SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

May 15, 2016

KOMBAINI FC YAICHAPA LIKONGOWELE FC


Na Haji balou






Ligi ya Mbuzi Vijana Cup wilaya ya Liwale imeendelea tena hii leo  kwa mchezo mmoja kupigwa  katika uwanja wa shule ya msingi Muungano kwa Kombaini fc kuibuka na ushidi  wa  3-1 dhidi  ya  Likongowele fc.

Magoli ya Kombaini  fc yamefungwa na Mpilipili katika dakika ya  18 Sudi mbwana katika dakika ya 45 goli la mwisho limefungwa na zuberi zuberi dakika ya 65 goli la kufutia machozi kwa upande wa Likongowele fc limefungwa na Faraji Manyai katika dakika ya 25.

Baada ya mchezo kumalizika kapteni wa Likongowele Ramadhani mmango amesema kuwa kwa upande wao hawakucheza vizuri na timu yao ilikosa maelewano hasa eneo la kiungo.

Pia kocha wa Kombaini Haji mkutuma alisema mchezo ulikuwa mzuri lakini refa hakuwa katika upande wao ingawa wameibuka na ushindi wa goli 3-1 na malengo yao ni kushika nafasi ya kwanza katika kundi lao ili kusonga  mbele katika mashindano.