SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Feb 22, 2015

PRISONS YAITULIZA AZAM CHAMANZI

Sare ya bila kufungana dhidi ya Prisons ya Mbeya imezidi kuibana Azam FC.

Sasa imefikisha pointi 27 baada ya mechi hiyo ya Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam, leo.

Yanga inaendelea kuongoza ikiwa na pointi nne zaidi ya Azam FC ikiwa ni baada ya kuitwanga Mbeya City kwa mabao 3-1.

Azam imecheza mechi 15, imeshinda saba, sare sita na wamepoteza mbili.

HUU NDIO MSIMAMO LIGI KUU ENGLAND

 Huu ndio msimamo ligi kuu England baada ya mechi za leo jumapili kuisha
 
Pos
Team P            W         D         L           GS      GA      +/-            Pts
1 Chelsea FC Chelsea 26 18 6 2 56 22 +34 60
2 Manchester City FC Manchester City 26 16 7 3 56 25 +31 55
3 Arsenal FC Arsenal 26 14 6 6 49 29 +20 48
4 Manchester United FC Manchester United 26 13 8 5 44 26 +18 47
5 Southampton FC Southampton 26 14 4 8 38 19 +19 46
6 Liverpool FC Liverpool 26 13 6 7 38 29 +9 45
7 Tottenham Hotspur FC Tottenham Hotspur 26 13 5 8 41 36 +5 44
8 West Ham United FC West Ham United 26 10 9 7 38 30 +8 39
9 Swansea City AFC Swansea City 26 10 7 9 30 34 -4 37
10 Stoke City FC Stoke City 26 10 6 10 30 34 -4 36
11 Newcastle United FC Newcastle United 26 8 8 10 31 42 -11 32
12 Everton FC Everton 26 6 10 10 33 37 -4 28
13 Crystal Palace FC Crystal Palace 26 6 9 11 28 37 -9 27
14 West Bromwich Albion FC West Bromwich Albion 26 6 9 11 24 34 -10 27
15 Hull City AFC Hull City 26 6 8 12 25 35 -10 26
16 Sunderland AFC Sunderland 26 4 13 9 22 36 -14 25
17 Queens Park Rangers FC Queens Park Rangers 26 6 4 16 27 45 -18 22
18 Burnley FC Burnley 26 4 10 12 25 44 -19 22
19 Aston Villa FC Aston Villa 26 5 7 14 13 36 -23 22
20 Leicester City FC Leicester City 26 4 6 16 24 42 -18 18

LIVERPOOL YAPATA USHINDI UGENINI

Southampton 0-2 Liverpool: Coutinho & Sterling ensure Rodgers' men march onTimu ya Liverpool imeibuka na ushindi  wa goli 2-0 ugenini dhidi ya wenyeji wao Southampton. Magoli ya Liverpool yamefungwa na  Philippe Coutinho dakika ya 3 na Raheem Sterling dakika ya 73.





EVERTON
2 - 2
LEICESTER

TOTENHAM 
2 - 2
WEST HAM UNITED


















SOUTHAMPTOM VS LIVERPOOL MAPUMZIKO MATOKEO YAPO HAPA

Premier League - all the action LIVELiverpool wakiwa ugenini wanaongoza goli 1-0 dhidi ya wenyeji wao Southamptom goli la Liverpool lilipatikana dakika ya tatu kupitia kwaPhilippe Coutinho na sasa ni mapumziko.

MWADUI FC YA JULIO BINGWA LIGI DARAJA LA KWANZA

Bao pekee lililofungwa na Kelvin Sabato limeiwezesha Mwadui FC kuibuka na ubingwa wa Ligi Daraja la Kwanza.

Mwadui FC chini ya Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ imeibuka na ushindi wa bao hilo dhidi ya African Sports ya Tanga na kutawazwa kuwa bingwa katika mechi iliyopigwa kwenye Uwanja wa Azam Complex, Chamazi jijini Dar.
SABATO AKISHANGILIA BAADA YA KUFUNGA BAO HILO PEKEE. KULIA NI BAKARI KIGODEKO AKIMPONGEZA.
Mechi hiyo iliwakutanisha vinara wa makundi ya daraja la kwanza ambao walikuwa wameishajihakikishia kucheza Ligi Kuu Bara mwaka.

