SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Apr 29, 2015

VAN PERSIE ‘AFUFUKA’, APIGA MBILI MAN UNITED IKISHINDA 4-1 ENGLAND

MSHAMBULIAJI Robin van Persie usiku huu amefunga mabao mawili katika ushindi wa 4-1 wa  U21 ya Manchester United dhidi ya vijana wenzao wa Fulham Uwanja wa Craven Cottage.
Van Persie ambaye amekuwa nje ya Uwanja tangu Februari kutokana na majeruhi, alifunga mabao hayo katika dakika za 13 na 80, huku mabao mengine ya United yakifungwa na Joe Rothwell dakika ya 20 na 43.
Mholanzi huyo, Van Persie alirejea uwanjani kikosi cha kwanza cha United Jumapili timu hiyo ikifungwa 3-0 na Everton katika LIgi Kuu ya England.
Kikosi cha Fulham kilikuwa: Norman, Donnelly, Buatu, Baba, Sheckleford, Mesca, Edun/de la Torre dk67, Smile, Evans, Plumain, Redford/Humphreys dk60.
Manchester United: Lindegaard, Love, Blackett, Thorpe, Kellett, Rothwell/Willock dk81, Goss/Fletcher dk88, Grimshaw, Pereira, Van Persie/Weir dk81 na Januzaj.
Van Persie made an appearance for Manchester United Under 21s away at Fulham on Tuesday night
Van Persie akipongezwa na wenzake baada ya kufunga mabao mawili katika ushindi wa 4-1 wa U21 ya Manchester United dhidi ya Fulham usiku wa Jumanne

FERGUSON: RONALDO ANAWEZA KUNG'ARA POPOTE, HATA MILLWAL, QPR... MESSI NI WA BARCELONA TU

KOCHA wa zamani wa Manchester United, Sir Alex Ferguson ametaja sababu za wakati wote kumuona Cristiano Ronaldo yuko juu ya Lionel Messi wakati anazungumza na John Parrott wakicheza pool table, maarufu pia kama snooker.
Kocha huyo mwenye mafanikio makubwa zaidi katika historia ya soka ya Uingereza amezungumza na Parrott na mtangazaji Hazel Irvine katika mahojiano maalum ya BBC ya michuano ya Ubingwa wa Dunia Crucible.
Ferguson amesema wakati wote anaulizwa nani ni mchezaji bora duniani?, kabla ya kufafanua kwa nini humchagua mchezaji wake wa zamani United dhidi ya nyota wa Barcelona.
Former Manchester United amanger Sir Alex Ferguson (left) speaks with John Parrott over a frame of snooker
Kocha wa zamani wa Manchester United, Sir Alex Ferguson (kushoto) akizungumza na John Parrott kwenye meza ya snooker

Ferguson anaamini Cristiano Ronaldo ni mzuri zaidi ya Lionel Messi kwa sababu anaweza kufunga akiwa na timu yoyote

"Watu wengi kwa urahisi tu wanasema Messi na huwezi kukataa maoni yao,"alimuambia bingwa wa mwaka 1991 wa Snooker duniani.
"Ronaldo anaweza kuchezea Millwall, QPR, Doncaster Rovers, (timu moja) yoyote, na akafunga hat-trick. Sina uhakika kama Messi anaweza kufanya hivyo. Ronaldo yuko fiti mno, ana kasi, mzuri wa kurukia mipira ya juu kupiga kichwa na mkali.
"Nafikiri Messi ni mchezaji wa Barcelona,' amesema.
Kocha huyo wa zamani wa United wakati wote amekuwa na uhusiano mzuri na nyota huyo anayecheza Real Madrid kwa sasa tangu aondoke Old Trafford, na Ferguson anampa heshima Mreno huyo sambamba na Ryan Giggs na Paul Scholes kama wachezaji bora duniani aliowahi kuwafundisha.

