SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Jan 19, 2016

MAYANJA ATOA NENO KUHUSU MAKIPA SIMBA

Kocha Mkuu wa muda wa Simba, Jackson
Mayanja amewataka makipa Peter
Manyika na Vicent Agbani raia wa Ivory
Coast kuwa katika utimamu wa asilimia
mia kwa fitnesi.

Mayanja raia wa Uganda amewataka
makipa hao kuongeza mazoezi
kuhakikisha wanakuwa walinzi sahihi
katika kila dakika 90 za mechi.
“Kwa mchezaji wakati wote anatakiwa
kuwa fiti kwa asilimia mia, kipa ni mlinzi
namba moja. Akipitiwa yeye, maana yake
mmefungwa, hivyo anatakiwa kuwa fiti
kamilifu.

“Mchezaji anapokuwa timilifu kwa maana
ya kuwa fiti sana, basi uhakika wa
kufanya anachotaka iwe ni kwenye kuokoa
au kushambulia unakuwa juu sana. Hivyo
nimewasisitiza na wao wanalijua hilo,”
alisema.
MAYANJA

Kwa sasa Simba haina kocha wa makipa
baada ya Iddi Salim raia wa Kenya
kutupiwa virago na uongozi wa Simba na
tayari ameisharejea kwao Nairobi, Kenya