Julio anayeaminika kuwa kocha mwenye maneno mengi, kikosi chake kilijitahidi kupamba na kasi ya Sports ambayo ilikuwa inaundwa na vijana wengi.
Soka lilikuwa safi na la kuvutia huku Mwadui ikitawala zaidi kutokana na wakongwe wake, Athumani Iddi ‘Chuji’, Juma Jabu, Bakari Kigodeko na wengine kuonyesha soka safi.

Hata hivyo, African Sports yenye vijana wengi pia ilionyesha soka safi.
 Mshambuliaji Ally Shiboli wa Sports naye alikuwa msumbufu sana kwa mabeki wa Mwadui lakini akatoa kali baada ya kumpiga kipa chenga lakini akashindwa kufunga akiwa amebaki na lango.




YANGA SC YAICHAPA 3-1MBEYA CITY



Yanga SC ya Dar es salaam  imeifunga 3-1 Mbeya City katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya. Mabao ya Yanga yamefungwa na Simon Msuva, Mrisho Ngassa na Haruna Niyonzima. Sasa yanga ipo kileleni mwa ligi kuu England.

CHRISTOPHER ALEX MASSAWE AFARIKI DUNIA



Na Omary Katanga, DAR ES SALAAM
CHAMA cha Soka Dar es Salaam (DRFA), kimeeleza kusikitishwa kwake na kifo cha mchezaji kiungo wa zamani wa klabu ya Simba na timu ya taifa, Taifa Stars, Christopher Alex Masawe, kilichotokea leo (Februari 22, 2015), katika Hospitali ya Mirembe Dodoma.
Mwenyekiti wa DRFA, Almas Kasongo, amemuelezea marehemu Christopher kuwa ni mchezaji aliyevuma enzi za uhai wake na kuiletea heshima kubwa klabu yake ya Simba na Taifa Kwa ujumla, pale walipofanikiwa kuisukumiza nje ya michuano ya afrika klabu ya Zamalek na kuivua ubingwa miamba hiyo ya soka ya kaskazini mwaka 2003.
Christopher Alex Massawe amefariki dunia leo
Christopher Alex Massawe (wa tatu kutoka kulia waliosimama) akiwa na kikosi cha Simba SC mwaka 2003 

Kiungo huyo aliyeanza kuvuma katika miaka ya 2000,amefariki dunia kutokana na kusumbuliwa kwa muda mrefu na ugonjwa wa kifua kikuu (TB).
Marehemu Christopher Alex, alizaliwa Septemba 12 mwaka 1975,na kupata elimu yake ya msingi katika shule ya msingi Uhuru na kumaliza katika shule ya Chamwino huko Dodoma mwaka 1993,na alianza kucheza mpira kwenye timu ya Daraja la nne Chamwino UTD na baadaye daraja la tatu akiwa na kikosi cha Aston Villa nayo ya Dodoma.
Mwaka 1999-2001 ameitumikia klabu ya CDA ya Dodoma,kabla ya kutimkia klabu ya Reli mwaka 2002 na baadaye kujiunga na wekundu wa msimbazi Simba,Marehemu ameacha mtoto mmoja aitwaye Alex.
Kasongo, kwa niaba ya kamati ya utendaji ya DRFA, wametoa ubani wa shilingi laki mbili (200,000/=) kwa familia ya marehemu,na kuwataka mashabiki wa soka na watanzania kwa ujumla kuungana pamoja katika kuifariji familia hiyo kwenye kipindi hiki kigumu cha majonzi.

STAND PUNGUFU WAILAZA SIMBA 1-0



Timu ya Simba imepoteza mchezo wake wa leo ugenini dhidi ya Stand United ya Shinyanga kwa goli 1-0 goli lililofungwa na mnigeria Chiddy katika dakika za mwanzo za kipindi cha kwanza. Huu ni mchezo wa kwanza kwa Simba kufungwa nje ya jiji la jiji la Dar es saalam.
Mchezaji Yasin Mustapha wa Stand United alipewa kadi nyekundu baada ya kumchezea rafu mbaya mchezaji wa Simba Abdi Banda, na mchezaji Abuu Ubwa wa Stand United alipewa kadi nyekundu dakika za mwisho kwa kosa la kupoteza muda