MESSI, SUAREZ KILA MMOJA APIGA MBILI BARCA IKIUA 6-0

TIMU ya Barcelona imezidi kuukaribia ubingwa wa Ligi Kuu Hispania, La LIga baada ya leo kuifunga Getafe mabao 6-0 Uwanja wa Nou Camp na sasa inawazidi Real Madrid kwa pointi tanio.
Lionel Messi aliwafungia wenyeji bao la kwanza dakika ya 10 kwa mkwajunwa penalti baada ya Luis Suarez kuangushwa. 
Luis Suarez akaifungia Barca bao la pili dakika ya 25, kabla ya Neymar Jnr kufunga la tatu dakika tatu baadaye na hilo kuwa bao la 100 kwa timu yake hiyo msimu huu.
Xavi akaifungia bao la nne timu ya Luis Enrique dakika ya 30, kabla ya Suarez kufunga lake la pili katika mchezo huo na la tano kwa Barca dakika ya 40 na Messi akafunga bao lake la 48 msimu huu la sita kwa timu yake dakika mbili tu baada ya kuanza kipindi cha pili.
Kikosi cha Barcelona kilikuwa: Bravo, Alves/Montoya dk68, Bartra, Mathieu, Adriano, Busquets, Xavi/Pedro dk59, Rafinha, Suárez, Messi na Neymar.
Getafe: Guaita, Alexis, Lago, Velazquez, Lacen, Arroyo, Pedro Leon/Escudero dk76, Baba, Juan Rodriguez/Felip dk65, Freddy na Emi.
Neymar celebrates with Lionel Messi after giving Barcelona a 3-0 lead at the Nou Camp on Tuesday night
Neymar akisherehekea na Lionel Messi baada ya kuifungia Barcelona bao la tatu usiku huu

Apr 28, 2015

KURASA ZA MWANZO NA ZA MWISHO ZA MAGAZETI YA MICHEZO LEO JUMANNE ZIPO HAPA

DSC01886 DSC01887 DSC01888 DSC01889 DSC01890 DSC01891

TAMBWE AZIDI KUWAUMIZA ROHO SIMBA

Tambwe akipewa mpira
AMISSI Tambwe ameendelea kuonesha thamani yake na kuwadhihirishia Simba kuwa yeye ni mfungaji hatari baada ya jana kupiga magoli matatu ‘hat-trick’ katika ushindi wa magoli 4-1 dhidi ya Polisi Moro.
Yanga walichukua ubingwa wa ligi kuu Tanzania bara msimu wa 2014/2015 baada ya ushindi wa jana wakifikisha pointi 55 ambazo haziwezi kufikiwa na timu yoyote.
Mwaka jana Simba walimuacha Tambwe katika mazingira ya utata akiwa ndiye mfungaji bora na dakika za mwisho za dirisha dogo la usajili desemba mwaka jana Yanga wakamsajili kwa kumpa mkataba wa mwaka mmoja.
Katika mechi tatu zilizopita, Tambwe amefunga magoli nane na kufikisha magoli 14 katika msimu huu mgumu wa ligi kuu.
Alifunga manne katika ushindi wa 8-0 dhidi ya Coastal, akatia kambani moja kwenye ushindi wa 3-2 dhidi ya Stand United na jana akapiga tatu dhidi ya Polisi Moro.
Baada ya kufanikiwa kwa muda mfupi ndani ya Yanga, Tambwe amesema anafurahia maisha ndani ya Yanga na ataendelea kufanya vizuri.
“Nashukuru nimefunga ‘Hat-trick’ yangu ya pili msimu huu, nikiwa Simba nilifunga ‘hat-trick’ mbili pia, kwangu haya ni mafanikio, nilipochukua kiatu cha dhahabu mwaka jana nilisikitika kuachwa na Simba, kichwa changu hakikuwa sawa”, Amesema Tambwe na kusisitiza: “Leo hii (jana) nachukua ubingwa Yanga nikifunga magoli muhimu, namshukuru Mungu, wachezaji wenzangu, mashabiki na viongozi, wanaonesha upendo mkubwa kwangu”.

