Feb 6, 2015

MANYIKA JUNIOR AFUNGUKA KUHUSU BINTI WA MBUNGE ANAYESABABISHA ASHUKE KIWANGO

NIMAA..
Kipa wa Simba, Peter Manyika Jr ameingia kwenye shutuma nzito zinazosababisha kushuka kwa kiwango chake ambapo inadaiwa kuwa uhusiano wa kimapenzi na mrembo mmoja anayejulikana kwa jina la Nima ndiyo sababu.

Manyika Jr amekuwa akionekana sehemu mbalimbali akiwa na mrembo huyo ambaye inadaiwa ni mtoto wa mbunge, pia picha zao hutawala kwenye ukurasa wa Instagram, lakini baada ya kugundua zimeshasambaa kwa watu mbalimbali, mrembo huyo alizifuta picha hizo.
 
PETER MANYIKA...
Inaelezwa kuwa hali hiyo ya kushuka kiwango imewakera viongozi wengi wa Simba pamoja na baba wa mchezaji huyo Manyika Peter ambaye alimuweka chini mwanaye na kumkanya.
Akizungumza kuhusiana na hilo, kipa huyo mwenye umri wa miaka 19, alisema: “Huyo dada ni rafiki yangu wa kawaida na wala sina uhusiano naye wa kimapenzi.  Tatizo letu Watanzania tukiona jambo basi tunalikuza kupita kiasi.”
Kuhusu picha wakiwa pamoja alisema: “Kweli tulipiga picha lakini hiyo siyo sababu ya kusema kuwa ni mpenzi wangu.”
Alipoulizwa kuhusu kukanywa na baba yake juu ya jambo hilo, alisema: “Kweli baba aliniuliza, nilimueleza ukweli kuwa hakuna kitu kama hicho.”
Alipotafutwa baba mzazi wa kipa huyo, Manyika Peter ambaye alikuwa na haya ya kusema: “Sitaki mwanangu apotee, nilipata taarifa hizo na nikamuita na kuzungumza naye kwa kina lakini aliniambia kuwa yule ni rafiki yake, hata hivyo nikiwa kama mzazi nilimkanya na kumpa mwongozo wa nini anatakiwa kukifanya kufika mbali kisoka.
 
MANYIKA SR (KULIA)...
“Kama alidanganya kuwa hayupo na mwanamke huyo, hilo silijui kwa sababu hivi sasa siko naye nyumbani, muda mwingi yupo na timu yake ya Simba lakini nitalifuatilia suala hilo.”
SALEHJEMBE ilimtafuta  Nima ambaye inaelezwa ndiye aliyekuwa mrembo katika wimbo wa Mbagala wa msanii Nasibu Abdul ‘Diamond’, naye alifunguka: “Manyika siyo mpenzi wangu ila ni rafiki yangu, mimi najua ana mtu wake lakini siyo mimi, hiyo video niliyokuwa nimeiweka Instagram tulipiga tukiwa tunatokea mazoezi ya Simba na hata siku hiyo mchumba wa Manyika alikuwa anajua kuwa nipo naye.”

0 maoni:

Post a Comment