchezo wa Europa League. Bao la kwanza la Fiorentina lilifungwa na mshambuliaji wa zamani wa Bayern Munich, Mario Gomez na hivyo wameitoa Spurs kwa jumla ya mabao 3-1, baada ya sare ya 1-1 katika mchezo wa kwanza.

LIVERPOOL YATUPWA NJE YA MICHUANO YA ULAYA

LIVERPOOL imetupwa nje ya michuano ya Europa League, baada ya kufungwa kwa penalti 5-4 na Besiktas kufuatia sare ya jula ya 1-1.
Tolgay Arslan alitokea benchi na kuifungia Besiktas bao dakika ya 72 Uwanja wa Ataturk, Istanbul nchini Uturuki akimalizia ‘pande’ la Demba Ba na kufanya sare ya jumla ya 1-1 baada ya Liverpool kushinda 1-0 katika mchezo wa kwanza England.
Ba angeweza kufunga bao la ushindi dakika ya  92, kama asingegongesha mwamba akiwa umbali wa mita sita.
Baada ya dakika 120, penalti za Besiktas zilifungwa na Ba, Lambert, Tore, Lallana na Kavlak, wakati zilifungwa na Can, Hutchinson, Allen na Arslan huku Lovren akikosa.
Kikosi cha Besiktas kilikuwa; Gonen, Opare, Franco, Uysal, Kurtulus, Hutchinson, Kavlak, Tore, Sosa/Arslan dk61, Sahan/Frei dk105 na Ba.
Liverpool: Mignolet, Toure, Lovren, Skrtel, Moreno, Can, Allen, Sterling, Ibe/Manquillo dk76, Sturridge/Lambert dk106 na Balotelli/Lallana dk82.
Liverpool failed to repeat their 2005 Champions League final heroics in Istanbul as they were dumped out of the Europa League by Besiktas
Wachezaji wa Liverpool wakisitika baada ya kutolewa Europa League na Besiktas, kulia Demba Ba akishangilia