MSUVA AZUNGUMZIA GOLI LAKE LINALO FANANA NA LA VAN PERSIE

NgassanaMsuva
SIMON Happygod Msuva amesema anajisikia furaha kuchukua ubingwa huku goli lake alilofunga kwa kichwa dhidi ya Ruvu Shooting likijadiliwa mno kwenye mitandao ya kijamii na kufananishwa na alilofunga mshambuliaji wa Manchester United na Uholanzi, Robin van Persie kwenye fainali za kombe la dunia mwaka jana nchini Brazil.
“Watu wanasema nilifunga kama Robin Van Persie, wanajadili sana kwenye mitandao, haya ni mafanikio kwangu, juhudi ndio siri ya mafanikio” Amesema Msuva.
Winga huyo anayeongoza orodha ya wafungaji akiwa amefumania nyavu mara 17 msimu huu akifuatiwa na Amissi Tambwe mwenye magoli 14 ameongeza kuwa ubingwa waliopata anafurahi kuchangia kwa kiasi kikubwa na ataendelea kufanya vizuri.
“Huu ni mwanzo tu, kila siku najifunza na kupunguza makosa, tuna kocha mzuri, tunaamini tutafanya vizuri zaidi siku zijazo tukianzia na mechi ijayo dhidi ya Etoile du sahel”. Amesema Msuva.

SHANGWE ZA UBINGWA YANGA RAHA TUPU WACHEZAJI, MAKOCHA HADI MASHABIKI





JOHN TERRY 'ANAVYOMSUTA' BENITEZ AELEKEA KUCHEZA MECHI 38 ZA MSIMU BILA TATIZO

MIAKA miwili ilitopita, kocha Rafa Benitez alipokuwa wa Chelsea mustakabali wa beki John Terry ulikuwa shakani Stamford Bridge.
Aprili mwaka 2013, kocha huyo Mspanyola alisema kwamba hawezi kuendelea kumchezesha mechi mbili kwa wiki na uamuzi huo wa utata ulitokana na maumivu ya goti ya mwanasoka huyo wa zamani wa kimataifa wa England. 
Terry alichezeshwa mechi 14 tu katika msimu wa 2012-2013 kwenye klabu hiyo kipenzi. Leo mwaka 2015, Nahodha huyo wa Blues anakarinia kuinua taji la Ligi Kuu ya England akiwa ametoa mchango wake katika mechi kati ya 33 ilizocheza Chelsea hadi sasa.
Na sasa mkongwe huyo anaelekea kucheza mechi zote 38 za msimu wa Ligi Kuu Chelsea. hakika ni jambo la kujivunia kwake.
Chelsea captain John Terry is on course to appear in all 38 Premier League matches for his side this season
Nahodha wa Chelsea, John Terry anaelekea kucheza mechi zote 38 za Ligi Kuu msimu huu

Apr 27, 2015

TAMBWE AWAGARAGAZA SIMBA SC ‘KIZIMBA CHA TFF’, WATAKIWA KUMLIPA MAMILIONI YAKE, VINGINEVYO WATAKOMA!

Na Princess Asia, DAR ES SALAAM
MSHAMBULIAJI Amissi Tambwe ameshinda kesi dhidi ya klabu yake ya zamani, Simba SC juu ya mafao yake.
Simba SC ilimtema mshambuliaji huyo wa Burundi ndani ya Mkataba, lakini ikashindwa kumlipa, naye akafungua kesi Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Kesi hiyo jana imesikilizwa mbele ya Kamati ya Hadhi za Wachezaji chini ya Mwenyekiti wake, Richard Sinamtwa na Tambwe ameshinda.  
Madai ya Tambwe jumla ni dola za Kimarekani 7,000 (Sh. Milioni 14 za Tanzania), kati ya hizo 1,000 zikiwa ni mshahara wa mwezi mmoja na nyingine za kuvunjia Mkataba.
Tambwe akiwa na Wakili Frank Macha jana jioni ofisi za TFF, Uwanja wa Karume, Dar es Salaam 

Simba SC wamepewa hadi Aprili 30 kuwa wamemlipa Tambwe dola 5,000 na nyingine wamalizie Mei 10, mwaka huu- na wakishindwa kufanya hivyo watakatwa fedha zote mara moja katika mapato ya mechi zao.
Tambwe aliongozana na Wakili wa klabu yake, Yanga SC, Frank Macha wakati Simba SC iliwakilishwa na Katibu wake, Stephen Ally.

