SAMATTA ATUPIA GENK IKIUA 2-1

HII NDIO DROO KOMBE LA FA

SIMBA CHALII KESSY AONESHWA NYEKUNDU

MANARA APATA AJALI

MKENYA APIGA MBILI LIVERPOO IKIUA 4-1

Mar 27, 2016

JOSE MOURINHO AMEYASEMA HAYA KUHUSU MESSI

Na Haji balou
Kocha Jose Mourinho hivi karibuni amefanya mahojiano na kituo cha BT Sport na kutoa maoni yake juu ya tofauti ya kuwa na Lionel Messi
katika kikosi na kucheza dhidi yake, hasa katika Champions League.

“Messi ameshinda Champions League na makocha tofauti. Nadhani ni rahisi kushinda ukiwa nae kuliko ukicheza dhidi yake,” alisema.

Kocha huyo Mreno bado anaamini kwamba kucheza kitimu – teamwork ni muhimu.
“Mimi ni kocha wa timu ya soka Najua kwamba wakati mwingine watu wanadhani kwamba mchezaji mmoja mmoja ni muhimu kuliko timu.

Bado nafikiri kwamba timu ni muhimu zaidi kuliko chochote. Lakini ni ukweli dhahiri kwamba kuna baadhi ya wachezaji ambao wanaweza kufanya tofauti,” alisema.