SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Mar 8, 2016

ULIMWENGU YUPO FITI KUCHEZEA TAIFA STARS DHIDI YA CHAD

NA Haji balou
MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa
Tanzania, Thomas Emmanuel
Ulimwengu (pichani) yuko fiti kabisa sasa na atakuja nchini
kuichezea nchi yake mechi mbili za
Kundi G kufuzu Fainali za Kombe la
Mataifa ya Afrika mwakani.

Na klabu yake, Tout Puissant
Mazembe imemruhusu kuja Dar es
Salaam kuugana na Taifa Stars kwa
ajili ya michezo miwili ya nyumbani
na ugenini dhidi ya Chad.

TPM imemuambia Ulimwengu,
maarufu kama Rambo mbele ya
mashabiki wa Lubumbashi kwamba
atakwenda Dar es Salaam mara tu
baada ya mchezo wa marudiano wa
Raundi ya Kwanza Ligi ya Mabingwa
Afrika dhidi ya St George ya Ethiopia
Jumapili ya Machi 20 mjini Lubumbashi.

Taifa Stars watakuwa wageni wa
Chad Jumatano ya Machi 23 mjini
N'Djamena, kabla ya timu hizo
kurudiana Machi 28 mjini Dar es
Salaam.

Ulimwengu aliumia mguu akiichezea
Mazembe dhidi ya St Eloi Lupopo
Februari 17, mwaka huu katika Ligi
Kuu ya DRC timu hizo zikitoka sare
ya 0-0 na akacheza kwa dakika 12 za
mwisho huku akichechemea Februari 20 katika mchezo wa Super Cup ya CAF dhidi ya Etoile du Sahel ya Tunisia mjini Lubumbashi, wenyeji
wakishinda 2-1.

MAHREZ ANAWEZA KUJIUNGA NA TIMU HII MSIMU UJAO

NA Haji balou
Leicester City wanaweza kuwa wamebakiwa na mechi 9 tu za kumuona star wao Riyad Mahrez
akifanya mazuri kwenye club hiyo. Ikifika muda wa usajili kutakua na vita kubwa kwa club mbalimbali kubwa kutaka kuchukua wachezaji
kutoka Leicester City ambao wanakikosi kizuri kwa ushirikiano na hata mchezaji kwa mmoja mmoja.

Boss wa Barcelona Luis Enrique amemuweka kwenye wish list yake mchezaji wa Leicester City ambapo angependa kumuona anajiunga na
club yake msimu ujao.

Hakuna mchezaji asiyependa kucheza na kikosi kinachoshinda makombe kama Barecelona.
Hivyo basi kutakua na hamu kubwa kwa Mahrez kutaka kujiunga na kikosi hicho ambapo atafaidika kiuchumi na kimchezo pia.

Taarifa zinasema kwamba Enrique
amemuangalia sana mchezaji huyu mwenye miaka 25 na kuvutiwa sana na style yake ya kufunga. Kipindi kijacho cha usajili kinategemewa kuwa na movement kubwa sana
ya wachezaji na makocha kwenda club mbali mbali.