MAGAZETI YA MICHEZO LEO 27 APRIL YAPO HAPA

DSC01841 DSC01842 DSC01843 DSC01844 DSC01845 DSC01846

GERRARD, LAMPARD WAPEWA 'HESHIMA YAO' ENGLAND

VIUNGO  wa zamani wa kimataifa wa England, Steven Gerrard na Frank Lampard usiku huu wamepewa tuzo kutokana na mchango wao mkubwa katika Ligi Kuu ya England.
Wawili hao wanaohamia Marekani mwishoni mwa msimu baada ya kucheza England kwa muda mrefu, wamepewa tuzo hizo na Chama cha Wachezaji wa Kulipwa (PFA) usiku huu.
Wote Gerrard na Lampard wanapewa heshima ya wachezaji wa 'kizazi cha dhahabu' England na kwa pamoja wameichezea timu ya taifa mechi 220 baina yao.
Steven Gerrard and Frank Lampard (right) were honoured with the merit award at the PFA awards on Sunday
Steven Gerrard na Frank Lampard (kulia) wamepewa tuzo na PFA usiku wa jana.

CHICHARITO AMSUTA HENRY, AIPIGIA MBILI REAL IKICHAPA MTU NNE LA LIGA

NYOTA ya mshambuliaji Javier Hernandez ‘Chicharito’ imeendelea kung’ara baada ya kuifungia mabao mawili Real Madrid ikiibuka na ushindi wa 4-2 dhidi ya wenyeji Celta Vigo Uwanja wa Balaidos katika mchezo wa La Liga usiku wa kuamkia leo.
Real sasa inapunguza pengo la idadi ya pointi inazozidiwa na vinara wa La Liga, Barcelona hadi kubaki pointi mbili (81-79), timu zote zikiwa zimecheza mechi 33.
Wenyeji ndiyo waliokuwa wa kwanza kupata bao dakika ya tisa kupitia kwa Nolito, kabla ya Real kusawazisha kupitia kwa Toni Kroos dakika ya 16 na Chicharito akafunga la pili dakika ya 24.
Hata hivyo, wenyeji wakasawazisha tena dakika nne baadaye kupiria kwa Mina, kabla ya James Rodriguez dakika ya 43 na Chicharito dakika ya 69 kuifungia Real bao la tatu na la nne.
Chicharito ndiye aliyeifungia Real bao pekee la ushindi katika Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Atletico Madrid, lakini Nahodha wa zamani wa Arsenal, Thierry Henry akamkandia ‘kinoma’.
Alisema alishangilia kama ametwaa Kombe la Dunia- na alishangilia bila ya mtu aliyemoa pasi, Ronaldo ambaye ndiye alifanya kazi kubwa. Na Henry ambaye sasa ni mchambuzi wa Sky Sports, akasema Chicharito anayecheza kwa mkopo kutoka Manchester United, hakucheza vizuri na hana uhakika kama atapewa nafasi zaidi kikosini Real. 
Javier Hernandez scored two more important goals for Real Madrid as they look to keep up with Barcelona in the quest for the La Liga crown
Javier Hernandez akishangiia baada ya kuifunjgia Real Madrid mabao mawili jana 

