SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

May 27, 2016

WACHEZAJI AZAM FC WAPEWA MAPUMZIKO

WACHEZAJI wa Klabu Bingwa ya Afrika
Mashariki na Kati Azam FC, wamepewa
mapumziko ya wiki tano baada ya
kumaliza mechi ya mwisho ya msimu wa
2015/16 dhidi ya Yanga kwenye mchezo
wa fainali ya Kombe la Shirikisho (Azam
Sports Federation Cup) juzi jioni.
Azam FC inayodhaminiwa na Benki ya
NMB ambayo ni benki bora kabisa
iliyosambaa kila kona nchini, ilipoteza
mchezo huo wa fainali baada ya
kufungwa mabao 3-1.

Akizungumza na mtandao rasmi wa klabu
Na mtandao huu mara baada ya
mchezo huo Ofisa Mtendaji Mkuu wa
Azam FC, Saad Kawemba, alisema kuwa
msimu ndio umeisha kwa timu hiyo na
kilichobakia ni kujipanga kwa ajili ya
kupata matokeo mazuri msimu ujao.
“Tunamshukuru Mwenyezi Mungu
tumecheza mchezo wa fainali, ingawa
matokeo yalikuwa si mazuri haikuwa
malengo yetu, tulipanga kushinda lakini
lazima tukubali ni matokeo ya mpira,”
alisema.

Kawemba alisema wachezaji watamaliza
likizo hiyo Juni 30 mwaka huu na Julai
Mosi wataanza maandalizi ya msimu
mpya.
“Kwa hiyo tutafanya nini kwa msimu ujao,
tutamuongeza nani, tutamtoa nani hayo
tutazungumza baadaye lakini sasa hivi
tunawaomba washabiki wetu wawe
watulivu na tutaendelea kujipanga,”
alisema.

HAYA NDIO MASHINDANO MAPYA YANAYO DHAMINIWA NA AZAM TV

KAMPUNI ya Azam Media Limited leo imeingia Mkataba na Shirikisho la
Mpira wa miguu Tanzania (TFF)
wenye thamani ya Sh.Bilioni 2 kurusha matangazo ya moja kwa moja ya Ligi Kuu ya Wanawake
Tanzania na Ligi Kuu ya Vijana wa
umri chini ya miaka 20.

Zoezi hilo limefanyika Ofisi za makao
Makuu ya Azam Media Ltd eneo la
TAZARA, Dar es Salaam upande wa
TFF ukiwakilishwa na Rais wake,
Jamal Malinzi na Azam Media
wakiwakilishwa na Mtendaji wake
Mkuu, Muingereza Rhys Torrington.

Akizungumza katika hafla hiyo fupi,
Torrington amesema Mkataba huo ni
wa miaka mitano na lengo laoe ni
kuendelea kusaidia kuinua michezo
Tanzania.

"Baada ya mafanikio ya awali tukiwa
na Ligi Kuu ya Wanaume na
mashindano mengine, sasa tunapiga
hatua nyingine hatika jitihada zetu
kuchangia maendeleo ya soka nchini
kwa kuingia mikataba ya ligi hizi
mbili,"amesema Torrington.

Kwa upande wake, Malinzi amesema
kwamba Ligi Kuu ya Wanawake
itaanza kwa kushirikisha klabu 10
Agosti mwaka huu na Ligi ya U20
itashirikisha klabu zote za Ligi Kuu ya Wanaume.

"Na Ligi ya U20 itachezwa sambamba na Ligi Kuu ya wanaume, kabla ya mechi za timu za wakubwa,
zitatangulia mechi za vijana. Na kila
timu itasafirisha timu yake ya vijana
kwa mechi za mikoani. Itakuwa ligi
kamili na yenye kanuni
madhubuti,"amesema Malinzi.

MUSSA MGOSI ATAJA VITU VIWILI AMBAVYO HAWEZI KUVISAHAU MSIMU HUU

Na Haji balou
Mshambuliaji mkongwe wa Simba Musa Hassan Mgosi kupitia Simba news amesema kuna vitu viwili ambavyo hatavisahau baada ya msimu huu wa VPL kumalizika huku klabu yake ikiangukia nafasi ya tatu kwenye msimamo wa ligi.

“Kuna mambo mengi ambayo yametokea kwenye msimu wa 2015-16 lakini kwa upande
wangu, kuna vitu viwili ambavyo siwezi kuvisahau”, amesema Mgosi ambaye hakupata nafasi ya kutosha kucheza msimu huu kwenye kikosi cha Simba.

“Kitu cha kwanza ni mechi kati yetu ya nusu fainali ya FA Cup dhidi ya Coastal Union. Coastal Union haikuwa timu ya kututoa sisi
lakini kwenye mpira hakuna udogo wa ukubwa wa timu inategemea na maandalizi ya timu, iliniuma sana kutolewa na timu kama Coastal”.

“Kitu kingine kilikuwa ni kufungwa mechi zetu zote mbili na watani wetu wa jadi Yanga, katika uwepo wangu Simba muda wote, hatujawahi
kufungwa na Yanga mara mbili mfululizo kwenye msimu mmoja, niliumia sana”.