SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Jan 13, 2016

SAMATTA KUTIKISA ZANZIBAR LEO


MWANASOKA Bora Anayecheza
Afrika, Mbwana Ally Samatta kesho
atatambulishwa kwa Wazanzibari
wakati wa mchezo wa fainali ya
Kombe la Mapinduzi, kati ya Mtibwa
Sugar na URA ya Uganda.
Katibu wa Kamati ya Kombe la
Mapinduzi, Mwinyimvua Khamis
ameiambia BIN ZUBEIRY SPORTS –
ONLINE leo kwamba Samatta
atawasili kesho Uwanja wa Amaan na
kusalimia mashabiki pamoja na kuinua
tuzo yake kuinoyesha.
Samatta, mshambuliaji wa kimataifa
wa Tanzania na klabu bingwa Afrika,
TP Mazembe ya DRC, anatarajiwa
kuketi pamoja na viongozi wakuu wa
serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar
kesho wakati mchezo huo ukiendelea.

Ikumbukwe ni jana tu Samatta
amepatiwa viza ya kwenda Ubelgiji
kujiunga na klabu ya KRC Genk ya
Ligi Kuu ya nchini humo.
Ingawa bado klabu yake, TP Mazembe
haijatangaza rasmi, lakini taarifa
zinasema mwishoni mwa mwaka jana,
Rais wa klabu hiyo ya DRC, Moise
Katumbi alifikia makubaliano na klabu
hiyo ya Ubelgiji juu ya biashara ya
mchezaji huyo.
Na kwa Samatta kwa kupatiwa viza
ya kwenda Ubelgiji, maana yake
anahitimisha miaka yake minne ya
kuishi Lubumbashi, yalipo makao
makuu ya TPM, klabu bingwa ya
Afrika mara ya tano.
Samatta aliyejiunga na TPM mwaka
2011 akitokea Simba SC aliyoichezea
kwa nusu msimu, akitokea African
Lyon, anaondoka Mazembe baada ya
kuichezea mechi 103 na kuifungia
mabao 60.
Kijana huyo wa umri wa miaka 24,
anaondoka Mazembe akiiachia taji la
Ligi ya Mabingwa Afrika, huku naye
akiibuka mfungaji bora wa michuano
hiyo na kutwaa tuzo ya Mchezaji Bora
Anayecheza Afrika.
Ikumbukwe ni jana tu Samatta
amepatiwa viza ya kwenda Ubelgiji
kujiunga na klabu ya KRC Genk ya
Ligi Kuu ya nchini humo.
Ingawa bado klabu yake, TP Mazembe
haijatangaza rasmi, lakini taarifa
zinasema mwishoni mwa mwaka jana,
Rais wa klabu hiyo ya DRC, Moise
Katumbi alifikia makubaliano na klabu
hiyo ya Ubelgiji juu ya biashara ya
mchezaji huyo.
Na kwa Samatta kwa kupatiwa viza
ya kwenda Ubelgiji, maana yake
anahitimisha miaka yake minne ya
kuishi Lubumbashi, yalipo makao
makuu ya TPM, klabu bingwa ya
Afrika mara ya tano.
Samatta aliyejiunga na TPM mwaka
2011 akitokea Simba SC aliyoichezea
kwa nusu msimu, akitokea African
Lyon, anaondoka Mazembe baada ya
kuichezea mechi 103 na kuifungia
mabao 60.
Kijana huyo wa umri wa miaka 24,
anaondoka Mazembe akiiachia taji la
Ligi ya Mabingwa Afrika, huku naye
akiibuka mfungaji bora wa michuano
hiyo na kutwaa tuzo ya Mchezaji Bora
Anayecheza Afrika.