HAZARD MCHEAJI BORA WA MWAKA ENGLAND


Eden Hazard with the PFA Player of the Year trophy following a ceremony in central London on Sunday
Na Anwar Binde,
Baada ya kusubiri kwa misimu miwili hatimae Eden Hazard wa Chelsea ameibuka mchezaji bora wa mwaka wa England na kutwaa tuzo ya PFA.
Hazard mwenye umri wa miaka 24 amefunga mabao 13 na na kusaidia wafungaji (assists) 8 katika michezo 33 ya ligi kuu ya nchi hiyo na kuisaidia timu yake kushika ususkani katika msimamo wa ligi.
Naye Harry Kane mwenye umri wa miaka 21 ameibuka kidedea kwa kunyakua tuzo ya mchezaji bora chipukizi huku naye Ji So-Yun wa Chelsea akiibuka mshindi kwa upande wa wanawake.
Hazard ambaye msimu uliopita aliibuka mshindi kwa upande wa chipukizi alikabidhiwa tuzo yake katika hoteli ya Grosvenor jijini London jana Jumapili. ” ninafuraha sana. Nataka siku moja niwe mjichezaji bora kabisa  na nilichofanya msimu huu ni kucheza vizuri na timu yangu imecheza vizuri sana” alisema Hazard baada ya kupokea tuzo hiyo. “sijui kama nastahili kushinda lakini jambo hili ni zuri kwangu. Ni jambo zuri kupigiwa kura na wachezaji kwasababu wanajua kila kitu kuhusu mpira” aliongeza mchezajia huyo.
“Tunaukalibia ubingwa labda hii ndio funguo ya kuelekea ubingwa huo,msimu uliopita tulimaliza nafasi ya tatu lakini kwa sasa ni tofauti ,tunayo nafasi na uwezo wa kuwshinda taji msimu huu”alisema hazard
Hazard alieisaidia timu yake kupata pointi zote 3 dhini ya Manchester united kwa kufunga goli pekee katika mchezo uli[igwa pale Stanford Bridge pia ametajwa katika kikosi cha wachezaji bora 11 wa kulipwa katika ligi kuu ya uingereza huku akiambatana na wachezaji wengine watano kutoka Chelsea ambao ni John Terry,Gary Cahil,Branislav Inanovic, Nemanja Matic na Diego Costa.

Apr 22, 2015

KURASA ZA MWANZO NA ZA MWISHO ZA MAGAZETI YA MICHEZO LEO JUMATANO ZIPO HAPA


 DSC01628 DSC01629 DSC01630 DSC01631 DSC01632

BARCA WAITAFUNA UPANDE WA PILI PSG, WATINGA NNE BORA ULAYA KIULAINI

Neymar (top) celebrates with Brazilian compatriot Dani Alves after scoring his and Barcelona's second goal of the night
Neymar (juu) akishangilia na Mbrazil mwenzake, Dani Alves baada ya kuifungia mabao yote Barcelona jana katika ushindi wa 2-0 dhidi ya PSG ya Ufaransa katika Robo Fainali ya pili Ligi ya Mabingwa jana Uwanja wa Camp Nou. Barca sasa inasonga mbele kwa ushindi wa jumla wa 5-1, baada ya awali kushinda 3-1 Paris.

BAYERN MUNICH WATINGA NUSU FAINALI LIGI YA MABINGWA ILE KIBABE HASWA


Muller lets out a roar in celebration and is congratulated by fellow goalscorer Thiago as the Bavarians took full control of Tuesday's tie
Mshambuliaji wa Bayern Munich, Thomas Muller akishangilia na mchezaji mwenzake, Thiago baada ya ushindi wa 6-1 dhidi ya FC Porto katika mchezo wa marudiano wa Robo Fainali Ligi ya Mabingwa Ulaya jana Uwanja wa Allianz Arena mjini Munich, Ujerumani. Mabao mengine ya Bayern yalifungwa na Thiago, Boateng, Lewnadowski mawili na Alonso 88, wakati la Porto lilifungwa na Martinez,dakika ya 73. The Bavarians sasa wanasonga mbele kwa ushindi wa jumla wa 7-4 baada ya awali kufungwa 3-1 mjini Munich.

Apr 20, 2015

KURASAZAMWANZO NA ZA MWISHO ZA MAAZETI YA MICHEZO LEO APRIL 20


DSC01539
DSC01540
DSC01541
DSC01542
DSC01543
DSC01544
DSC01545
DSC01546

KIUNGO ‘BABU KUBWA’ ANAYELIPWA MILIONI 44 KWA MWEZI TAYARI KUTUA YANGA SC

Na Mahmoud Zubeiry, DAR ES SALAAM
KIUNGO anayelipwa dola 25,000 za Kimarekani kwa mwezi Etoile du Sahel ya Tunisia, (zaidi ya Sh. Milioni 44 za Tanzania), Mcameroon Franck Kom amesema yuko tayari kutua Yanga SC iwapo wataweza kumlipa mshahara huo.
Kom aliwapoteza kabisa viungo wa Yanga Jumamosi katika mchezo wa kwanza hatua ya 16 Bora Kombe la Shirikisho Afrika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam timu hizo zikienda sare ya 1-1.  
Akizungumza na BIN ZUBEIRY juzi mjini Dar es Salaam, kiungo huyo aliyekuwa akiichezesha vyema timu yake, alisema kwamba anaweza kuja kucheza Tanzania.
Baada ya mechi Kom alikwenda kwenye benchi la Yanga kusalimiana na wachezaji wa timu hiyo na akatumia muda zaidi kuzungumza na kiungo wa DRC, Mbuyu Twite.
Frank Kom kushoto akizungumza na BIN ZUBEIRY juzi baada ya mechi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam

Kom alionyesha kumpenda Mbuyu Twite japo ndiyo walikuwa wanakutana kwa mara ya kwanza siku hiyo na wakapeana mawasiliano.
Alipoulizwa kama anaweza kujiunga na Yanga ikimhitaji, Kom alisema; “Kwa nini hapana, ninaweza kama wataweza kunilipa kama ninavyolipwa Etoile,”alisema mchezaji huyo ambaye wakala wake ni kampuni ya Smart Sports Management inayomilikiwa na Jacques Dongmo. Aidha, Kom aliyetua Etoile mwaka 2011 akitokea Panthere du Nde inayotumia jezi kama za Yanga kijani na njano, ya kwao Cameroon aliyoanza kuichezea mwaka 2009 amesema ndoto zake kubwa ni kucheza Ulaya.
Kom alitumia muda zaidi kuzungumza na kiungo Mbuyu Twite, raia wa DRC siku hiyo

“Nacheza Afrika kutafuta nafasi ya kucheza Ulaya, timu yoyote inayocheza haya mashindano ya Afrika, kama inaweza kunilipa vizuri naweza kujiunga nayo,”amesema mchezaji huyo ‘fundi’ mwenye umri wa miaka 23.
Kom ni mchezaji wa timu ya taifa ya Cameroon na alikuwepo kwenye kikosi cha timu hiyo kilichocheza Fainali za Mataifa ya Afrika mwaka 2010 nchini Angola walipotolewa Robo Fainali na Tunisia.

HANS POPPE AWACHOKOZA YANGA, AWAAMBIA; “MTAFUNGWA TUNISIA, NA PIGA, UA MSUVA ATAVAA JEZI NYEKUNDU”.

Na Hemed Kivuyo, DAR ES SALAAM
MWENYEKITI wa Kamati ya Usajili ya Simba SC, Zacharia Hans Poppe ameendeleza wimbi la kuitisha la kuitisha timu ya Yanga baada ya kutamba kwamba winga wa timu hiyo  Simon Msuva ni damu ya Simba ana atatua Msimbazi msimu ujao.
Poppe ameyasema hayo  alipokuwa akihojiwa katika kipindi cha TAMASHA LA MICHEZO kinachorushwa na kituo cha Luninga cha ITV kila siku ya jumapili saa nane kamili mchana.
Alisema kuwa  kwasasa wataendelea kuitesa timu ya ya Yanga kwakuendeleza wimbi la kuifunga kutokana na wao kuwa na mbinu nyingi za ndani na nje ya uwanja kila wanapokutana  katika michuano yeyote.
Hans Poppe kushoto amesema anaitakia dua mbaya Yanga SC ifungwe na Etoile

Amedai  sababu za kuifunga Yanga mara kwa mara wanazijua na baadhi ya mbinu hizo ni kuwavuruga na maneno kabla ya mchezo na kwamba wapo wachezaji wengi waliyowahi kuitumikia Simba ambao kwasasa wapo Yanga na hivyo kuiona Yanga kama ni Simba B.
``Wale Yanga sisi tunawaona kama ni Simba B kwakuwa wao wanaona kutuchukulia wachezaji wetu ndiyo sifa ya kutufunga jambo ambalo siyo kweli,tutaendelea kupa supu yam awe na kachumbari ya miba mpaka wawache wachezaji wetu``. Alisema Pope.
Alipoulizwa kama wamaechana na harakati za kumuhitaji winga Simon Msuva, Poppe alisema kuwa  bado wanamuhitaji Mchezaji huyo kwakuwa ni `mtoto` wao  na harakati za kumuwinda haziwezi kukoma mpaka hapo atakapovaa jezi Nyekundu za Simba.
``Yule Msuva ni kijana wetu toka siku nyingi tunajua Yule ni Simba damu na na anamapenzi na Simba hivyo lazima tuhakikishe anakuja Nyumbani kucheza Soka`. Alisema Mwenyekiti huyo wa Usajili  asiyeogopa kutoa kauli zenye kuumiza.
Hans Poppe amesema Msuva atavaa jezi nyekundu

Hakuishia hapo aliendelea kuimbea Yanga mabaya ili itupwe nje ya michuano ya Shirikisho na timu ya Etoel du Sahil ya Tunisa katika Mchezo wa marudiano utakaopigwa huko Tunisia wiki mbili zijazo.
``Mimi naomba Mungu Yanga itolewe hata kwakufungwa mabao nane,kwakuwa siipendi hii timu hata kidogo`.Aliongeza.

YANGA SC WAINGIA KAMBINI LEO, KESHO WANA STAND UNITED TAIFA

Kocha wa Yanga SC, Hans van der Pluijm
Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
YANGAS SC wanarudi kambini leo baada ya mapumziko ya siku moja, kujiandaa na mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya Stand United kesho Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Yanga SC walilazimishwa sare ya 1-1 na Etoile du Sahel ya Tunisia katika mchezo wa kwanza hatua ya 16 Bora Kombe la Shirikisho Afrika juzi Uwanja wa Taifa.
Na kabla ya kwenda Tunisia katika mchezo wa marudiano, Yanga SC watakuwa na mechi tatu za Ligi Kuu kesho na Mgambo na mwishoni ma wiki dhidi ya Polisi Morogoro na mwanzoni mwa wiki ijayo na Ruvu Shooting.
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Yanga SC, Jerry Muro ameiambia BIN ZUBEIRY jana kwamba timu inaingia kambini leo na habari njema ni kwamba, kiungo aliyekuwa majeruhi, Salum Telela amepona.
“Habari njema ni kwamba kiungo wetu tegemeo, Salum Telela aliyekuwa majeruhi amepona na atakuwepo dhidi ya Stand,”amesema. 
Telela alikosekana dhidi ya Etoile Jumamosi kutokana na maumivu ya enka aliyoyapata katika mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Mbeya City wiki iliyopita.
Kwa ujumla, Ligi Kuu itaendelea mwishoni mwa wiki kwa Mbeya City kuwakaribisha Kagera Sugar, Simba SC na Ndanda FC, Azam FC na Stand United, Polisi Morogoro na Coastal Union Jumamosi, wakati Jumapili Mtibwa Sugar wataikaribisha JKT Ruvu na Prisons watakuwa wenyeji wa Mgambo JKT.

Apr 17, 2015

KURASAZAMAGAZETIYA MICHEZO LEO IJUMAA ZIPO HAPA


DSC01431
DSC01432
DSC01433
DSC01434
DSC01435
DSC01436